Kwa mikopo ya trilioni 12 kwenye bajeti ya 2022/23, Tanzania itakuwa imefilisika kufikia 2027

Kwa mikopo ya trilioni 12 kwenye bajeti ya 2022/23, Tanzania itakuwa imefilisika kufikia 2027

Championship

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2019
Posts
5,500
Reaction score
10,616
Screenshot_20220614-224601~2.jpg


Jedwali linaonesha serikali itakopa walau trilioni 12 na pengine misaada ifikie trilioni 2.4

Makusanyo ya ndani wameweka trilioni 28 lakini uhalisia haivuki trilioni 23. Kwahiyo mikopo ni zaidi ya nusu ya makusanyo yote.

Maana yake wakikopa hivi kwenye bajeti za miaka minne ijayo (ukizingatia uwepo wa grace period) ni dhahiri kwamba itakuwa haiwezekani tena kukopesheka au kulipa deni ifikapo 2027.

Nchi itakuwa imefilisika rasmi na pengine itawekwa mnadani iuzwe vipande vipande.
 
Hapo ktk mapato ya ndani wamekosea kujumlisha

Ukirudi ktk mada sio lazima mapato yapatikane yote, bajeti ni makisio....
 
Hapo ktk mapato ya ndani wamekosea kujumlisha

Ukirudi ktk mada sio lazima mapato yapatikane yote, bajeti ni makisio....
Hesabu ulizikimbia shule? Ukijumlisha inakuja hiyo trilioni 28.

Unamaanisha hawatakopa kwa kiwango hicho? Mpaka sasa hivi nimeshaona wamekopa zaidi ya trilioni 3.5
 
Back
Top Bottom