Kwa nini Rais Kikwete umeamua kuihujumu Jamuhuri ya Muungano?

Kwa nini Rais Kikwete umeamua kuihujumu Jamuhuri ya Muungano?

tpmazembe

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
2,469
Reaction score
586
Mhe Rais wakati unakabidhiwa nchi hii na aliyekutangulia nchi hii ilikuwa moja,katiba ya zanzibar ilitambua zanzibar kama sehemu ya jamuhuri ya muungano wa tanzania.

Wewe ulipoingia madarakani ukaruhusu nchi mpya kuzaliwa ndani ya Jamuhuri ya muungano,pale zanzibar ilipobadili katiba na kujiita nchi.Haya yalifanyika bila ridhaa ya wananchi wote wa jamuhuri ya muungano.kwa hilo ninapokuita kuwa umeihujumu jamuhuri nakusimanga au ni ukweli ulio wazi?.

Mhe Rais unatambua vyema kabisa kuwa hata mwasisi wa Taifa hili alijenga nchi moja,yenye serikali inayotambulika kimataifa moja na ile ya zanzibar kwa ajili ya zanzibar pekee. kwa maana hiyo Nyerere alijenga umoja. sasa unapoanzisha nchi ndani ya nchi tukueleweje?umekusudia kuligawa taifa vipande vipande?.

Mhe Rais pamoja na kuihujumu jamuhuri hukutosheka nalo ukaona hujuma uipeleke mpaka ndani ya chama chako cha ccm ambacho kimekupa uenyekiti, Mhe Rais unaposhiriki vikao na kuwa na msimamo ya serikali mbili ndani ya nchi mbili unakuwa na maana gani?Mwasisi wa chama chako na Taifa hili alipotoa msimamo wa serikal mbili kulikuwa na nchi moja,ila wewe unachanganya vichwa wanachama wako kuwaamba wakubali mfumo usio kuwepo tangu awali.
 
Rais kikwete pamoja na kuwa mwenyekiti wa ccm aliruhusu wana ccm zanzibar kupitisha kitu kisichokuwepo.Kikwete anachojua ni kutenganisha watu.kazi yake kubwa kutenganisha na sio kuunganisha.hata udini umeibuka sana katika utawala wake.
 
mwaka 1990 ,Nyerere alikataa mapendekezo ya serikali tatu kwa nia njema kabisa.Nyerere alijua nchi ni moja,miaka hiyo zanzibar hawakujiita nchi, wala hawakuwa na wimbo wala bendera wala majeshi yanayotambulika kikatiba kama JKU au KMKM.Hivyo nyerere akaona hakuna haja ya serikali tatu kutambiana utanganyika na uzanzibar ni ujinga.Rais kikwete umejenga mazingira tofauti kabisa ambayo hayafai tena serikali mbili.

Inatumika nguvu kuwashawishi wana ccm wote nchini kukubali serikali mbili badala ya kutumika nguvu ndogo kuwashawishi wana ccm waammend katiba yao barazani kwao.
 
chadema atatapatapa sana kwa suala hili,bungen ccm watapitisha serkal 2 na mtaani ambapo wanaccm ni wengi watapitisha serkal 2 kwenye kura ya maon rejea matokeo ya uchaguz mkuu
 
kwa sababua hujuma ndio imani yake kuu..kwa sababu haamini ktk mipaka ya nchi,labda wakiwa madarakani tuu,otherwise ana ndugu wengi wa kiutamaduni duniani.
 
chadema atatapatapa sana kwa suala hili,bungen ccm watapitisha serkal 2 na mtaani ambapo wanaccm ni wengi watapitisha serkal 2 kwenye kura ya maon rejea matokeo ya uchaguz mkuu

tatizo sio kupitishwa.hata ikipitishwa ni batili. sio misingi aliyotuachia mwasisi wetu
 
JK malipo ni hapa hapa Duniani usijefikiria labda haya yote unayofanya tunayafurahisi laa hasha!

Watu wamekusihi sana kwa busara,hekima na uadilifu mkubwa hasa pale ulipofanya kinyume lakini mara zote JK kupitia wasaidizi wake amepuuza ushauri na kuwa hasikii.

Tunategemea mengi ya ajabu utakapotoka madarakani kuyaona na kuyasikia sasa hapo utaishi vibaya sana kwa maana ya kutoisikia ya ya Wengi ni Sauti ya Mungu(Ukiikataa unamkataa Mungu).
 
Mamtu mna malengo yenu iacheni Znz kivyake na tanganyika kivyake
 
mwaka 1990 ,Nyerere alikataa mapendekezo ya serikali tatu kwa nia njema kabisa.Nyerere alijua nchi ni moja,miaka hiyo zanzibar hawakujiita nchi, wala hawakuwa na wimbo wala bendera wala majeshi yanayotambulika kikatiba kama JKU au KMKM.Hivyo nyerere akaona hakuna haja ya serikali tatu kutambiana utanganyika na uzanzibar ni ujinga.Rais kikwete umejenga mazingira tofauti kabisa ambayo hayafai tena serikali mbili.

Inatumika nguvu kuwashawishi wana ccm wote nchini kukubali serikali mbili badala ya kutumika nguvu ndogo kuwashawishi wana ccm waammend katiba yao barazani kwao.

Usituletee
mambo ya Nyerere hapa!

Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
 
Rais kikwete pamoja na kuwa mwenyekiti wa ccm aliruhusu wana ccm zanzibar kupitisha kitu kisichokuwepo.Kikwete anachojua ni kutenganisha watu.kazi yake kubwa kutenganisha na sio kuunganisha.hata udini umeibuka sana katika utawala wake.


Hivikatiba ya Tanganyika itaanza lini?
 
JK malipo ni hapa hapa Duniani usijefikiria labda haya yote unayofanya tunayafurahisi laa hasha!

Watu wamekusihi sana kwa busara,hekima na uadilifu mkubwa hasa pale ulipofanya kinyume lakini mara zote JK kupitia wasaidizi wake amepuuza ushauri na kuwa hasikii.

Tunategemea mengi ya ajabu utakapotoka madarakani kuyaona na kuyasikia sasa hapo utaishi vibaya sana kwa maana ya kutoisikia ya ya Wengi ni Sauti ya Mungu(Ukiikataa unamkataa Mungu).

Kweli mkuu huyu jamaa.akitoka madarakani watamgeuka nakweli tutasikia madudu mengi
 
Cdm mnatumia vibaya jina la nyerere na kumbukeni njia mwongo ni fupi. 2015 mtapondana mawe
 
Mhe Rais wakati unakabidhiwa nchi hii na aliyekutangulia nchi hii ilikuwa moja,katiba ya zanzibar ilitambua zanzibar kama sehemu ya jamuhuri ya muungano wa tanzania.

Wewe ulipoingia madarakani ukaruhusu nchi mpya kuzaliwa ndani ya Jamuhuri ya muungano,pale zanzibar ilipobadili katiba na kujiita nchi.Haya yalifanyika bila ridhaa ya wananchi wote wa jamuhuri ya muungano.kwa hilo ninapokuita kuwa umeihujumu jamuhuri nakusimanga au ni ukweli ulio wazi?.

Mhe Rais unatambua vyema kabisa kuwa hata mwasisi wa Taifa hili alijenga nchi moja,yenye serikali inayotambulika kimataifa moja na ile ya zanzibar kwa ajili ya zanzibar pekee. kwa maana hiyo Nyerere alijenga umoja. sasa unapoanzisha nchi ndani ya nchi tukueleweje?umekusudia kuligawa taifa vipande vipande?.

Mhe Rais pamoja na kuihujumu jamuhuri hukutosheka nalo ukaona hujuma uipeleke mpaka ndani ya chama chako cha ccm ambacho kimekupa uenyekiti, Mhe Rais unaposhiriki vikao na kuwa na msimamo ya serikali mbili ndani ya nchi mbili unakuwa na maana gani?Mwasisi wa chama chako na Taifa hili alipotoa msimamo wa serikal mbili kulikuwa na nchi moja,ila wewe unachanganya vichwa wanachama wako kuwaamba wakubali mfumo usio kuwepo tangu awali.

Huyo nyerere ndie alieleta matatizo kwa udikteta wake,kwanini alazimishe muungano wakati wazanzibr hawautaki?kamfukuza jumbe urais kisa kahoji muungano,hizi ni nchi 2 huru,wazanzbr wamechoka kutawaliwa na mkoloni mweusi aliejivika koti la muungano.
 
Wazanzibar wameachwa wafanye watakavyo ndani ya muungano huku, watanganyika wakibanwa kwa lengo la kuikandamiza tanganyika! Wanasiasa kutoka tanganyika ni wasaliti ndani ya mfumo wa serikali 3!
 
Jk kamuuzia Zanzibar Amani Karume na rafiki zake, matokea yake TRA ikafukuzwa Zanzibar, Meli za Mihadarati, Kuzama kwa Meli ovyo, Uamsho kuanzishwa, Wabara kupigwa marufuku kununua Ardhi na kuondolewa kwenye ajira, Rais wa Nchi jirani ( karume) kawatukana Watanzania wote Dodoma japo alikuwa amekunywa viroba kama kawaida yake. Na mengine mengi.
 
Hakuna kosa lolote alilofanya JK. Zanzibar ilikuwa na itaendelea kuwa na haki ya kutengeneza katiba yake na kujitambulisha kama nchi kama ambavyo Tanganyika inayo haki kama hiyo. Tatizo baadhi ya wananchi wa Tanganyika hawaitaki nchi yao. Wamezoea kuinyonya ZAnzibar. Hawa ni kupe. Ndiyo maana hii leo kuna wimbo wa serikali mbili
 
Huyo nyerere ndie alieleta matatizo kwa udikteta wake,kwanini alazimishe muungano wakati wazanzibr hawautaki?kamfukuza jumbe urais kisa kahoji muungano,hizi ni nchi 2 huru,wazanzbr wamechoka kutawaliwa na mkoloni mweusi aliejivika koti la muungano.

kwani huyo jumbe urais alipigiwa kura na wazanzibar? karume ndiye aliyeomba kuungana
 
Hakuna kosa lolote alilofanya JK. Zanzibar ilikuwa na itaendelea kuwa na haki ya kutengeneza katiba yake na kujitambulisha kama nchi kama ambavyo Tanganyika inayo haki kama hiyo. Tatizo baadhi ya wananchi wa Tanganyika hawaitaki nchi yao. Wamezoea kuinyonya ZAnzibar. Hawa ni kupe. Ndiyo maana hii leo kuna wimbo wa serikali mbili
Mtu anayeelewa maana ya upamoja na muungano hawezi kuwa na sera za umimi ubinafsi, tunapokuwa na taifa moja kubwa mwananchi anakuwa huru na wigo mpana wa kiuchumi.
 
Tuna mlaumu mzee wa watu bure,huu Muungano ulikuwa unashida nyingi na kunakundi hasa Zanzibar nikama walilazimishwa kuwa humu,katika tawala zote ilitumika nguzu kubwa kuyaficha haya hata ikiwemo watu kwenda uhamishoni au kuuwawa lakini Kikwete kwakuwa nimuuni wa uwazi akakubari kila mmoja atoe dukuduku lake katika utawala wake,kwanza ndo raisi wa kwanza kukiri nyufa katika muungano nakutumia kila namna kulikabiri hili..
 
Back
Top Bottom