Kwa mnaotafuta maeneo ya kufanyia field tambueni hili

Kwa mnaotafuta maeneo ya kufanyia field tambueni hili

MarianaTrench

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
1,212
Reaction score
941
Wadogo zangu ambao mko vyuo vikuu na taasisi za juu za elimu nyinginezo, Unapoenda kufanya field mahali kuwa makini sana. Namaanisha nini?

Wewe umeenda kwa watu wenzio wanakusoma matendo yako pale. Wanakusoma unavyowahi na kuchelewa, majibu yako, uvaaji wako zaidi utendaji wako.

Sasaa wewe unafika ofisini kwa watu huyooo umshakimbilia milo maraa nido mara umechana karatasi kwenye diary ya mtu kitu kimeachwa mezani unadokoa....haaaa nakwambia ukweli unajizibia milango ndugu yangu. Fika tulia unapewa kazi unafanya...una swali uliza kwa upole na sio kukurupuka tena jinyenyekeshe. Basi kwa kufanya hayo utakuwa umejijengea nafasi nzuri kama utakuwa na maono ya kufanya kazi na hao jamaa baadae.

Basi ni hayo tu. Alasiri njema kwako na soma kwa biddii sana.

Nilitaka kusahau mavazi pia. Milegezo wanavaa wahuni ukiingia nao tu basi wanajua wewe mhuni. Na huku masuala ya gpa msiyalete hukooo kwenye campus zenu. Ofisini ni utendaji, jithidi kama ni kazi ujue vema huwa wanazifanyeje na si kukaa kihasara.
 
ndio ajira hizo wakizingua tu
tusi sikie ajira hamna mkaanza kuilalamikia serikal kumbe uliaribu kwenye field
 
Back
Top Bottom