Kwa nini kuna watu wanachukia Marekani kutetea maslahi yake?

Kwa nini kuna watu wanachukia Marekani kutetea maslahi yake?

Afghanistan Taliban waliambiwa wawakabidhi Osama na Al Qaeda yake waliokiri kufanya ugaidi wa September 11 lakini Taliban walikataa, walionza kutangaza vita walikuwa ni Al Qaeda.

Syria imeingia vitani katika wimbi la Araba spring kwa sababu ya udikteta wa Bashar Al-Asaad, majeshi ya nje yalienda kutuliza hali iliyochafukia na ikiwezekana kumng'oa kwa sababu yeye na utawala wa miaka 40 wa familika yake ndio chanzo cha machafuko Syria.

Uvamizi wa Iraq ulikuwa wa hovyo na ulipingiwa na watu wengi hata huko West kwenyewe mfano kina Nancy Pelosi, Bernie Sanders, Jeremy Corbyn hadi na baadhi ya wakuu wa majeshi wa zamani.
Je waliofanya huo uvamizi wa hovyo huko Itaq wameshachukuliwa hatua au imeishia kwenye kulaani tu

Na kama majeshi ya nje yanaona ni vema kuingilia nchi nyingine ili kutetea raia wa nchi husika

Mbona hawaendi Congo,Msumbiji ili wasaidie wananchi wanaoteseka maeneo hayo

Lakini pia mbona hayo majeshi hayajaingia moja kwa moja pale Ukraine ili wamsaidie kuliko kuishia kulaani na kuweka vikwazo.
 
Kwa nini watu huilaumu Marekani kwa kutetea maslahi yake Ulimwenguni? Kwani kuna nchi inakatazwa kutetea maslahi yake dhidi ya nchi nyingine?

Kwani kuna ulazima gani wa kuwa Rafiki wa Marekani au kutii maagizo yake??
Kwa nini umekua unapinga Russia ikitetea maslahi yake/usalama wake for future generation hapo Ukraine?

Ukiweza kujibu hilo ndio vivyo hivyo watu wanaoipinga USA, kila mtu ana mtazamo wake huwezi kuitetea USA kwamba inatetea maslahi yake hata kwa kutumia nguvu ya kijeshi wakati huo huo unaipinga Russia kutetea maslahi yake kwa kutumia nguvu za kijeshi.
 
US hakuna demokrasia kungekua na demokrasia zingeheshimiwa kura za raia kuliko za wale wachache wa electro

US ndio inaongoza kwa ufikteita
Shujaa Mwendazake,rejea ule uchaguzi wa Hirary Clinton.
 
Umeandika pumba sana ila kwa vile umetumia mipasho naamua kukupuuza

Na kwa kukushauri tu sio kama siwezi kukuita majina ya kukukera ila sina stress za kumalizia kwako

Wewe unaonekana una stress unatafutia faraja hapa JF haya endelea na kazi utatunukiwa.
Jamaa kakukandamiza na kitu kizito.
 
Back
Top Bottom