Kwa nini tulipigania Uhuru wa Tanganyika?.

Kwa nini tulipigania Uhuru wa Tanganyika?.

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Hali ya mambo inavyokwenda kwenye nchi hii inafanya turejee nyuma na kujihoji kuwa kwa nini "Tulipigania Uhuru wa Tanganyika?".

Damu za wazee wetu zinatulilia, zinahoji uhalali wa sisi kurithi nchi nchi hii,

Madini tumeshindwa kuyalinda na sasa nchi imebaki ukiwa, nchi imepasuliwa miamba kuanzia kas hadi kusi, nchi imebaki matundu tena wasivyo na aibu wameyacha wazi bila kufukia,

Ndio, wangefukia na nini wakati vifusi vyote wamepakia kwenda navyo ulaya?

Wamemaliza madini sasa wamehamia kwenye mbuga, huku jangiri sio mgeni bali ni serikali yenyewe tuliyoipa dhamana!

Sasa watanzania wanasubiri msaada wa mamlaka za Hong Kong ili kubaini wezi, jiulizi zimepitaje bandarini mpaka mashariki ya mbali?

Hivi tumwamini nani kama tuliyempa mamlaka hasimamii sheria za nchi?

Mwezi juzi tu wamekwapua twiga wetu wazimawazima na kuwakunja mpaka wakatosha kwenye ganda la kiberiti na wakatokomea nao mpaka Qatar.
Ndege ya jeshi la Qatar ndio iliyotumika ubeba twiga na sungura wetu wakiwa hai!


Hebu jiulize ni nchi gani duniani ambayo ndege ya kijeshi ya kigeni inaweza kutua bila usalama na IKULU vya nchi hiyo kuwa na taarifa za msingi?

Hali ya kijamii ni mbaya sana, elimu inazidi kudorola, afaya imebaki mfukoni mwa mgonjwa,

Kwaujumla hawatupi nafasi tupumue, wakimaliza hapa wanahamia pale!

Swali ni kwa nini tulipigania Uhuru wa Tanganyika?.

Kama ni ili tujitawale mbona siasa zetu chafu?

Kama ni ili tuwe huru kutoka mikononi mwa wakoloni wanyonyaji, sasa mbona tupo na mkoloni mweusi ccm mbaya kuliko mzungu mwenye pua ndefu?!

Naamini taifa limewakosea wale wazee wetu 17 wapigania uhuru wa nchi yetu, na damu yao inatulilia,

Hebu tutafute maana halisi ya Watanganyika kudai uhuru ilikuwa ni nini?

Na je tunaishi katika lengo hilo?
 
CCM ndo imesababisha haya yote, watatoka tu madarakani ingawa wanajifanya miungu,siku wakiwa chama pinzani ndo watakumbuka kuomba dua.
 
Hali ya mambo inavyokwenda kwenye nchi hii inafanya turejee nyuma na kujihoji kuwa kwa nini "Tulipigania Uhuru wa Tanganyika?".

Damu za wazee wetu zinatulilia, zinahoji uhalali wa sisi kurithi nchi nchi hii,

Madini tumeshindwa kuyalinda na sasa nchi imebaki ukiwa, nchi imepasuliwa miamba kuanzia kas hadi kusi, nchi imebaki matundu tena wasivyo na aibu wameyacha wazi bila kufukia,

Ndio, wangefukia na nini wakati vifusi vyote wamepakia kwenda navyo ulaya?

Wamemaliza madini sasa wamehamia kwenye mbuga, huku jangiri sio mgeni bali ni serikali yenyewe tuliyoipa dhamana!

Sasa watanzania wanasubiri msaada wa mamlaka za Hong Kong ili kubaini wezi, jiulizi zimepitaje bandarini mpaka mashariki ya mbali?

Hivi tumwamini nani kama tuliyempa mamlaka hasimamii sheria za nchi?

Mwezi juzi tu wamekwapua twiga wetu wazimawazima na kuwakunja mpaka wakatosha kwenye ganda la kiberiti na wakatokomea nao mpaka Qatar.
Ndege ya jeshi la Qatar ndio iliyotumika ubeba twiga na sungura wetu wakiwa hai!


Hebu jiulize ni nchi gani duniani ambayo ndege ya kijeshi ya kigeni inaweza kutua bila usalama na IKULU vya nchi hiyo kuwa na taarifa za msingi?

Hali ya kijamii ni mbaya sana, elimu inazidi kudorola, afaya imebaki mfukoni mwa mgonjwa,

Kwaujumla hawatupi nafasi tupumue, wakimaliza hapa wanahamia pale!

Swali ni kwa nini tulipigania Uhuru wa Tanganyika?.

Kama ni ili tujitawale mbona siasa zetu chafu?

Kama ni ili tuwe huru kutoka mikononi mwa wakoloni wanyonyaji, sasa mbona tupo na mkoloni mweusi ccm mbaya kuliko mzungu mwenye pua ndefu?!

Naamini taifa limewakosea wale wazee wetu 17 wapigania uhuru wa nchi yetu, na damu yao inatulilia,

Hebu tutafute maana halisi ya Watanganyika kudai uhuru ilikuwa ni nini?

Na je tunaishi katika lengo hilo?
ni maombi tu ndiyo yataiinua tanzania sio siasa wala wasomi
 
CCM ndo imesababisha haya yote, watatoka tu madarakani ingawa wanajifanya miungu,siku wakiwa chama pinzani ndo watakumbuka kuomba dua.

ndugu yangu mungu mwenyewe ndo anaweza kututoa hapa tulipo ni toba na maombi ndiyo yataiinua TANZANIA
 
ni maombi tu ndiyo yataiinua tanzania sio siasa wala wasomi

Mkuu mtz one

Tupatie mfano wa nchi moja duniani iliyoinuka kwa kutegemea maombi tu. Nchi hiyo ambayo haina nafasi kwa siasa wala wasomi hawaruhusiwi kutumia taaluma yao kuiinua nchi.

Au nimeshindwa kukufahamu?

Nimeshasikia mara nyingi wanasiasa wanawaomba "viongozi" wa dini/ kiroho waiombee nchi. Je wamekataa kuiombea Tanzania?
 
Mkuu mtz one

Tupatie mfano wa nchi moja duniani iliyoinuka kwa kutegemea maombi tu. Nchi hiyo ambayo haina nafasi kwa siasa wala wasomi hawaruhusiwi kutumia taaluma yao kuiinua nchi.

Au nimeshindwa kukufahamu?

Nimeshasikia mara nyingi wanasiasa wanawaomba "viongozi" wa dini/ kiroho waiombee nchi. Je wamekataa kuiombea Tanzania?
utakapoiombea nchi baraka hao wasomi watatumia usomi wao na utaleta manufaa ni miaka mingapi tuna wasomi lakini tuko hapa?? ni mungu tu ndo atakae tuokoa
 
Hali ya mambo inavyokwenda kwenye nchi hii inafanya turejee nyuma na kujihoji kuwa kwa nini "Tulipigania Uhuru wa Tanganyika?".


Swali ni kwa nini tulipigania Uhuru wa Tanganyika?.

Kama ni ili tujitawale mbona siasa zetu chafu?


Hebu tutafute maana halisi ya Watanganyika kudai uhuru ilikuwa ni nini?

Na je tunaishi katika lengo hilo?

Ndugu Yericko

Tulipigania uhuru wa Tanganyika ili baadae tubadilishe jina tu. Jina Tanganyika lilikuwa la hovyo.
Angalia sasa tuna Tanzania bara, ukipenda sema Tanzania tu.


Bado tunaishi katika lengo hilo. Kama unatamani malengo ya kupigania Tanganyika basi tudai Tanganyika yetu kwanza. Baada ya kuipata tena Tanganyika ndio tutaanza safari mpya.

Tanzania haina mwenyewe ndio sababu ya hao pua refu wanakuja kujichumia shamba la bibi.

Tanzania ni mazingaombwe ya CCM ya kutugawia umaskini na ahadi hewa.

Tulikubali kupigwa changa la macho. Unazungumzia uhuru wa Tanganyika wakati Tanganyika haipo?

Au wewe unafikiri Tanganyika ipo? Ukiwa na majibu ya hili suali basi itasaidia "kujielewa"!

Tafuta jibu katika katiba ya nchi, sheria za nchi au popote pale. Ukiikuta Tanganyika huko, nitoe na mimi usingizini.

Na ukipata muda pitia hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/334649-tundu-lissu-na-kiini-macho-cha-muungano.html
 
Mkuu mtz one

Tupatie mfano wa nchi moja duniani iliyoinuka kwa kutegemea maombi tu. Nchi hiyo ambayo haina nafasi kwa siasa wala wasomi hawaruhusiwi kutumia taaluma yao kuiinua nchi.

Au nimeshindwa kukufahamu?

Nimeshasikia mara nyingi wanasiasa wanawaomba "viongozi" wa dini/ kiroho waiombee nchi. Je wamekataa kuiombea Tanzania?
kUNA KITU KIITWACHO act of god. Ujamaa na kijitegemea pamoja na kutufanya watumwa na kutubana sana uliteketezwa na act of god. Yaani URRUSI ilisambaratika na ukomunisti kufa na nchi zote zote zilizobobea katika ukomunisti kumlaani mrusi vibaya sana. CCM haikuwa na ubavu kabisaa wa kuzuia mageuzi yasije hapa tanzania maana hilo lilikuwa azimio la dunia nzima kila nchi iwe na demokrasi.

Kuhusu kuhujumiwa nchi vibaya sana kiasi cha sisi kuhoji kwa nini tulidai uhuru wa tanganyika. Hili ni hoja bora sana na inatia uchungu mno kuitafakari. Ila kabla ya kuwalaumu hawa wanaotutesa hivi sasa, jaribu kuwa mkweli na kuhoji matumizi mabaya ya pesa za serikali ya sweeden iliyokuwa inatupatia 5% ya msada kila mwaka katika bajeti yao ili tuboreshe maisha yetu na kuijenga tanzania. sasa jiulize hizo pesa zimefanya kitu gani kinachooneka tangia mwaka 1978 mpaka leo?

serikali wakati huo haikuwa na vyuo vya ualimu vya kutosha badala ya kujenga vyuo vya ualimu vingi ikaanzisha ualimu wa UPE. watu walikuwa wanarudia darasa la saba mara kumi kumi, badala ya kujenga shule za secondari mpaka ngazi ya kata ili kuondoa adha ya kurudia darasa la saba mara nyingi, wao ndio kwanza wakaanzisha chuo cha sasa hombolo na handeni ili makada wakasome huko!

Uhuni wa kutuhujumu haki yetu ya maendeleo haukuanzia leo, bali ulianzia tangia miaka ya 1970 serikali ilipovunja serikali ya mitaa. kuna viongozi walifikia mpaka kupeleka watoto wao wakaishi sweeden ili wafaidi hizo pesa za misaada. na mara baada ya kufa kwa ujamaa na kujitegemea tuu, wakawarudisha watoto wao hapa nchini kwa haibu. je na hilo sio dhambi la nguvu.?
 
kUNA KITU KIITWACHO act of god. Ujamaa na kijitegemea pamoja na kutufanya watumwa na kutubana sana uliteketezwa na act of god. ..... je na hilo sio dhambi la nguvu.?
Tango73

Act of god ndio nini tena, mkuu?

Dhambi ni kupewa asilimia 3 na wasweden au kuweka mfukoni hiyo asilimia tatu?

Hizi act of god ziko ngapi?.... Sijakufahamu umekusudia nini.
Upunguze kula matango au vitango.
 
tumemuondosha mzungu tumemueka mnyapara bado tumetawaliwa mpaka leo hebu kule uk wanayo ofisi ya makoloni kwanini? baya zaidi tuna mnyapara bora yule mkoloni tunajuwa ana hisia nasi lakini huyu mnyapara ndio anaonesha kule kwa mkoloni kuwa kazi anaweza
Agalia viongozi wote wa upinzani wanakwenda lalamika kwa wazungu kwani huko ndio kwenye mamlaka sio huku kwenye mnyapara yeye haezi kufanya lolote na tupo hapa kama CCM hawatokwenda tofauti na mkoloni basi CCM daima
 
Kwa mfano mmoja wa haraka haraka, tunaweza kusema labda ni mzee gani aliyemwaga damu akipigania uhuru wa Tanganyika?

Ieleweke mkuu kuwa katika vita vya ukombozi damu ya mwanaukombozi sio lazimi iwe ya aliyezikwe,

Damu ya mtu ni pamoja na jasho lake! Sio lazima awe alikufa!
 
CCM ndo imesababisha haya yote, watatoka tu madarakani ingawa wanajifanya miungu,siku wakiwa chama pinzani ndo watakumbuka kuomba dua.

Na watanzania tunatakiwa kuelimishana ili wote tuamke, ukombozi mzuri ni ule uendao na elimu ya uraia!
 
Unazuga!

Ulichemka kusema damu za wazee wetu zinatulilia.

Hakuna mzee aliyemwaga damu akipigania uhuru wa Tanganyika.

Kwahiyo unamaana kuwa hiyo ndio sababu ya yanayotokea leo katika nchi hii?

Watanganyika hawakupigania UHURU wa nchi yao?

Unamaana UHURU wa Tanganyika wale wazee 17 waliletewa kwenye kisosi tu?

Hebu fafanua zaidi mkuu!
 
Tango73

Act of god ndio nini tena, mkuu?

Dhambi ni kupewa asilimia 3 na wasweden au kuweka mfukoni hiyo asilimia tatu?

Hizi act of god ziko ngapi?.... Sijakufahamu umekusudia nini.
Upunguze kula matango au vitango.

Hehee umenikumbusha machungu ya kilo 100 za dhahabu sisi watanzania tunapewa kilo tatu (3) tu tena hatupewi yote kwapamoja!
 
Back
Top Bottom