Kwa nini necta hawajatumia majina ya wanafunzi mataokeo haya

eskimo

Member
Joined
Apr 27, 2012
Posts
21
Reaction score
3
nimesikitishwa na kitendo cha NECTA cha kutotumia majina ya wanafunzi badala yake wametumia namba. kwa jinsi matokeo yalivyomabaya wanafunzi wengi watadanganya namba zao au watakuwa wagumu kutoa namba zao sahihi. au ni kwa sababu ya MWANAISHA aliyemaliza mwaka jana ikawa gumzo????
 
Teh! Division mwanaisha noma,mwaka kesho watatoa no za shule tu maana gumzo limerud kwenye majina ya wakubwa wenyewe j.k sec
 
unataka ujue matokeo yao ili iweje, nafikiri ni jambo zuri kuna tabia za kuwanyanyasa watu waliofeli iwe kwa bahati mbaya au amefeli kutokana na uwezo wake. ukumbuke kufeli mtihani sio kufeli maisha. huu ni mfumo mmojawapo unaoweza kuchochea vipaji vya watu lakini wakati mwingine anafanikiwa sana hata kama alifeli darsa la 7 kuliko hata mwenye PhD. JAMBO LA MSINGI NI KULE KUJITAMBUA HUO NDIO UKOMBOZI WA MAISHA. KAMA UNA AJIRA ZA KUWAPA SUBIRI WATAKUL;ETEA HIVYO VYETI UVIKAGUE KAMA WNAFAA AU LA. MATOKEO YA MTU IS NOT A PUBLIC GOOD. NI KWELI KITENDO KILICHOFANYWA MWAKA JANA KUHUSIANA NA MTOTO WA RAIS WETU HAKIKUWA CHA KIUNGWANA HATA KIDOGO HUWEZI JUA ALIVYUMIZWA. SIJUI YALE MALUMBANO YALIMSAIDIAJE. LAKINI PIA KUNA MMOJA alijinyonga
 
Bongo hamna privacy.

Waweke majina ili iweje?
 
Lol, matokeo yamekuwa mashaka matupu! Uzazi wa sasa nao ni chai ya moto, ukinywa shurti upulize.
 
Mbona hiyo ni llkawaida jamani...? Mimi mwenyewe matokea yangu nilipolea kwa namba tuu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…