Kwa Mkurugenzi wa BRELA: Naomba kujua namba za simu za customer care staff wako zinazofanya kazi

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725
Mheshimiwa Mkurugenzi wa BRELA,

Hizi ni zama za kidijitali, na tuko fourth industrial revolution.

Lakini hapo kwako BRELA kuna tatizo.

NImeingia mfumo wa ORS nimekwama, na hakuna namna ya kupata msaada wa haraka kutoka customer care office ya BRELA.

Nimechukua namba za customer care staff wako, lakini zote naambiwa hazifanyi kazi. Yaani zimefungwa.

Naomba namba za customer care staff wako zinazofanya kazi tafadhali.


 
Mimi nina bahati pengine maana sijawahi kukutana na usumbufu wowote nikiwa na task yoyote brela.

Hebu tueleze shida yako nini pengine tunaweza kukusaidia before hujawasiliana na brela
 
Pole sana Mama Amon namba ya kituo cha miito ni +255 (0) 222 212 800, unaweza kuwachek pia Instagram brela_tanzania WhatsApp pia wanapatikana kwa namba hii +255735331003 au kuwatumia barua pepe maoni@brela.go.tz
 
Mimi nina bahati pengine maana sijawahi kukutana na usumbufu wowote nikiwa na task yoyote brela.

Hebu tueleze shida yako nini pengine tunaweza kukusaidia before hujawasiliana na brela
User account recovery process
 
Utakuta wamejazana makada wa ccm ambao tunajua hawana akili.
 
Brela wanasumbua kinoma nina application nilikuwa nafanya mwezi sasa haijakamilika juzi kuna jamaa kafungua application akatoa na 50k siku mbili tu imekamilika daah ipo siku kuna mtu ntamshikisha pesa za takukuru
 
Brela wanasumbua kinoma nina application nilikuwa nafanya mwezi sasa haijakamilika juzi kuna jamaa kafungua application akatoa na 50k siku mbili tu imekamilika daah ipo siku kuna mtu ntamshikisha pesa za takukuru
Hiyo 50k alimpa nani sasa wakati mambo yote yanafanyika online.
 
Hiyo 50k alimpa nani sasa wakati mambo yote yanafanyika online.

Hata mimi nina maombi yapata miezi 2 sasa. ukipga wanasema hii tunairipoti. sijui tunahamisha mafile kwenda jengo jipya. yaani files za online zinahmishwa miezi 2.

Nafikiri Brela ingefutwa tu ikabuniwa kitu kingine.

Juzi nikampigia jamaa yangu kumuuliza akasema nimtumie elfu 50 kazi itakamilika kesho yake.

Navuta siku nyingine 7 ikigoma itabidi nilipie tu.

RIP Magufuli
 
RIP Magufuli hawa jamaa wanasumbua hivi ili uwape rushwa tu.
 
Poleni sana, mimi nimesajili jina la biashara siku mbili na kesho yake nikasajili kampuni, baada ya siku tatu wakanitumia marekebisho ya kufanya na nilipofanya marekebisho nika upload tena documents, baada ya siku nne wakanitumia cheti cha usajili. Sikutoa chochote hata mia na maombi yote niliyafanya online nikiwa mkoani.
 
Acha unafiki wewe ni kishoka wao,huwezi kusajili kampuni brela kwa siku 4
INAWEZEKANA mkuu, usipinge. Hata mimi nimeshuhudia tena bila kutoa hata mia kwa yeyote. Hakikisha tu documents zako zipo sawa.
Labda iwe ilikua bahati yangu na wewe kucheleweshwa ilikua bahati yako
 
Hili nadhani kilio kimewafikia, nilisikia za makoridoni kuwa BRELA itabadilishwa naman ya uendeshaji hivi karibuni
 
Hiyo usilipe kwa ubaya lipa kwa wema
Brela wanasumbua kinoma nina application nilikuwa nafanya mwezi sasa haijakamilika juzi kuna jamaa kafungua application akatoa na 50k siku mbili tu imekamilika daah ipo siku kuna mtu ntamshikisha pesa za takukuru
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…