Kwa Nini Tunamgeuza Warioba Kama Mbuzi wa Azazeli?

Kwa Nini Tunamgeuza Warioba Kama Mbuzi wa Azazeli?

Wanaopendekeza serikali tatu welewe kuwa wanaelekea kwenye kuuvunja muungano. Pamoja na mawazo mazuri wanayoweza kuwa nayo lakini ndio utakuwa mwisho wa Tanzania. CCM imeliona hilo na imeshtuka.
 
Wanaopendekeza serikali tatu welewe kuwa wanaelekea kwenye kuuvunja muungano. Pamoja na mawazo mazuri wanayoweza kuwa nayo lakini ndio utakuwa mwisho wa Tanzania. CCM imeliona hilo na imeshtuka.

kwa hiyo wewe unapendekeza ngapi mkuu?
 
Wanaopendekeza serikali tatu welewe kuwa wanaelekea kwenye kuuvunja muungano. Pamoja na mawazo mazuri wanayoweza kuwa nayo lakini ndio utakuwa mwisho wa Tanzania. CCM imeliona hilo na imeshtuka.

Serikali moja itavunja Muungano (Zanzibar wana Serikali tayari thus ni sawa na kuwaambia wavunje serikali yao ibaki moja ya Muungano, Ukisema Serikali mbili ni sawa na ku-maintain status quo (ni ubatili na kujilisha upepo)
 
Kada maarufu wa CCM, Peter Kisumo, amemtupia lawama jaji Warioba na kumtuhumu kwamba yeye ndiye chanzo cha serikali tatu-- hoja ambayo imeingizwa kwenye rasimu ya mwisho ya katiba ili ikajadiliwe kwenye bunge la katiba litakaloketi mwezi ujao.
 
tunataka mifano hai namna hii
Mkuu Amavubi. Nyakati nyingi sisi wadanganyika tunadhani mageuzi ya kisera yanakuja kwa kupinga bila kuonesha alternative policies (sera mbadala) ama kuonesha madhara ya utendaji uliopo. Ni vema kubainisha mapungufu, lakini inakuwa bora zaidi tukitoa mapendekezo pia. Kwa bahati mbaya wapenzi wa serikali 2 wametupatia upande mmoja. Lakini wanasahau kuwa miaka 50 ya Muungano inatosha kutambua wapi tumepungukiwa. Hii ni kwamba mjadala huru huchangia kuleta mabadiliko chanya. Hakuna kutishana. Hakuna kunyoosheana vidole bali objectively tunapingana na constructively tunapeana mawazo mbadala. Hii hakuna nani alikuwa mshindi nani ameshindwa, bali wote tunatafuta common good ya watanganyika na wazanzibar kwanza kisha ndo tunaangalia Muungano. Maana bila Tanganyika na Zanzibar, Muungao (yaani Tanzania) haipo!!!!!!!!!!!!
 
Watu wamechoka kweli kweli kufikiri, wanamjadili mtu badala ya kujadili suala lililopo mezani. Wengine wamefikia hatua ya kuhoji integrity ya mzee Warioba.
Kazi ipo ndani ya nchi hii, watu wanadai eti 'sisi hatujatoa maoni hayo' kana kwamba tume ilijifungia chooni kisha ikaja na rasmu. Mungu tusamehe, tumejawa hofu hata hatutumiii akili ipasavyo, hofu ya tumbo
Mkuu, Mungu yupo atawahukumu maana wameisha zowea kudanganya familia zao hivo hawaoni aibu kufanya hivo hadharani.
 
Mkuu Amavubi. Nyakati nyingi sisi wadanganyika tunadhani mageuzi ya kisera yanakuja kwa kupinga bila kuonesha alternative policies (sera mbadala) ama kuonesha madhara ya utendaji uliopo. Ni vema kubainisha mapungufu, lakini inakuwa bora zaidi tukitoa mapendekezo pia. Kwa bahati mbaya wapenzi wa serikali 2 wametupatia upande mmoja. Lakini wanasahau kuwa miaka 50 ya Muungano inatosha kutambua wapi tumepungukiwa. Hii ni kwamba mjadala huru huchangia kuleta mabadiliko chanya. Hakuna kutishana. Hakuna kunyoosheana vidole bali objectively tunapingana na constructively tunapeana mawazo mbadala. Hii hakuna nani alikuwa mshindi nani ameshindwa, bali wote tunatafuta common good ya watanganyika na wazanzibar kwanza kisha ndo tunaangalia Muungano. Maana bila Tanganyika na Zanzibar, Muungao (yaani Tanzania) haipo!!!!!!!!!!!!
Sawa mkuu, lakini hawa wang'ang'aniaji serikali mbili hoja zao ni mbili tu za kumuenzi baba wa taifa Nyerere na kuwa ni sera ya chama cha CCM basi. Matatizo yaliyopo ambayo ni mengi hawayasemi japo yanaonekana dhahiri.
 
Back
Top Bottom