Kwa Nini Baadhi ya Wasichana Wanapata Waume Wa Kuwaoa Haraka Lakini...?

Ok! Kwa hiyo unategemea kulea "watoto haramu?" (ie watoto wa nje ya ndoa? Au kama wanavyodai kitanda hakizai haramu?)

Ni dhana ya kikatili kabisa kudhania kuwa mtoto anaweza kuwa haramu. Binadamu atakuwaje haramu? Ni watu wasio na moyo ndio wanaweza hata kujaribu kufikiria hivyo. Hakuna binadamu aliye haramu. Halafu kwanza ni nani anayempa mtu mwingine mamlaka ya kuamua nani haramu na nani asiye haramu? Ujinga mtupu.

Na vipi kuhusu fact kwamba kuzaa nje ya ndoa ni dhambi kwa Mungu? Au unafikiri maisha yataishia hapa duniani tu?

Ukishaanza kum invoke mungu kunakuwa hakuna mambo ya "fact" tena. Mambo ya dhambi ni mambo ya mtazamo tu. Iweje kuzaa mtoto iwe dhambi? Labda ungeniambia kuzaa na kutelekeza mtoto ni dhambi basi hapo tungekubaliana. Lakini kuzaa mtoto iwe nje au ndani ya ndoa ni baraka kwa mtazamo wangu ili mradi unatimiza wajibu wako kama mzazi.
 

Kuzini ni dhambi, adhabu yake ni moto wa milele, usiozimika! Hata ujifariji namna gani, nafsi yako itakuhukumu daima milele!
 
mwanamke anapofika mda wakuolewa anakuwa kama mau kwaiyo vipepeo utua namanisha wanaume umfata anapoonaanafatwa anaanza kuchagua mda unazidi kwenda umri unasogea same time walewadogo nao wanaanza kukua wanaume wanaanza kuwafata wao so wale wakubwa wanabaki kupiga magoti na kuwasumbua wachungaji inakuwa ni mradi wa maombi kanisani hawa ni wale wachaguzi
 

Mi nimeipenda sana alalysis yako hasa ya wadada waliookoka. Thanks
 
Nna mfano live wa dada mmoja mpaka leo hajaolewa na ana 37yrs, eti yeye anataka mwanaume tall, handsome mwenye degree au masters awe na mpunga wa kutosha atoke kwenye family bora, na awe famous hapa town, basi amengojea mpaka sasa ana 37 na anamegwa na watu wa ajabu ajabu tu, halafu yeye mwenyewe halipi wala nini, lkn ana nata ajabu, kwa kung'ang'ania wanaume TALL utadhani ana ugonjwa labda sababu yeye ni MMASAI. SIku hizi bwana hiii sekta ni ngumu sana tena sana. ukitaka uone thamani ya mtu, pita asubuhi kwenye kituo cha dala dala wakati mabinti kibao wanaenda JOB ukiwa kwa miguu no one notice you! lkn pita pale na usafiri, utaona macho unayokodolewa pale ukisimamisha gari hukosi mmoja wa kuondoka naye, mabinti wana dream za ajabu ajabu na kubwa kuliko hata umri zao. Niliwahi kuwa na Girfriend kabla sijaoa, yeye sifa kubwa ya mwanamke kwake kuwa ame achieve ni kupangishiwa na mme wa mtu, rafiki zake wote akikusimulia utasikia, yule dada yuko juu kafunguliwa stationery na baba fulani kimara, au yule dada usimuone vile anakaa nyumba ya laki mbili na nusu sinza kapangishiwa na fulani, akimtaja huyo fulani utaona ni kigogo fulani ambaye ana ndoa hata zaidi ya miaka 20, utasikia mambo yake supa anavaa gauni la mariedo laki na ishirini, ukiuliza ana biashara gani au yupo ofisi gani utasikia anatembea na waziri gani sijui, yaani ilikuwa naboreka mno halafu hao wasichana sasa watoto wa miaka 18-24, na wengi wanasoma vyuo vya hapa town, CBE, IFM, Ustawi, Magogoni pale na vinginevyo, hawasomi yaani hao waume za watu wakisafiri ndo wanasafiri na hivyo vitoto, mara Arusha, Dodoma, Morogoro, Mwanza Mbeya hawa sasa ndo wanaoharibu kizazi chote cha wasicha sasa hivi, maana utakuta demu anasoma chuoni lkn anamiliki gari, wengine wakiona hivyo lazima watafute mababu wakuwanunulia mkoko. mtoto anasoma chuo kapangishiwa nyumba nzima full furnished na usafiri nje hapa ndo panapowaponza dada zetu. niliingia mitini maana demands zilikuwa kubwa mno, anataka kila week twende Zanzibar, bagamoyo, kama bongo hapa hapa basi weekend tukalale atleast golden tulip sasa hayo ni mapenzi au kuibiana. siku ya kwanza nilipoingia mkenge kwenda Bwagamoyo, aliwa text mashosti zake wote na kuwapigia simu watu eti leo tuko bagamoyo, siwezi kuja town, anawakaribisha nikajua hapa nimeliwa mazee, mwanamke namna hii ndani ya nDoa ni pasua kichwaaa, mwanaume hatuwezi OA starehe hizi.
 
jamani yaani hii mada imegonga penyewe kabisa..mie mwenyewe mwenzenu nilikoma kwa kuchagua kwanza nilianza na mwanaume aweje ,sifa nikawa nazo kwa hiyo kila aliyekuwa akija kwangu namcheki kwanza kama yuko vile ninavyotaka kama akiwa sivyo ndo basi tena miaka ikaenda weeeeeeeeeee miaka ikarudi..

harafu sometimez wadada huwa tunadanganyana sijui kama tunakuwa tumeingia katika true love eti ooh namtaka mwanamme ambaye hata nikumuonyesha kwa mashostito wangu anakubalika ..hata nikitembea naye popote sijutiii wakati mwingine unakuwa usichana unatudanganya

lakini ikifika wakati na mwenyezi mungu kama ameweka yes wakwako yupo anatokea na anaweza kuwa hana sifa hata moja unayoitaka na huyo ndio anakuwa mmeo
 

Umesema mengi lakini hujamalizia stori... kwani bado hujapata... nina mdogo wangu ambaye atakufaa kama bado.... soulbrother2 anasubiria kuwa na firstlady1 wa kwake
 
Umesema mengi lakini hujamalizia stori... kwani bado hujapata... nina mdogo wangu ambaye atakufaa kama bado.... soulbrother2 anasubiria kuwa na firstlady1 wa kwake

hahahaha heheheh nimeolewa na mtu ambaye nadhani mungu alimuumba kwa ajili yangu na mie kwa ajili yake till death do us apart😉
 

Hapo kwenye bold, na PRESSURE JUU.......!!!! 🙂
 

What if kama msichana akifanikiwa kumshawishi mchumba wake naye aokoke je watapokelewa kanisani na ndoa itafungwa?
 
What if kama msichana akifanikiwa kumshawishi mchumba wake naye aokoke je watapokelewa kanisani na ndoa itafungwa?

Wokovu unaopatikana kupitia mchumba ni mbaya sana, hata kama ndoa itafungwa! Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, hayo yote (wachumba, etc) mtazidishiwa! Msigeuze maneno na kusomeka: Tafuteni kwanza wake/waume na hayo yote (ufalme wa Mungu) mtazidishiwa!
 
Mada ni nzuri.Asante kwa wote mliochangia na alioanzisha hii mada.
Mtazamo wangu mimi ni kwa wote wanawake kwa wanaume ni kwamba huwezi kumpata mtu ambaye atakuwa na sifa zote unazozitaka.Hilo haliwezekani kamwe labda umuumbe wako!
Kwahiyo katika maisha yako kama umekutana na mtu ambaye ana walau sifa 2 au tatu kati ya 5 unazozitaka na umri na vigezo vingine vinakuruhusu basi huyo ndiye wako.Mapungufu mengine mnaweza kurekebishana au kuvumiliana wakati maisha yanaendelea.
Just my 2 cents!
 

Kuna sababu nyingi sana muhimu zimetajwa ila naomba kuongezea hizi:
1. Dini: unakuta watu tunaabudu tofauti lakini tunakuwa muda mwingi vyuoni, makazini, manyumbani na watu ambao ni dini tofauti na sisi, matokeo yake wachumba wengi lazima watatokea humu tunamokuwa muda mwingi, kwa wale ambao dini sio issue kwao unakuta wanaolewa mapema tu bila tatizo ila kwa msichana ambaye anamsimamo na dini yake inakuwa vigumu, mfano mwislamu ana option ya kuolewa hata mke wa nne, kuolewa na alieacha mke bila sababu yoyote ya msingi wakati mkristo hii ni kuvunja misingi ya imani yake.
2. Misimamo ya wazazi, hii inamchango mkubwa kuliko hata mnavyosema mabinti wanachagua ni kutokana na mzazi amekuwa akimsisitizia specifications gani
1. umri wa mchumba (watoto wadogo hawafai, mzee sana analingana na mimi)
2. kazi au kipato (usiniletee kabisa maskini au mwenye elimu au kipato kidogo, wengi mfanyabiashara ni mtu tapeli hataki)
3. kabila ( hapa hata sina haja ya mfano)
4. dini (familia iliyosimama ktk misingi ya dini inategemea binti aolewe na mwenye imani sawa hivy binti labda aasi ndio ataolewa nje ya imani yake)
5. mwingine hata mahali anakoishi kufanyia kazi mfano mikoani, au nje ya nchi hataki

Kwahiyo msiwalaumu mabinti ispokuwa ni malezi na expectation za wazazi, jamii ndio zinazowakwaza mwishowe wanaishia kukaa bila kuolewa, lakini kwangu naona ni bora wakae hivyo kuliko kukosa amani.
 

Kwenye pointi hizo mbili hapo juu (in red) nakubaliana na wewe kabisa! Lakini tazizo ni kwamba tabia za wachumba huwa zimefichwa ndani ya maneno matamu matamu wanayopeana wakati wa uchumba! Na wakati huo tamaa za mwili zinafunika mabaya yote na yanaonekana, superficially, kwamba yanavumilika! Pindi wanapoingia kwenye kuishi pamoja vijitabia vilivyojificha vinajitokeza moja baada ya nyingine, mwishowe inajitokeza mijitabia ambayo haivumiliki! Hapo ndipo machungu ya ndoa yanapoanza na uvumilivu unapoanza kutoweka.
Ushauri wangu ni kwamba mshirikisheni Mungu kabla ya kupata wake au waume. Msikimbilie kumshirikisha tu matatizo yanapojitokeza, huku tangu mwanzo mlifanya maamuzi wenyewe! Mimi ndivyo nilivyofanya na naishi na mke wangu kwa raha mustarehe, hata kama tunakwazana, tunaishia kuombana msamaha na amani inatawala maisha yetu siku zote! Thank you God!
 

Mke ni kipaji kama ilivyo kwa urefu au ufupi. Nyumba moja, malezi mamoja, wazazi walewale lakini wanaweza kuzaliwa mabinti kumi na akaolewa mmoja tu. Au pia wanaweza kuzaliwa kumi na wote wakaolewa.

Au mwanamke anaweza akafiwa na mumewe kwa namna yeyote ile hata kwa HIV na bado akagombewa hata kabla ya mazishi watu wakitaka wamuoe.

Cha ajabu zaidi ni kuwa wengi wa wanawake wasio na kipaji cha mke ni wazuri mno kwa sura na maumbile kuliko wenye kipaji hiki. Kwa hiyo kwa mabinti ambao ni wazuri msiringe saaaana kwa kuwa mnapapatikiwa kunako asubuhi itakapofika nane kasorobo ndo mtaelewa ninachoandika hapa.

Hivyo si kila mwanamke anafaa kuwa mke. Mke ni taasisi nzito mno kuliko hata mume. Watoto bila baba wanaweza kwenda lakini bila mama watoto wengi huishia kuwa na mioyo ya kigaidi.

Soma biblia Methali 31:10 mpaka mwisho utajifunza kibiblia zaidi, maana ya mke yaani mke mwema(Yaani mwenye kipaji hiki), asiye mwema ni yule aliyeolewa ambaye hana kipaji cha mke.
 
What if kama msichana akifanikiwa kumshawishi mchumba wake naye aokoke je watapokelewa kanisani na ndoa itafungwa?
Bora mara mia Msichana akubali kuolewa na mwanaume akiwa hajaokoka ,na akae akijua wazi yupo na mtu wa aina gani,kuliko kutumia ushawishi wa aina yoyote "kumuokoa" au yeye mwanaume "ajilazimishe" kuokoka,it will be a disaster.
NB; kuhusu swali lako,inategemea na dhehebu,mengine hawakupokei ng'oo,wengine watakuchunguza,na wengine utapokelewa chapchap hasa kama una vijisenti.
 

very very true indeed.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…