KIKOSI cha timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars kimesafiri kwa zaidi ya saa 10 hadi katika mji mdogo kabisa wa Kartepe hapa nchini Uturuki kwa ajili ya kuweka kambi.
Kambi hiyo ni kwa ajili ya kujiwinda ili kuwa fiti kabla ya mechi ya kuwania kucheza Kombe la Mataifa aAfrika dhidi ya Nigeria, mechi itakayopigwa Septemba 5 jijini Dar es Salaam.
Kabla haitakuwa mechi ndogo na Stars ambayo kwa mara ya kwanza, mara nyingine timu hiyo inanilewa na makocha wote wazalendo.
Safari:
Safari ya Stars kuja hapa Uturuki ilianzia Dar es Salaam na ndege iliondoka saa 9:45 usiku na kuwasili Istanbul Uturuki saa 4:45 asubuhi ikiwa ni saa saba bila ya kupumzika angani.
Safari hiyo ndeefu iliwafanya wachezaji wa Stars kuonekana wakiwa wamechoka sana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ataturk na baada ya hapo safari ya kwenda kambini iliyochukua saa tatu na shee ilianza kwa basi.
Awali ilionekana ni kama safari fupi tu, lakini haikuwa hivyo baada ya wachezaji kujikuta wakisafiri kwa saa tatu kutoka Istanbul hadi katika mji wa Izmil ambao ni wa tatu kwa ukubwa hapa Uturuki baada ya Istanbul na Ankara.