Kwa mwitikio huu hafifu wa wananchi kujiandikisha, Serikali wana la kujifunza!

Kwa mwitikio huu hafifu wa wananchi kujiandikisha, Serikali wana la kujifunza!

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
640
Reaction score
958
Zikiwa zimebaki siku chache kufanyika uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa, ni wananchi wachache sana ambao wamejitokeza kwenda kujiandikisha. Nilipojaribu kuwahamasisha wakajiandikishe, nilisikitishwa na nilichoambiwa.

1. Wananchi wengi miongoni mwa niliowauliza wanatambua umuhimu wa kupiga kura/kuchagua viongozi wao ili kuleta maendeleo.

2. Wananchi wengi wamekata tamaa kuona hata wakichagua kiongozi wanayemtaka, bado serikali/CCM ina viongozi wake na lazima wapite.

3. Wananchi wengi wanasema rushwa inafanya wapoteze haki yao.

4. Baadhi ya niliowauliza wanaogopa kuonyesha msimamo wao wa mgombea yupi/chama kipi wangekipigia kura kwa kuhofia usalama wao.

5. Wananchi wanaona viongozi wanaochaguliwa siyo waadilifu.

6. Wananchi wanaona viongozi wao wanatoa ahadi za uongo.

7. Wananchi wengi wameamua kupambania senti yao ya kila siku kuliko kupoteza muda kuchagua viongozi wasiokuwa na faida kwao.

8. Wananchi wengi maombi yao kwa Mungu ni afya na amani nchini.

Kipi kifanyike?

Viongozi badilikeni. Hata kama nafasi za kisiasa/uongozi ni biashara zenu na mmewekeza mitaji yenu, wananchi wengi wanatamani kuona ahadi zinatekelezeka.
 
Zikiwa zimebaki siku chache kufanyika uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa, ni wananchi wachache sana ambao wamejitokeza kwenda kujiandikisha. Nilipojaribu kuwahamasisha wakajiandikishe, nilisikitishwa na nilichoambiwa.

1. Wananchi wengi miongoni mwa niliowauliza wanatambua umuhimu wa kupiga kura/kuchagua viongozi wao ili kuleta maendeleo.

2. Wananchi wengi wamekata tamaa kuona hata wakichagua kiongozi wanayemtaka, bado serikali/CCM ina viongozi wake na lazima wapite.

3. Wananchi wengi wanasema rushwa inafanya wapoteze haki yao.

4. Baadhi ya niliowauliza wanaogopa kuonyesha msimamo wao wa mgombea yupi/chama kipi wangekipigia kura kwa kuhofia usalama wao.

5. Wananchi wanaona viongozi wanaochaguliwa siyo waadilifu.

6. Wananchi wanaona viongozi wao wanatoa ahadi za uongo.

7. Wananchi wengi wameamua kupambania senti yao ya kila siku kuliko kupoteza muda kuchagua viongozi wasiokuwa na faida kwao.

8. Wananchi wengi maombi yao kwa Mungu ni afya na amani nchini.

Kipi kifanyike?

Viongozi badilikeni. Hata kama nafasi za kisiasa/uongozi ni biashara zenu na mmewekeza mitaji yenu, wananchi wengi wanatamani kuona ahadi zinatekelezeka.
ccm hawawezi kujifunza katu. hawa ni mashetani, shetani hawezi kubadirika, lazima apigwe mpaka afe ndiyo salama ya wanadamu!
 
ccm hawawezi kujifunza katu. hawa ni mashetani, shetani hawezi kubadirika, lazima apigwe mpaka afe ndiyo salama ya wanadamu!
Unakumbuka kuwa miaka ya nyuma wapinzani walifanikiwa kupata viongozi wengi? Sema tu walilikoroga wenyewe baada ya kukaribusha kirusi.
 
Unakumbuka kuwa miaka ya nyuma wapinzani walifanikiwa kupata viongozi wengi? Sema tu walilikoroga wenyewe baada ya kukaribusha kirusi.
Hivi hizo lawama kina Lissu na Mbowe huwa wanatoa statements gani ku cover story?

Sijawahi kuwasikia wakitetea hoja yao ya kufika bei na mamluki!

Hilo doa limeacha kilema cha kudumu kwenye upinzani na kuonekana kama ni vyama vya mfukoni ama vyama vya kifamilia.
 
Kukata tamaa ni faida zaidi kwa mtawala mtawala anaweza kutawala ata miaka 100 na nguvu ikawa vile vile kama watu wataendelea kukata tamaa kupiga kura ni faida tu kwa mtawala
Yes hatupaswi kukata tamaa tunatakiwa kupambana na Ibilisi CCM kwa nguvu zote
 
Back
Top Bottom