Kwa mujibu wa Nyerere, Kikwete hatufai!

Kwa mujibu wa Nyerere, Kikwete hatufai!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Moja ya hotuba ya baba wa Taifa,ambayo sehemu yake hurushwa kila siku na ITV mara baada ya taarifa ya habari kama wosia wa baba wa taifa,inasema na hapa nanukuu "mtu anaeona haya kuitetea katiba aliyoapa kuilinda hatufai na aende akafanye kazi nyingine(akalime)".

Sasa kwasababu raisi Kikwete aliona haya kuitetea katiba yetu kwa kuruhusu utungwaji wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010 iliyovunja katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo Raisi Kikwete mwenyewe aliapa kuilinda, basi ni wazi kuwa Raisi Kikwete hatufai na arudi kijijini kwake Msoga akalime.

Kama kweki tunamuenzi Nyerere kwa vitendo,basi Raisi Kikwete aonyeshe mfano kwa kujiuzulu na si kwa maneno matupu.
 
rais anayeogopa kuwakamata mafisadi,wezi,wauza sembe hatufai,kiujumla kiwete ni janga.
 
Huu ulimbukeni utaisha lini huyo baba yenu wa taifa wakati wa utawala wake kaitetea katiba alivyokuwa anaweweka watu kwenye viziwizi na wengine wanafia huko.

Nikupe orodha alivyowatesa watu na kudhulumu mali za watu.

Nyerere ndiyo kaacha mifumo mibovu ya kiutawala ambao ipo mpaka leo.
 
Huu ulimbukeni utaisha lini huyo baba yenu wa taifa wakati wa utawala wake kaitetea katiba alivyokuwa anaweweka watu kwenye viziwizi na wengine wanafia huko.

Nikupe orodha alivyowatesa watu na kudhulumu mali za watu.

Nyerere ndiyo kaacha mifumo mibovu ya kiutawala ambao ipo mpaka leo.
Mbona leo CCM mnamuona Lissu kama muhaini kwa kumkosoa Nyerere kuhusu Muungano tena mkiongozwa na Kikwete mwenyewe?!

Au ndio ule msemo wa ....kuku lakini .... bata kaharisha?
 
Huu ulimbukeni utaisha lini huyo baba yenu wa taifa wakati wa utawala wake kaitetea katiba alivyokuwa anaweweka watu kwenye viziwizi na wengine wanafia huko.

Nikupe orodha alivyowatesa watu na kudhulumu mali za watu.

Nyerere ndiyo kaacha mifumo mibovu ya kiutawala ambao ipo mpaka leo.

Tupe hiyo orodha mkuu ,tuanze maisha mapya ya maelewano kwenye Tanganyika yetu mpya.
 
We kweli zuzu! Watanzania tunahangaika kujinasua kutoka kwenye katiba mbovu aliyotuachia halaf wewe bado unamfanya nyerere kama reference?...kweli nchi hii mazuzu wanaongezeka kila siku
 
We kweli zuzu!
Watanzania tunahangaika kujinasua kutoka kwenye katiba mbovu
aliyotuachia halaf wewe bado unamfanya nyerere kama reference?...kweli
nchi hii mazuzu wanaongezeka kila siku

kweli mkuu na bado tuna safari ndefu ya ukombozi kutoka na nchi kujaa mazuzu.
 
We kweli zuzu! Watanzania tunahangaika kujinasua kutoka kwenye katiba mbovu aliyotuachia halaf wewe bado unamfanya nyerere kama reference?...kweli nchi hii mazuzu wanaongezeka kila siku

Huna lolote wewe ni kibaraka wa JK tu.
 
UKISOMA KISA HIKI UTAELEWA KWA NN SAMWEL LUHANGA ANAMCHUKIA MWL

Sasa ilikuwa hivi,
Mzee Sayore alikuwa anafuga ng'ombewengi pamoja kufanya shughuli za kilimo kwawingi wakati huohuo akiwa mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli.

Hivyo basi baada ya kuona ng'ombe wanatoa maziwamengi mno na mazao yametapakaa mashambani,. akaamua kuwa awe analiuzia jeshi mazao kama vile maharage na mahindi pamoja na maziwa na nyama kutoka kwenye mifugo yake.......na pesa anachukua yeye mwenye mazo.

Aliendelea kufanya hivyokwa kipindi kirefu tu.. ikiwa ni kama sehemu yake ya maisha....

Sasa bwana ,,kumbe Kikwette (JK) ilikuwa inamuuma sana sana, yaani mno! sasa haieleweki kama ilikuwa kweli ni kwa uzalendo ua wivu tu....akaandika barua kwa raisi kipindi hicho JK Nyerere.

Katika barua hiyo akaandika lawama nyiingi mno na majungu mengi sana dhidi ya Sayore, akimwita bepari, bwenyenye, mnyonyaji n.k huku akisema hafai kuwa mkuu wachuo hicho kwakuwa navunja miiko ya uongozi na mambo mengine meengi (si mnamjua JK anavyojua kupiga fitna!)...

Basi bwana, akamalizia mwisho kwakujiandika jina lake na sahihi yake huku akijiita mzalendo kamili barua ikapostiwa ikiwa imeadresiwa kwa rais wa nchi wakati huo!......

Mwalimu, aliipata barua ile aliifungua akaisomaaaa kisha akapiga hesabu zake....sijui aliwaza nini mzee yule, akaihifadhi ile barua ikaa sana ofini kwake bila kuchukua uamuzi wowote.

Siku moja alipokuja mkuu wa majeshi wakati huo "General Mtukula" (David Musuguli) ofisini kwa Mwalimu eaisi kipindi hicho, mwalimu akampa ile barua kutoka kwa Kikwete "akisema hayo ni maMbo yenu kayamalizeni hukohuko".

Basi bwana ile barua Mkuu wa majeshi alikaa nayo muda hivi kwenye makabrasha yakee...., sasa siku mija alikuja Mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli(Sayore) Dar es salaam kufanya shughuli za kikazi akaenda hadi ofisini kwa Mkuu wa majeshi.

Baada ya shughuli kwisha na Sayore akiwa anajiandaa kwenda Monduli Mkuu wa majeshi alimwita, akampa ile barua ya Kikwete aliyomwandikia rais!!....

Sayore akaisoomaaa we akashangaa mno!! na akafura kwa hasira yule mmasai...., akuliza mwalimu kasemaje? Akaambiwa mwalimu kasema yamalizeni wenyewe!!.... Akasema naam, na akaondoka na ile barua hadi Monduli...

Alipofika tu yule mmasai aliitisha kikao cha wakufunzi wote na wakuu wengine pale chuoni, wakati wanajikusanya kwenda kwenye chumba cha mkutano yeye aliamua kwenda kutoa copy ile barua ya Kikwete, kopi nyingi idadi sawa na wajumbe wa mkutano ule....

Alipoingia mkutanoni akawaona wakuu na wakufunzi wote wameketi wakimsubiri wajue alicho waitia,.. akaanza kwa kuwauliza..jamani kama kuna mtu ana matatizo, au anaona kuna jambo haliendi sawa anyooshe mkono na saemekinacho mkereketa......watu wote wakawa kimya huku wengine wakisema hamna mkuu akiwemo Kikwette!!!

Basi bwana, tumalizie mkasa huu wa ------...

Sayore akaanza kuwagawia zile nakala (copies) za ile barua ya Kikwete kwenda kwa rais akawagawia wooote including Kikwete!!! Huku yule mmasasi Sayore akiwa amefura kwa hasira, macho mekunduuu! Akagonga ngumi juu ya meza kwa hasira na kusema someni hiyo barua!! kisha akatoka na kusema anakuja muda si mrefu...

Hapo Kikwete akajua kifo chake kimefika, akikumbuka macho ya yuile mmasai! akatetemeka macho yakamtoka lip! kwa woga!.. na wenzie wakamwanzishia zogo mle ndani......

Alichokifanya ni kuondoka haraka pale kikaoni wenzie wakajua bado yupo chuoni, kumbe safari ya Dar ikawa imeanza...!! Jamaa alitembea uchochoroni kwa muda mrefu sana huku akiogo kabisa kuingia barabara ya kuu...

Mashuhuda wanasema yule bwana akaja kupanda lift ya gari za vyama vya ushirika maeneo ya USA RIVER, hakukumbuka kubeba mzigo wowote!! Just imagine kutoka Monduli hadi hapo jamaa aliteseka sana... lakini yeye hakujali, cha muhimu ilikuwa kusalimisha maisha yake......

Basi huo ndiyo ukawa mwisho wa JK Monduli,........... hukurudi akaja Dar na kupangiwa kazi nyingine na chama... lakini alikuwa anamlaani sana Nyerere eti kwanini alimfanyia vile!!

Hicho ndicho chanzo cha JK kumchukia mwalimu na kugoma katakata kumwita baba wa taifa hadi leo! Yeye humwita mzee Nyrere tu au mwalimu baasi...na mara chache akiwa nje ya nchi humwita 'Father of our Nation', lakini ni pale anapotaka kupigiwa makofi kwa nukuu za Mwalimu....

**Ndugu zangu hiki ni kisa cha ukweli kwa 100%, inawezekana uandishi wangu ukawa na upungufu, lakini niemekipata kutoka watu mbalimbali waliowahi kuwa karibu sana na mkasa huu...
 
Huu ulimbukeni utaisha lini huyo baba yenu wa taifa wakati wa utawala wake kaitetea katiba alivyokuwa anaweweka watu kwenye viziwizi na wengine wanafia huko.

Nikupe orodha alivyowatesa watu na kudhulumu mali za watu.

Nyerere ndiyo kaacha mifumo mibovu ya kiutawala ambao ipo mpaka leo.

hahahaaaaa! Kweli watanzania vichwa maji si ndio nyie juzi tu mlikuja kulalama hapa ohh! Nyerere katusiwa sasa wewe leo tena umefanya nini wakati ndio mmejifanya wapenzi wakubwa.
 
Mwanzo, nilidhani utakua uzushi, ila leo kupitia maadhimisho ya miaka 36 ya kuzaliwa CCM, ndio nimeamini kupitia matamshi yake. Hv ni kwanini Ndg. Mrisho Kikwete huwa hataki kutamka Jina "Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere"????
Je na zile picha za kumbukumbu zenye Jina la Baba wa Taifa..., ziliandikwa kimakosa??


By bullet proof:
Nimewahi kusikia kwa mtu kuwa Rais Kikwete huwa hamuiti Mwalimu Nyerere 'baba wa taifa', kama tunavyofanya watanzania wengi. Japo sina uhakika sana na hili, mimi pia nimemsikiliza JK mara kadhaa anapoongea kuhusu Nyerere hamuiti baba wa taifa bali humuita 'mzee Nyerere'.

Kuna sababu yoyote ya maana inayomfanya JK asimuite baba wa taifa? au ameamua mwenyewe tu kumuita hivyo? Kuna tatizo lolote kutokumuita baba wa taifa?
 
Sipendi sana kila mtu kumnukuu mchonga kama kauli zake ni holy scriptures.Yeye mwenyewe alikuwa hatufai na fikra zake ndio zinadumu mpah leo hii
 
Moja ya hotuba ya baba wa Taifa,ambayo sehemu yake hurushwa kila siku na ITV mara baada ya taarifa ya habari kama wosia wa baba wa taifa,inasema na hapa nanukuu "mtu anaeona haya kuitetea katiba aliyoapa kuilinda hatufai na aende akafanye kazi nyingine(akalime)".

Sasa kwasababu raisi Kikwete aliona haya kuitetea katiba yetu kwa kuruhusu utungwaji wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010 iliyovunja katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo Raisi Kikwete mwenyewe aliapa kuilinda, basi ni wazi kuwa Raisi Kikwete hatufai na arudi kijijini kwake Msoga akalime.

Kama kweki tunamuenzi Nyerere kwa vitendo,basi Raisi Kikwete aonyeshe mfano kwa kujiuzulu na si kwa maneno matupu.

ni tahaira pekee atakaekubali kujiudhuru
 
Sipendi sana kila mtu kumnukuu mchonga kama kauli zake ni holy scriptures.Yeye mwenyewe alikuwa hatufai na fikra zake ndio zinadumu mpah leo hii

Kwa ma-CCM Nyerere ni Mungu mtu!
 
Mbona leo CCM mnamuona Lissu kama muhaini kwa kumkosoa Nyerere kuhusu Muungano tena mkiongozwa na Kikwete mwenyewe?!

Au ndio ule msemo wa ....kuku lakini .... bata kaharisha?
Wewe kauzu kweli ina maana wewe hapa upo kuitetea Chadema, mimi siyo kama wewe sishikiwi akili natumia akili yangu kupambanua mambo.
 
mmmh nyie si ndo mnasema wazee hawasemwi tena waasisi, mbona unamuita sasa muasisi ni dhuruma kumbe lisu hakukosea kusema alizoea kuishi kwa uongo
 
Huu ulimbukeni utaisha lini huyo baba yenu wa taifa wakati wa utawala wake kaitetea katiba alivyokuwa anaweweka watu kwenye viziwizi na wengine wanafia huko.

Nikupe orodha alivyowatesa watu na kudhulumu mali za watu.

Nyerere ndiyo kaacha mifumo mibovu ya kiutawala ambao ipo mpaka leo.
mmmh nyie si ndo mnasema wazee hawasemwi tena waasisi, mbona unamuita sasa muasisi ni dhuruma kumbe lisu hakukosea kusema alizoea kuishi kwa uongo
 
hahahaaaaa! Kweli watanzania vichwa maji si ndio nyie juzi tu mlikuja kulalama hapa ohh! Nyerere katusiwa sasa wewe leo tena umefanya nini wakati ndio mmejifanya wapenzi wakubwa.
Tena wewe kichwa maji machafu, humjui Ritz unaropoka tu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom