Kwa nini Dk. Idris Rashidi bado yuko kazini hadi leo?

Kwa nini Dk. Idris Rashidi bado yuko kazini hadi leo?

Dr. Idris Rashidi aliteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu baada ya kifo cha Gilman Rutihinda mwaka 1993. Aliweza kudumu hapo kwa kipindi cha miaka sita toka 1994-1999, kipindi kilichogubikwa na wingu zito la ufisadi lililohusisha hii Benki ya Wananchi. Katika kipindi hicho tulishuhudia serikali ikiingia mikataba mbalimbali iliyoifunga serikali na kuisababishia madeni makubwa.

Baada ya hapo na katika kipindi cha miaka sita alifanya kazi katika taasisi tatu tofauti ambako inasemekana alijiuzulu kwa sababu zisizojulikana mpaka alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco. Mwaka 2007 alitingisha kiberiti kwa kutishia kujiuzulu lakini JK, kwa sababu zisizojulikana, akaamua kumtetea na kukataa kumkubalia .

Je, ni uswahiba peke yake ama kuna zaidi ?

Na alitingisha kiberiti kwa kesi mbuzi ya Tanga Cement! Kama alivyoshughulikia ishu ile ndio menejimenti style yake, basi kweli tumekwisha!

Amandla............
 
Leo hii Dr. Idris Rashidi, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, baada ya kuitisha Jamhuri ya Tanzania na watu wake kwa giza totoro, bado anapeta - kulikoni ? Kufukuzwa hafukuzwi, kujiuzulu hataki na kuwajibika hakusudii - kulikoni ? Tawi alokalia linakatika lakini yeye bado kang'ang'ania - anapata wapi support ? Dili lake limeshtukiwa, maombi yake yametupwa na kusudio lake limekwama - analindwa na nani ? Kwa nini bado yuko kazini ?
 
Leo hii Dr. Idris Rashidi, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, baada ya kuitisha Jamhuri ya Tanzania na watu wake kwa giza totoro, bado anapeta - kulikoni ? Kufukuzwa hafukuzwi, kujiuzulu hataki na kuwajibika hakusudii - kulikoni ? Tawi alokalia linakatika lakini yeye bado kang'ang'ania - anapata wapi support ? Dili lake limeshtukiwa, maombi yake yametupwa na kusudio lake limekwama - analindwa na nani ? Kwa nini bado yuko kazini ?

Ni vigumu kuamini huyu jamaa pamoja na wengine kama yeye, kwa sababu gani bado wameng'ang'ania na wameachwa tu kwenye nafasi walizo nazo!

Kama si kuna mkono mkubwa ambao sisi hatuuoni basi sisi inawezekana taarifa tulizao nazo ni za ''kimbeya'' la sivyo kwa mambo yalivyo sasa hawa jamaa hawakupaswa kuwepo kny nafasi hizo now.....right place kwao likuwa Keko may be!
 
Idris Rashid bado yukoTanesco kupitisha dili za kifisadi. Kwa kuwa yeye ni mla rushwa na wakuu wanajua (Rada, nk, nk), walimtaka nae awafanyie kazi. Dili kubwa alikuwa afanye limeshtukiwa. Naona ataondolewa pale muda si mrefu...siku zake zinahesabika.
 
Idris Rashid bado yukoTanesco kupitisha dili za kifisadi. Kwa kuwa yeye ni mla rushwa na wakuu wanajua (Rada, nk, nk), walimtaka nae awafanyie kazi. Dili kubwa alikuwa afanye limeshtukiwa. Naona ataondolewa pale muda si mrefu...siku zake zinahesabika.

Inawezekana kuwa amewekwa kutimiza mahitaji ya watu fulani. Ila sioni kuwa ataondolewa. Inawezekana pia kuwa aliamua mitambo ya DOWANS inunuliwe kutokana na vitisho ambavyo wanaotaka awafanyie mambo yao walimpa. Vitisho vya kufunguliwa mashitaka kwa mambo aliyowahi kufanya kinyume na mataratibu (Rada n.k).
 
Inawezekana kuwa amewekwa kutimiza mahitaji ya watu fulani. Ila sioni kuwa ataondolewa. Inawezekana pia kuwa aliamua mitambo ya DOWANS inunuliwe kutokana na vitisho ambavyo wanaotaka awafanyie mambo yao walimpa. Vitisho vya kufunguliwa mashitaka kwa mambo aliyowahi kufanya kinyume na mataratibu (Rada n.k).

Serikali, kupitia waziri wake wa Nishati na Madini William Ngeleja, imewaahidi wananchi kuwa hakuna hatari ya nchi kuingia gizani katika siku za karibuni na kwamba mipango ipo madhubuti ya kuhakikisha hivyo. Swali hata hivyo linabaki kuwa tishio la Dr. Idris Rashidi, Mkurugenzi wa Tanesco lilitokana na nini na alipata jeuri wapi ya kusema alilosema.

Ni dhahiri kuwa aliudanganya umma wa Watanzania na kwa hali kama hii napata taabu kuelewa kwa nini mpaka dakika hii hajachukuliwa hatua yoyote. Je alitaka kutumia huu uwongo kuwezwesha mitambo ya Dowans kununuliwa na kama ni hivyo, hii ina tofauti gani na mshtakiwa anayejipatia mali kwa njia ya udanganyifu ?

Wakati tunamsubiri mwali wa Dowans - Dr. Idris Rashid must GO
 
Mag 3, mi naomba kama una petition tuweke sahihi hapa JF! Dr Idris mi nimemshikilia bango AJIUZULU! Na tusitake kutafuta ushahidi wa rada na vitu vilivyopita maana yanaweza yakakwamishwa, sisi tunatumia kigezo cha TANESCO kwani ametishia nchi na ametudanganya wananchi akidai eti tutakaa gizani.
DR IDRIS RASHID MUST GO - nakuunga mkono Mag3

Dr W. Slaa, mheshimiwa mi naomba msiendelee kumwendekeza Rais wetu maana kama makosa ameshafanya mengi sana. Pia ni dhahiri kuwa yeye ni sehemu ya mtandao huu wa mafisadi. Si kwamba eti hafanyi lolote mpaka asukumwe, ni kwamba hafanyi lolote PERIOD. Tunaomba wabunge wetu muanze process ya kum-impeach rais na kutunisha misuli yenu ili tuwahishe uchaguzi! Ikiwezekana tufanye uchaguzi mwaka huu huu! Tumechoka na ufisadi, ulaghai na uharamia unaoendelea ndani ya serikali ya awamu ya nne!
IMPEACH THE PRESIDENT
 
Haki na sheria ni vitu viwili tofauti. Lakini haki ya watu haipotei. Ushahidi wa mchukua chochote huwa haupo labda awe mjinga sana, hivyo kama unangoja ushahidi hupati n'go. Lakini basi kwa wasiwasi huo usimpe majukumu mengine!!!!!!!
 
THE ISSUE IS OUR GOVERNMENT APPOINT PEOPLE WITHOUT LOOKING AT THEIR CVS
Hivi Mtu anapewa vipi post ya MD wa shirika la Umeme wakati hajui hata umeme ukoje?
Hivi mtu anapewa vipi post ya Wizara e.g fedha - wakati kisomo cha Finance NIL
Hivi mtu anapewa je post ya e.g. Wizara ya afya wakati hajui chochote kuhusu medicine
Sawa inawezekana hizi ni Management or leadership positions lakini its high time VIONGOZI WA MASHIRIKA,WIZARA ETC. WAKAWA WANACHUKULIWA KWA WALIOSOMEA WANACHOONGOZA - ENGINEER AKISEMA HUU MTAMBO MBOVU - KWA VILE KIONGOZI HAJUI MAANA YA MTAMBO - HATAJALI - ATAANGALIA TU MASLAHI YAKE ANAYOPATA - WAKO WASOME WENGI WANAOWEZA KUWA WAKUU WA IDARA NYETI - IKISHAINGIZWA SIASA - LAZIMA MAMBO YAHARIBIKE - WASHAURI WA RAIS - MSHAURINI VYEMA
 
THE ISSUE IS OUR GOVERNMENT APPOINT PEOPLE WITHOUT LOOKING AT THEIR CVS
Hivi Mtu anapewa vipi post ya MD wa shirika la Umeme wakati hajui hata umeme ukoje?
Hivi mtu anapewa vipi post ya Wizara e.g fedha - wakati kisomo cha Finance NIL
Hivi mtu anapewa je post ya e.g. Wizara ya afya wakati hajui chochote kuhusu medicine
Sawa inawezekana hizi ni Management or leadership positions lakini its high time VIONGOZI WA MASHIRIKA,WIZARA ETC. WAKAWA WANACHUKULIWA KWA WALIOSOMEA WANACHOONGOZA - ENGINEER AKISEMA HUU MTAMBO MBOVU - KWA VILE KIONGOZI HAJUI MAANA YA MTAMBO - HATAJALI - ATAANGALIA TU MASLAHI YAKE ANAYOPATA - WAKO WASOME WENGI WANAOWEZA KUWA WAKUU WA IDARA NYETI - IKISHAINGIZWA SIASA - LAZIMA MAMBO YAHARIBIKE - WASHAURI WA RAIS - MSHAURINI VYEMA

Mkuu Preacher hapo tuko sawa kabisa. Lakini ni tatizo la JK, hii kazi ilitangazwa kwenye magazeti na walitaka mojawapo ya qualification mtu awe na ujuzi wa uhandisi wa umeme na menejimenti. JK nadhani kwa sababu jamaa ni mshikaji wake akampasia. Kazi ilivyotangazwa waombaji ina maana wangesailiwa na kuchaguliwa yule mwenye CV inayofaa. Lakini wakampa huyu jamaa hata bila kumsaili na ndiyo alikuwa akiwatambia wafanyakazi kuwa yeye huwa anaombwa kufanya kazi huwa haombi kazi kwi kwi kwi kwi. Hiyo inaonyesha ni meneja wa aina gani. Katika kizazi hiki ambacho unaweza kuongoza watu wenye ujuzi kuliko wewe humanage watu kwa mkwara na kutamba. No wonder umeme unakatikakatika kila wakati
 
Just like there is a war on corruption there should be a war on incompetence.

From TANESCO to BOT to Air Tanzania their are people in high level positions that have no business being there.
 
Kufuatana na taarifa iliyopo huyu Dr.Rashid ana mkataba wa Miaka mitatu na unaishia Novemba 2009 na alipewa hii kazi na RAIS Jakaya Mrisho Kikwete hakuna mwenye ruksa ya kugusa mkataba wake mpaka atimize malengo. Kama ilivyo mikataba ya IPTL,SONGAS,MADINI,TICTS,TRL ambayo ni mibovu kuliko huo wa Dr. Rashid ambao kamshahara ni tshs.20 millioni kwa mwezi tu. Hii ni fidia kwa kufanikisha Rada hamjui pension ya BOT ni kiduchu. Sasa mwataka yeye Mzee mstaafu akale wapi na Rias ni Rafiki. Shikeni adabu hawezi toka tena tutamwongezea mkataba mpaka afie huko tanesco. Vijisenti vya bodi havimfai anataka apakue mwenyewe yote kwa Ruksa ya Jakaya kwani uwongo? Sisi tuna swala tano na ALLAH yuko nasi kwenu hakuna wazee nini? Shut up???????????
 
We are not going to shut up mpaka kieleweke. Hakuna wenye haki zaidi ya wengine kwenye nchi hiyohiyo. Kwamba wengine wakiiba sehemu moja wapewe na sehemu nyingine waendelee kuiba, na huku wengine wakishutumiwa kuiba wanarundikwa jela maisha? Haiwezekani. Dr. Rashidi na wezi wenzie (kuanzia raisi wake) na marafiki zao lazima waachie ngazi na wawajibishwe. Kusema lazima tuseme; isipotokea leo, mapambano yataendelezwa kesho na yatatokea tu! Haki ya mnyonge haipotei, watatunyonga lakini kabla hatujafa wote damu yetu wachache itasafisha kizazi hiki na haya maovu.
 
Kuna taarifa za kujiuzulu kwa huyu mkurugenzi wa TANESCO zimezagaa katika baadhi vitongoji vya Dar,mwenye Taarifa zaidi ninaomba atuhabarishe.
 
Kujiuzulu haitoshi tunataka kuona wale waliojiuzulu wote wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria na kujibu tuhuma za kujiuzulu kwao ,wakuwajibika ni serikali ya Sultani CCM kuhakikisha makada wake wanapanda kizimbani na kujibu tuhuma.
Yaani kwa mtindo uliopo mtu ameshafanya madudu ,anajiuzulu na mchezo kwisha ,hivi tutafika ?
 
Kujiuzulu haitoshi tunataka kuona wale waliojiuzulu wote wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria na kujibu tuhuma za kujiuzulu kwao ,wakuwajibika ni serikali ya Sultani CCM kuhakikisha makada wake wanapanda kizimbani na kujibu tuhuma.
Yaani kwa mtindo uliopo mtu ameshafanya madudu ,anajiuzulu na mchezo kwisha ,hivi tutafika ?
Are You sure?......au Mbwembwe zako...!!!!
 
I hope safari hii hatabembelezwa kama wakati ule.
 
Ukishindwa Ku-deliver kujiuzulu its Fine...Kuna wabongo wetu ambao hawajapewa nafasi ili tuone Vipaji vyao...!!!

Mambo ya kufikishwa Mahakamani any person anaweza..Ikiwa Mtikila anaweza sembuse wengine washindwe....Kupelekwa mahakamani hakutegemei upo ktk Kiti au Umejiuzulu...!!!
 
Back
Top Bottom