Kwa mtaji wa milioni 3 naweza kuingia shambani nikalima kisasa?

Kwa mtaji wa milioni 3 naweza kuingia shambani nikalima kisasa?

Hela inatosha sana hiyo Kwa mkoa ulioutaja ila Lima heka mbili za maharage, mahindi Lima heka Moja Kwa haraka ukilima Kwa msimu matumizi yote ayawezi zaidi 1.3 m na inabidi upige kambi uko uko kilimo Cha Simu kimewagalagaza wengi.
Wazo zuri,ila tatizo ni moja,msimu mzima mpaka uishe hapo atamaliza mwaka mzima akisubiria mazao ya eka 3 na kambi kaweka,kuna gharama zake za kua nje ya mzunguko wake wa kawaida,anaweza jikuta kala hela iliyo bakia..
 
Huu ulimwengu, game ni tight sana hasa upande wa kutafuta pesa, kuna saving zangu kama million 3 nimeamua kurisk shambani sina matarajio makubwa lakini najua itakua ni sehemu ya kujifunza.

Hii mada inahusu wazoefu tu, nipo kasulu nafikiria kulima maharage na mahindi kwa msimu unaokuja, nimejaribu kutafuta bonde lakini mambo yamekua magumu, watu wanalima kwa kutegemea msimu, kuna watu waliojaribu kulima mbali na wanapoishi?

Yaani mfano nakaa kasuku alafu nalima singida? /Mbeya?
Kama una moja wapo kati ya hii list usilime

1. Majukumu kwamba huna pesa ingine yakuendesha maisha pindi unasubiri kuvuna -USILIME


2. Huna muda wakusimamia in 100% shughuli za shamba -USILIME


3. Pesa ndo hiyo hiyo ukipoteza huna pakuipata kwingine -USILIME


4. Huna uzoefu wa kilimo na huko uliko ni mgeni - USILIME
 
Hela inatosha sana hiyo Kwa mkoa ulioutaja ila Lima heka mbili za maharage, mahindi Lima heka Moja Kwa haraka ukilima Kwa msimu matumizi yote ayawezi zaidi 1.3 m na inabidi upige kambi uko uko kilimo Cha Simu kimewagalagaza wengi.
Mpaka avune MAZAO yote maharage na mahindi na hela ya kupiga kambi... Hana hela hapo labda kama atakuwa anakula upepo yeye na kambi..
 
3m ni nyingi sana,kuna mazao ya mboga mboga ukipata eneo lenye maji,kwa maana kilimo cha umwagiliaji,mazao ya mboga yasio na usumbufu Bamia na Ngogwe yanaweza badili kabisa maisha...
Binafsi nimegundua wa TZ wengi kuna ka sehemu hua tunajizima data kidogo,mfano...tuseme mtu ana shamba lake mahali ekari 10 halina rutuba ama maeneo hayo mvua sio nzuri na kwa ujumla mazao hayatoki,ila tunakomaa hapo hapo miaka na miaka,hili ni kosa kubwa kwa muono wangu,ni bora ukakodi hata ekari 5 sehemu nzuri na yenye uhakika wa kupata mavuno bora ukakimbiza.

Turudi kwenye mboga mboga,

1.Bamia

Unaweza kodi shamba ekari 2 kwa laki ama laki 2 kila ekari,ukafanya ya kufanya ukapanda na ukazisimamia vizuri,mbegu za bamia ni 15,000/Kg na ekari moja utapanda kilo 3-4,zinakua haraka,hazina purukushani ya mbolea,changamoto za wadudu na magonjwa ni za kawaida,utavuna miezi 3 na utachuma kila baada ya siku 2 kwa muda huo wote,mchumo wa chini wa ekari haupungui debe 10 na mchumo wa juu debe 30 kwa mbegu hizi za kienyeji,ukitumia hybrid itazaa zaidi na muda mrefu zaidi,
Debe haliwezi pungua Tsh 3000 hata iweje,kuchuma 500 kwa ndoo ya kutolea shambani,ama 700 kwa kipimo cha ndoo ya kuuzia,na kiwango cha juu kinaweza fikia 15,000 kwa debe wakati gharama zingine zote ni zile zile.

Unaweza piga hesabu unaweza ingiza kiasi gani kipindi hata cha kiangazi,
Na hapa ndipo pa kutengeneza mtaji wa kulima kilimo kikubwa cha mazao mengine wakati hii ina ku sustain,hutoi hela mfukoni.

Kumbuka,eka 2 ya bamia kwa 700,000 inaweza kukulimia ekari 20-50 ya mahindi/maharage/ufuta/mbaazi/ekari 10 ya karanga na mazao mengine yanayo ota vizuri na yenye soko yatakayo kupendeza.

Kwanini nimekushauri Bamia?

Sio labour intensive,soko lake ni uhakika,na ni kilimo cha bei nafuu,eneo dogo litakupa faida kubwa,eneo dogo ni rahisi kuli manage(mfano kupiga dawa unakomaa mwenyewe-ila zingatia maziwa pembeni ukimaliza unakunywa) etc

2.Ngogwe...,hapa ni waache kwanza mmeze hiyo ya Bamia
 
U
Kama una moja wapo kati ya hii list usilime

1. Majukumu kwamba huna pesa ingine yakuendesha maisha pindi unasubiri kuvuna -USILIME


2. Huna muda wakusimamia in 100% shughuli za shamba -USILIME


3. Pesa ndo hiyo hiyo ukipoteza huna pakuipata kwingine -USILIME


4. Huna uzoefu wa kilimo na huko uliko ni mgeni - USILIME
Uzoefu nitapata wapi kama nisipoanza
 
Kama una moja wapo kati ya hii list usilime

1. Majukumu kwamba huna pesa ingine yakuendesha maisha pindi unasubiri kuvuna -USILIME


2. Huna muda wakusimamia in 100% shughuli za shamba -USILIME


3. Pesa ndo hiyo hiyo ukipoteza huna pakuipata kwingine -USILIME


4. Huna uzoefu wa kilimo na huko uliko ni mgeni - USILIME
Atapataje uzoefu asipolima?
 
Huu ulimwengu, game ni tight sana hasa upande wa kutafuta pesa, kuna saving zangu kama million 3 nimeamua kurisk shambani sina matarajio makubwa lakini najua itakua ni sehemu ya kujifunza.

Hii mada inahusu wazoefu tu, nipo kasulu nafikiria kulima maharage na mahindi kwa msimu unaokuja, nimejaribu kutafuta bonde lakini mambo yamekua magumu, watu wanalima kwa kutegemea msimu, kuna watu waliojaribu kulima mbali na wanapoishi?

Yaani mfano nakaa kasuku alafu nalima singida? /Mbeya?
Nenda sehemu inaitwa miono ipo njia ya saadan tafuta heka mbili nunua hazizid milioni moja ambazo hazina visiki. Lima muhogo mbegu inaitwa msaada msimu mmoja tu hizo heka mbili hukosi milioni tatu na laki mbili. Toa garama za palizi zote mbili weka milioni moja mpaka unavuna. Kilimo Cha muhogo msimu kwa mwaka ni mara mbili.
 
Nenda sehemu inaitwa miono ipo njia ya saadan tafuta heka mbili nunua hazizid milioni moja ambazo hazina visiki. Lima muhogo mbegu inaitwa msaada msimu mmoja tu hizo heka mbili hukosi milioni tatu na laki mbili. Toa garama za palizi zote mbili weka milioni moja mpaka unavuna. Kilimo Cha muhogo msimu kwa mwaka ni mara mbili.
Oky kwaiyo Kwa kila mti mmoja wa muhogo unapata faida ya 350-400 .

Nielekeze jambo mnapandaje muhogo yenu huko .
 
Hiyo Miono iko wapi, wilaya na mkoa?
Nenda sehemu inaitwa miono ipo njia ya saadan tafuta heka mbili nunua hazizid milioni moja ambazo hazina visiki. Lima muhogo mbegu inaitwa msaada msimu mmoja tu hizo heka mbili hukosi milioni tatu na laki mbili. Toa garama za palizi zote mbili weka milioni moja mpaka unavuna. Kilimo Cha muhogo msimu kwa mwaka ni mara mbili.
 
Back
Top Bottom