Kwa Nini Tunamgeuza Warioba Kama Mbuzi wa Azazeli?

Kwa Nini Tunamgeuza Warioba Kama Mbuzi wa Azazeli?

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
Sipati picha lawama zote kutupiwa Jaji Warioba kwenye Rasimu ya Katiba kana kwamba yeye ndio mbuzi wa Kafara (Scapegoat) hasa kwenye suala la Serikali Tatu, Utasikia Warioba amsaliti Nyerere, Warioba ndio chanzo cha Serikali Tatu, CCM yamtuhumu Warioba serikali tatu etc etc


  1. Tume Tumeiteua wenyewe iratibu maoni ya Katiba na Mwenyekiti (Moderator) akawa Jaji Warioba
  2. Maoni tumeyatoa wenyewe kama Watanzania na kwa mujibu wa ripoti 61% wamegusia Muungano
  3. Tumeuinda Mabaraza ya Kata yakapeleka maoni Tume
  4. Tunalo Bunge Maalum la Katiba Linakuja
  5. Why igeuke kuwa ni Mawazo ya Warioba?
 
Waswahili wanasema " mbaazi ukinyauka, husingizia maji"! Tume imechukua maoni kutoka kwa wananchi kwa njia mbalimbali. Haiwezekani Mzee Warioba achakachue kutaka Serikali tatu wakati Wajumbe wengine wa Tume walioteuliwa wanatoka Zanzibar na ambao asilani hawataki serikali tatu!
 
Sipati picha lawama zote kutupiwa Jaji Warioba kwenye Rasimu ya Katiba kana kwamba yeye ndio mbuzi wa Kafara (Scapegoat) hasa kwenye suala la Serikali Tatu, Utasikia Warioba amsaliti Nyerere, Warioba ndio chanzo cha Serikali Tatu, CCM yamtuhumu Warioba serikali tatu etc etc


  1. Tume Tumeiteua wenyewe iratibu maoni ya Katiba na Mwenyekiti (Moderator) akawa Jaji Warioba
  2. Maoni tumeyatoa wenyewe kama Watanzania na kwa mujibu wa ripoti 61% wamegusia Muungano
  3. Tumeuinda Mabaraza ya Kata yakapeleka maoni Tume
  4. Tunalo Bunge Maalum la Katiba Linakuja
  5. Why igeuke kuwa ni Mawazo ya Warioba?

Sisi waTanzania tunapenda sana mijadala. However, Generali Ulimwengu ndiye pekee naona pgram zake ziko focused, hasa katika hili!
 
Tena mtu 'eti mhadhiri wa UDOM' kama Bashiru Ali analeta hoja za ajabu kabisa kabisa, hivi hao wanafunzi wake watakuwaje kwa taifa letu? Inasikitisha.
 
Hata jana kwenye marumbano ya hoja naona ITV walichagua watu wao kwanza ili waje kumchambua Warioba. ITV nimepoteza imani nanyi.
 
Watu wamechoka kweli kweli kufikiri, wanamjadili mtu badala ya kujadili suala lililopo mezani. Wengine wamefikia hatua ya kuhoji integrity ya mzee Warioba.
Kazi ipo ndani ya nchi hii, watu wanadai eti 'sisi hatujatoa maoni hayo' kana kwamba tume ilijifungia chooni kisha ikaja na rasmu. Mungu tusamehe, tumejawa hofu hata hatutumiii akili ipasavyo, hofu ya tumbo
 
Mimi binafsi nilishiriki kwenye mchakato. Nilipata fursa ya kukutana na tume nikiwa na kundi la watu wapatao ishirini na tano. Kuhusu suala la Muungano timu yangu ilipendekeza SERIKALI 3. Sababu muhimu ilikuwa kama ifuatavyo:
  1. Kama Muungano ulikuwa wa nchi mbili, ni vema hizo nchi zikaendelea kuwa na historia yake (Serikali ya Tanganyika.....Serikali ya Mapinduzi) ili kuwakumbusha vizazi kuwa Tanzania ilitokana na nia njema ya kuunganisha nguvu ya pamoja (Umoja ni Nguvu) ili kuweza kutetea maslahi yetu.
  2. Kwa sasa muundo wa serikali mbili hauleti picha kama kuna nchi ziliungana wakati moja ime-maintain identity yake (SMZ) na nyingine imesahaurika (Tanganyika). Hii haileti usawa kabisa
  3. Mgawanyo wa rasilimali na fursa utaendana sawa na mchango wa mwanachama - proportionate distribution based on equity not on equal! Kama Zanzibar ni raia mil 6 hawawezi kudai haki sawa na raia milioni sitini (huu ni mfano tu), hawawezi kuwa na nafasi za uongozi sawa. Similar hata mgawanyo wa fedha utaendana na mikakati ya pamoja kwa kuzingatia mahitaji ya makundi mbalimbali
  4. Serikali kuu (Muungano) itakuwa na watendaji wachache....ambayo wanakuwa na political power kwa zile za Muungano kwa kufuata mijadala, ushawishi na makubaliano

Sasa, endapo mfumo wa SERIKALI 3 haukubariki, tuliishauri tume ipendekeze Serikali1. Sababu za msingi ni hizi

  1. Hapo hakuna mimi Mpemba, Mgazija wala Mtanganyika. Wote tunakuwa watanzania
  2. Mgawanyo wa rasilimali utawekwa sawa bila kujali ni visiwani au bara, wote ni watz wanahitaji huduma toka serikali yao
  3. Itapunguza maneno yasiyo ya lazima kusema kuna sheria ya Znz na sharia ya bara. Tutaongozwa na serikali moja tu.
  4. Itaondoa mijadala ya Zanzibar ni nchi /////si nchi. Na je Tanganyika ni nchi au si/// nchi? Itakuwa nchi moja, lugha moja taifa moja na jamii moja ya watanzania
  5. Hakutakuwepo kubaghuliwa wabara waendapo Zanzibar maana ilmradi ni Mtz ruksa kuishi popote na kuendeleza maisha yako
  6. Serikali ya mzigo (mawaziri kibao) itakuwa imeondoka, na hivyo hela nyingi kuingizwa kwenye maendeleo badala ya kuhudumia viogozi. Pia hakutakuwepo na orodha ndefu ya viongozi wastaafu wanaokula pensheni bali orodha itakuwa ndogo
NI UPOTOVU WA NIDHAMU KUMSHAMBULIA MZEE WARIOBA, LABDA WALE WANAOMSHAMBULIA HAWAKUPATA MUDA (HAWAKUTAKA KWENDA) KUKUTANA NA TUMI YA MZEE WARIOBA WAKASUBIRI KUJA KUMSULUBISHA KWENYE VYOMBO VYA HABARI. HII SIO SAHIHI

  1. Watu wamechoka kweli kweli kufikiri, wanamjadili mtu badala ya kujadili suala lililopo mezani. Wengine wamefikia hatua ya kuhoji integrity ya mzee Warioba.
Kazi ipo ndani ya nchi hii, watu wanadai eti 'sisi hatujatoa maoni hayo' kana kwamba tume ilijifungia chooni kisha ikaja na rasmu. Mungu tusamehe, tumejawa hofu hata hatutumiii akili ipasavyo, hofu ya tumbo
 
pole sana mzee wetu warioba kazi ilikuwa ya tume nzima leo lawama kwako.Ila kumbuka watanzania wengi shule hamna kama wale wa Bongo movie wasamehe bure Mzee wangu na katiba bora kwa Maslahi ya Nchi yetu Itapatikana
 
pole sana mzee wetu warioba kazi ilikuwa ya tume nzima leo lawama kwako.Ila kumbuka watanzania wengi shule hamna kama wale wa Bongo movie wasamehe bure Mzee wangu na katiba bora kwa Maslahi ya Nchi yetu Itapatikana

umenena vyema mtumishi
 
tunataka mifano hai namna hii
Mimi binafsi nilishiriki kwenye mchakato. Nilipata fursa ya kukutana na tume nikiwa na kundi la watu wapatao ishirini na tano. Kuhusu suala la Muungano timu yangu ilipendekeza SERIKALI 3. Sababu muhimu ilikuwa kama ifuatavyo:
  1. Kama Muungano ulikuwa wa nchi mbili, ni vema hizo nchi zikaendelea kuwa na historia yake (Serikali ya Tanganyika.....Serikali ya Mapinduzi) ili kuwakumbusha vizazi kuwa Tanzania ilitokana na nia njema ya kuunganisha nguvu ya pamoja (Umoja ni Nguvu) ili kuweza kutetea maslahi yetu.
  2. Kwa sasa muundo wa serikali mbili hauleti picha kama kuna nchi ziliungana wakati moja ime-maintain identity yake (SMZ) na nyingine imesahaurika (Tanganyika). Hii haileti usawa kabisa
  3. Mgawanyo wa rasilimali na fursa utaendana sawa na mchango wa mwanachama - proportionate distribution based on equity not on equal! Kama Zanzibar ni raia mil 6 hawawezi kudai haki sawa na raia milioni sitini (huu ni mfano tu), hawawezi kuwa na nafasi za uongozi sawa. Similar hata mgawanyo wa fedha utaendana na mikakati ya pamoja kwa kuzingatia mahitaji ya makundi mbalimbali
  4. Serikali kuu (Muungano) itakuwa na watendaji wachache....ambayo wanakuwa na political power kwa zile za Muungano kwa kufuata mijadala, ushawishi na makubaliano

Sasa, endapo mfumo wa SERIKALI 3 haukubariki, tuliishauri tume ipendekeze Serikali1. Sababu za msingi ni hizi

  1. Hapo hakuna mimi Mpemba, Mgazija wala Mtanganyika. Wote tunakuwa watanzania
  2. Mgawanyo wa rasilimali utawekwa sawa bila kujali ni visiwani au bara, wote ni watz wanahitaji huduma toka serikali yao
  3. Itapunguza maneno yasiyo ya lazima kusema kuna sheria ya Znz na sharia ya bara. Tutaongozwa na serikali moja tu.
  4. Itaondoa mijadala ya Zanzibar ni nchi /////si nchi. Na je Tanganyika ni nchi au si/// nchi? Itakuwa nchi moja, lugha moja taifa moja na jamii moja ya watanzania
  5. Hakutakuwepo kubaghuliwa wabara waendapo Zanzibar maana ilmradi ni Mtz ruksa kuishi popote na kuendeleza maisha yako
  6. Serikali ya mzigo (mawaziri kibao) itakuwa imeondoka, na hivyo hela nyingi kuingizwa kwenye maendeleo badala ya kuhudumia viogozi. Pia hakutakuwepo na orodha ndefu ya viongozi wastaafu wanaokula pensheni bali orodha itakuwa ndogo
NI UPOTOVU WA NIDHAMU KUMSHAMBULIA MZEE WARIOBA, LABDA WALE WANAOMSHAMBULIA HAWAKUPATA MUDA (HAWAKUTAKA KWENDA) KUKUTANA NA TUMI YA MZEE WARIOBA WAKASUBIRI KUJA KUMSULUBISHA KWENYE VYOMBO VYA HABARI. HII SIO SAHIHI

 
Kumkataa ha2mkatai ila suala la serikali 3 ata kipindi cha muungano alimpinga mwl:Nyerere yeye akawa anataka serikari 3 mm naona bora serikali 1iundwe tu.
 
We unaona wanaomlaumu mzee Warioba ni hawa akina bongo muvi na watu waliolishwa maneno tu. Wengi hawana hoja ni kelele tu

sidhani kama hata hao Bongo movi wanajua kinachoendelea kuhusu katiba, wengi wako bize kichama ............
 
Kumkataa ha2mkatai ila suala la serikali 3 ata kipindi cha muungano alimpinga mwl:Nyerere yeye akawa anataka serikari 3 mm naona bora serikali 1iundwe tu.

kwa hiyo unataka kusema ni maoni yake binafsi?
 
pole sana mzee wetu warioba kazi ilikuwa ya tume nzima leo lawama kwako.Ila kumbuka watanzania wengi shule hamna kama wale wa Bongo movie wasamehe bure Mzee wangu na katiba bora kwa Maslahi ya Nchi yetu Itapatikana
nakushukuru sana Dansmith kwa kunielewa
 
Kumkataa ha2mkatai ila suala la serikali 3 ata kipindi cha muungano alimpinga mwl:Nyerere yeye akawa anataka serikari 3 mm naona bora serikali 1iundwe tu.

Mkuu serekali moja haliwezekani,hata nyerere limemshinda,zanzibar haimezeki,zanzibr kwanza.
 
Warioba na tume yote wamefanya kazi kwa uadilifu, tatizo kuna watu katika nchi hii hawapendi kuambiwa ukweli, wamezoea sana kuchakachua kila kitu. Warioba kutokuchakachua maoni ya wananchi kwao imekuwa ni tatizo
 
Back
Top Bottom