Kwa nini Museveni anaheshimika sana, akifuatia Kagame

Kwa nini Museveni anaheshimika sana, akifuatia Kagame

flyingcrane

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2014
Posts
241
Reaction score
88
Wakuu nimeliwaza hili jambo kwa muda mrefu sasa. Rais Kaguta Museveni wa Uganda anaheshimika sana nchini Kenya. Yaani anapoongea wakenya humshangilia na kuhisi kama wanahutubiwa na Rais wao. Amekaa na mawaidha mazuri na kuwa na imani na muungano wetu wa EAC (namaanisha CoW).

Wakenya kumkubali Museveni kunadhihirisha ukubaliano wa waganda nchini Kenya hivi basi kutuonyesha mfano mema kwa majirani zetu hapa EAC. Miaka ya Nyuma museveni alidharau wakenya na jeshi letu hivyo wananchi kumkemea hadharani, kuchoma sanamu yake na kung'oa Reli.

Rais wa pili anayehishimiwa Kenya ni Kagame kwa kutembea nasi kimaendeleo na kuheshimiana nasi kimaendeleo. Rais wa tatu asiyejulikana na Kuheshimika ni Jakaya Mrisho Kikwete, licha ya kuwa Tanzania na Kenya zimekuwa rafiki wa toka nitoke, majirani wema sawa tu na ndugu pacha miaka ya nyuma, hali hii imegeuka kwenye hatamu yake na Kikwete sababu ya dharau na ubinafsi, kutoshiriki kimaendeleo na wenzake na kutoa sababu.

Hutawahi sikia Rais Kikwete kapewa nafasi kuhutubia wakenya katika sherehe kubwa, na akipatiwa ruhusa basi atazomewa tu bure, asipokanyaga yeye kwa sherehe kubwa za Kenya hutasikia wakenya wakiongea lakini Museveni ama Kagame asipohudhuria sherehe za Kenya, wakenya watalalamika sana kutosikia sauti za viongozi hawa wanaoongoza kwa matendo.

Chukulia mfano makaribisho ya Museveni na Kagame wanapokuja Kenya hao hukaribishwa vizuri kwa heshima ikilinganishwa na Kikwete anapowasili. Hii tofauti baina ya Kenya na Tanzania ni hatari sana kwa uhusiano wa wananchi kwa mataifa haya mawili.

Tanzania imejitenga na CoW hivi basi kutoshirikishwa kwa miradi mikuu ya pamoja, biashara n.k hili si jambo zuri kwa watanzania Itabidi wabadili sera zao na mataifa jirani bila hii watabaki kuchelewa barabarani wakati basi limewaacha.
 
Kenya hawamuheshimu kwasababu jk amewanyima fursa kuingia tz
 
Wakenya twapenda viongozi wenye mielekeo dhabiti,kama kuna jambo ambalo halinufaishi nchi analiweka parwanja.kama vile kaguta alisema kwake hakuruhusi wasagaji,kagame akaonya bbc wapeleke undaku kwao, no nonsense leaders,ths is the way forwand no bone of contetion
 
Wakenya twapenda viongozi wenye mielekeo dhabiti,kama kuna jambo ambalo halinufaishi nchi analiweka parwanja.kama vile kaguta alisema kwake hakuruhusi wasagaji,kagame akaonya bbc wapeleke undaku kwao, no nonsense leaders,ths is the way forwand no bone of contetion

kweli kabisa wakenya mnapenda viongozi thabiti: kama kenyatta aliyeiba ardhi robo ya nchi, kama Moi aliyekuwa dikteta, kama Kibaki aliyesababisha machafuko mpaka tukaja kuwasuluhisha, kama Uhuru ambaye kaachiwa na ICC kutokana na mashahidi "kupotea", no wonder mnapenda viongozi kama Kaguta, anayeongoza kwa miaka zaidi ya 25 kimabavu, kama kagame a genocide perpertrator....hongera zenu.
 
Heshima ya mtu huijenga mwenyewe kama vile usivyoweza tengeneza jina bali matendo yako ndo yalitengenezalo jina lako.
 
Jamaa kadai eti chelewachelewa utakuta bus limeisha ondoka bila hata ya kufahamu kuwa hilo basi dereva mwenyewe ni Jakaya Mrisho Kikwete na makonda wake ni Wabongo halisi.JK hana haja ya kujikomba kwa Wakenya au marais wa nchi za east africa.Wivu hiyana na chuki za kijinga ndio sababu ya watanzania kuchukiwa na majirani zetu,wao kila siku bado wanafikiria kuidhulumu Tanzania na kuirudisha nyuma.Nimetumia neno kuidhulum,hapo ninamaanisha tangu sakata la kuvunjwa east african community deliberately ili tudhulumiwe assets zetu nyingi zilizokuwa Kenye wakati huo bado hawa jamaa wanaota ndoto za kurudia kitendo ka kile.Rais Kikwete kama kiongozi wa nchi yenye nguvu na utajiri mwingi hana muda wa kujihangaisha na loosers.Kifupi hivi sasa economicaly tuko juu sana na kumbukeni tunayo sadc bado inatufanya tuongeze jeuri yetu.Murage Msherwampamba.
 
flyingcrane

Source,data na statistics za ukweli zipo wapi katika habari hii maana JamiiForums lazima ulete uzi (thread) unaozingatia viwango (standards) na siyo ''mahaba'' au tetesi.
 
Last edited by a moderator:
flyingcrane

Umewaza sana lakini ulisahau kufikiri
~Kwanini kenya ndo inawaheshimu sana akina Mseveni na Kagame!?
~~Vipi kuhusu historia ya Afrika ya mashariki kiuchumi,kijamii,kisiasa,kitekinolojia na kimazingira..inakupa picha gani?
~~~vipi kuhusu haki za kisiasa na kiraia nchini Uganda na Rwanda,nikweli kwamba Mseveni na Kagame wanastahili heshima katika ulimwengu wa demokrasia na utawala bora!?
~~mwisho fikiri kuhusu madhara ya kuutangaza udhaifu wako,familia yako,jamii yako,nchi yako n.k?

kwanini usishauri ama kutoa maoni yako bila kuitweza ama kuifedhehesha nchi yako ati imekosa heshima!!!!
WATANZANIA NCHI YETU INAHESHIMA SANA.VIONGOZI WOTE WATAPITA LAKINI NCHI ITASIMAMA.TUWENI WAZALENDO,TUILINDE NCHI YETU!!!
 
Last edited by a moderator:
Umewaza sana lakini ulisahau kufikiri
~Kwanini kenya ndo inawaheshimu sana akina Mseveni na Kagame!?
~~Vipi kuhusu historia ya Afrika ya mashariki kiuchumi,kijamii,kisiasa,kitekinolojia na kimazingira..inakupa picha gani?
~~~vipi kuhusu haki za kisiasa na kiraia nchini Uganda na Rwanda,nikweli kwamba Mseveni na Kagame wanastahili heshima katika ulimwengu wa demokrasia na utawala bora!?
~~mwisho fikiri kuhusu madhara ya kuutangaza udhaifu wako,familia yako,jamii yako,nchi yako n.k?

kwanini usishauri ama kutoa maoni yako bila kuitweza ama kuifedhehesha nchi yako ati imekosa heshima!!!!
WATANZANIA NCHI YETU INAHESHIMA SANA.VIONGOZI WOTE WATAPITA LAKINI NCHI ITASIMAMA.TUWENI WAZALENDO,TUILINDE NCHI YETU!!!


Mkuu usisahau ule usemi wa ndege wenye sifa sawa huruka pamoja, katika nchi inayoheshimu haki za watu mtu mwenye kesi ICC hawezi kuthubutu kuchukua fomu kugombea uongozi hata wa kijiji. Kitendo cha UHURUTO kushinda uraisi huku kesi ikiendelea ICC ni uthibitisho tosha kua PK na M7 wataheshimika sana kwenye maeneo waliyo na ushawishi lakini kuna maeneo hawawezi kukanyaga. Kuna siku Uhuru alizomewa na kudhalilishwa sana maeneo ya nyanza.
 
flyingcrane

Hatuhitaji CoW. Sisi tuna raslimali za kutosha kuliko nchi yoyote Africa mashariki. Tuna Ardhi kubwa yenye rutuba, tuna gesi, makaa ya mawe, akiba ya chuma, uranium, Hifadhi za wanyama n.k na kiuchumi tutawapita kama mmesimama miaka michache sana ijayo. Sisi ndo tuliopigania uhuru wa nchi zote za kusini mwa Afrika ikiwemo Angola, Zimbabwe, Mozambique, Namibia, South Africa, Usheliseli na sasa hivi tupo Kongo DRC kulinda amani, tumetumia resource zetu miaka yote hiyo na bado uchumi wetu unakua kwa kasi kuliko nchi yoyote Afrika mashariki kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
Hatuhitaji CoW. Sisi tuna raslimali za kutosha kuliko nchi yoyote Africa mashariki. Tuna Ardhi kubwa yenye rutuba, tuna gesi, makaa ya mawe, akiba ya chuma, uranium, Hifadhi za wanyama n.k na kiuchumi tutawapita kama mmesimama miaka michache sana ijayo. Sisi ndo tuliopigania uhuru wa nchi zote za kusini mwa Afrika ikiwemo Angola, Zimbabwe, Mozambique, Namibia, South Africa, Usheliseli na sasa hivi tupo Kongo DRC kulinda amani, tumetumia resource zetu miaka yote hiyo na bado uchumi wetu unakua kwa kasi kuliko nchi yoyote Afrika mashariki kwa sasa.

Ndo tumekalia hayo hayo! Wenzetu wana chanja mbuga!
 
mi kama mtanzania msomi, nASEMA KTK HILI NI Tanzania Kwanza ! we kama mkenya humpendi kikwete usimpende lkn heshimu personality ya mtu alafu tuki compare JK na Uk ah unakosea UK ni kendergaten level !
 
wakenya wamesahau MUSEVENI AMESOMA DAR ES SALAAM, wala sio NAIROBI AU MOMBASA
 
wakenya wamesahau MUSEVENI AMESOMA DAR ES SALAAM, wala sio NAIROBI AU MOMBASA

Pictured below is President Museveni with a first borne Brigadier General Muhoozi Kainerugaba ...in their Moshi ,Kilimanjaro residence in mid 70 s ...by then he was a lecture at cooperative college ...as a code .
Todate Museveni Family still keep their Moshi Residence .,at upmarket Shanty Town..View attachment 238627 ImageUploadedByJamiiForums1427548792.111716.jpg
 
Back
Top Bottom