Kwa nini tuwaombee waliokufa?

Kwa nini tuwaombee waliokufa?

G'taxi

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
6,625
Reaction score
8,639
Nimekua najiuliza ni kwa nini mala nyingi hasa mwisho wa mwaka utasikia watu wengi wanakimbia majumbani mwao hasa vijijini na lengo ni kwenda kuwaomba ndugu walioishatangulia kwa maana ya kufa.

Wanaenda mbali na kupeleka maombi yao juu ya maisha yanayowazunguka kwa hao waliokufa,ni kweli kuna maana yoyote au kuna ulazima wa kufanya hili?kama ni kweli MUNGU tunaemuabudu na kuamini kua yupo na ndiyo alietuumba anapata nafasi ipi iwapo tutafikia kupeleka shida zetu kwa wafu?
 
Last edited:
Nimekua najiuliza ni kwa nini mala nyingi hasa mwisho wa mwaka utasikia watu wengi wanakimbia majumbani mwao hasa vijijini na lengo ni kwenda kuwaombea ndugu walioishatangulia kwa maana ya kufa.

wanaenda mbali na kupeleka maombi yao juu ya maisha yanayowazunguka kwa hao waliokufa,ni kweli kuna maana yoyote au kuna ulazima wa kufanya hili?kama ni kweli MUNGU tunaemuabudu na kuamini kua yupo na ndiyo alietuumba anapata nafasi ipi iwapo tutafikia kupeleka shida zetu kwa wafu ?

kwani mungu yupo? Waache wapeleke kwa wafu tu shida zao..angalau wamewahi kuwepo!!
 
kwani mungu yupo? Waache wapeleke kwa wafu tu shida zao..angalau wamewahi kuwepo!!

Ni vyema ungetoa sababu za msingi juu ya kuamini kwako kua MUNGU hayupo...nachotaka mimi kujua ni kwa nini kuwaombea wafu pasipokujua wako wapi,ukisema bola wao wamewahi kuonekana kweni huko walikoenda wewe umewahi kupaona na ukajua wapo mpaka watu wawaombe kutatua shida zao?
 
Hizo ni Ibada za Matambiko, wanaposema wanaenda kuwaombea marehemu basi ujue wao ndo wanapeleka hoja kwa marehemu ili wasafishiwe mambo yao.

Ni inahusu na Ibada za Mizimu, ni somo pana sana kuhusu Mizimu, hii huwa inaabudiwa kizazi hadi kizazi. Mungu alieumba Mbingu na Nchi kamwe hasikilizi maombi ya Wafu na kupitia Biblia Mungu hajaruhusu maombi ya Wafu.
 
hizo ni Ibada za Matambiko, wanaposema wanaenda kuwaombea marehemu basi ujue wao ndo wanapeleka hoja kwa marehemu ili wasafishiwe mambo yao. Ni inahusu na Ibada za Mizimu, ni somo pana sana kuhusu Mizimu, hii huwa inaabudiwa kizazi hadi kizazi. Mungu alieumba Mbingu na Nchi kamwe hasikilizi maombi ya Wafu na kupitia Biblia Mungu hajaruhusu maombi ya Wafu.

Nimekusoma mkuu,nakua nafikili sana jambo hili na tena wafanyao haya ni wale wale tunaowaona wanaingia kwenye nyumba za ibada kila mala,mizimu ni kitu gani?

Na kama ni wafu nini kinachofanya kazi kwao juu walio hai, iweje babu wa babu alikua mzinzi, mlevi, mchawi na kila aina ya dhambi na mtu anajua lakini anaenda kumuomba makaburini amsaidie,napata shida hapa labda nielimishwe vyema
 
Someni dini mzifahamu vizuri, zote za asili na za ufunuo kisha mtajua kuwa waliokufa bado ni sehemu ya familia au jamii.

Vyema ndugu..tusaidie maandiko tusiojua,wapi katika biblia au wapi katika Msahafu ili tujilidhishe kua maombi ya wafu ni sahihi na yana maana kubwa katika maisha ya binadamu! Jibu tafadhari
 
OK. Tazama 2 Makabayo 12: 43-46

Duh! Mkuu sio makabayo ni Matayo labda kama ulimaanisha kitabu nisichokijua lakini kama ni Matayo 12:43 hapa Yesu alikua anazungumzia pepo wachafu. tena anazungumzia pepo saba walio waovu, sasa ukweli tunaoutafuta wa kuwaombea wafu na kupeleka shida zetu kwa wafu upo wapi katika mistali hii?

au umechukua kitabu kingine cha Mungu nisichokijua ndo maana nilitaka kusaidiwa kujua umaana wa kuwaombea wafu, bado hujanijibu nikakuelewa ndugu!
 
Duh! Mkuu sio makabayo ni Matayo labda kama ulimaanisha kitabu nisichokijua lakini kama ni Matayo 12:43 hapa Yesu alikua anazungumzia pepo wachafu.tena anazungumzia pepo saba walio waovu,sasa ukweli tunaoutafuta wa kuwaombea wafu na kupeleka shida zetu kwa wafu upo wapi katika mistali hii?au umechukua kitabu kingine cha Mungu nisichokijua ndo maana nilitaka kusaidiwa kujua umaana wa kuwaombea wafu,bado hujanijibu nikakuelewa ndugu!

Duh! Kumbe tatizo ni kubwa zaidi. Tafuta Biblia yenye vitabu 73 utakiona kitabu cha 2Makabayo.
 
Dah! Kumbe shida ni kubwa zaidi. Tafuta Biblia yenye vitabu 73 utakiona kitabu cha 2 Makabayo

Toa utetezi ndugu tueleweshane na tusije shitukia hapa wanakuja watu wa imani tofauti tofauti na uzi ukaonekana ni wa udini wakati mimi sijalenga huko,umaana wa kuombea wafu na kupeleka shida zetu ilihali tayali walisha lala,mahusiano ya mtu hai na mtu mfu ni yapi?tukisema nafsi yake ipo na inaongea na sisi au inatusaidia ni kivipi na kwa namna gani au niamini vipi?
 
Toa utetezi ndugu tueleweshane na tusije shitukia hapa wanakuja watu wa imani tofauti tofauti na uzi ukaonekana ni wa udini wakati mimi sijalenga huko,umaana wa kuombea wafu na kupeleka shida zetu ilihali tayali walisha lala,mahusiano ya mtu hai na mtu mfu ni yapi?tukisema nafsi yake ipo na inaongea na sisi au inatusaidia ni kivipi na kwa namna gani au niamini vipi?

Tafuta hilo andiko mkuu, majibu yapo hapo.
 
KWA NINI TUNASEMA IBADA ZA WAFU NI IBADA ZA KIPAGANI SEHEMU YA I
ANGALIZO:
a. Ninajua, tena nina uhakika sio wote ambao watakubaliana na mafundisho haya, wapo ambao ni kwa sababu hawaujui ukweli, wapo ambao ni kwa sababu tu wamekaririshwa na dini zao na wapo ambao ni mawakala ‘typically' wa Ibilisi kwa hiyo wako kwa kazi maalumu ya kumsaidia shetani kuipindisha kweli ya Neno la Mungu.

b. Jambo la pili nimegundua kwamba, kuna watu ambao wanajiita Wakristo na nafsi zao zimeshiba dini na madhehebu yao, wako tayari kuchinjwa kwa ajili ya kufia madhehebu yao, lakini kamwe hawajui kilichoandikwa kwenye Biblia, wao wamekaririshwa historian a heresies na viongozi wao wa madhehebu, kwa hiyo itikadi za dhehebu ndizo wanazodhani ni fundisho la Neno la Mungu, hawa ni wasumbufu, wanasimamia wasivyovijua, na watakwambia viko kwenye Biblia wakati ukweli ni kwamba havipo na havijawahi kuwepo.

Hapa ninakuja na somo kuhusu IBADA ZA WAFU. Ibada hizo ziko sehemu mbili, ya kwanza ni ile ya kuwaomba Watu (au watakatifu) waliokufa zamani nay a pili ni ile ya kuwaombea watu waliokufa. Kwa mujibu wa Neno la Mungu ibada zote hizi mbili hazikubaliki na neno la Mungu.
KUWAOMBEA WAFU

Mnamo tarehe 24 Januari 2013, Askofu mmoja wa dhehebu fulani hapa Dar es salaam aliwahi kusema kwamba "Kanisa linawaombea marehemu ili WATAKASWE, IKIWA WANAHITAJI KUTAKASWA kabla ya kupokelewa mbinguni wakati miili yao inapobaki ardhini ikingoja kurudi kwa Kristo na ufufuko wa wafu.

Hii ndiyo sababu kanisa linatolea sadaka ya misa kwa ajili ya marehemu. Pia kanisa linasali na kuwaombea marehemu kusudi wapate msaada wa kiroho na waamini walio bado hai wapate matumaini ya uzima ujao mbinguni"

KATIKA KAULI HII YA ASKOFU HUYU TUNAPATA YAFUATAYO;
1. Anakiri kwamba Kanisa huwa linawaombea wafu
2. Anakiri kwamba Kanisa huwa linatoa sadaka kwa ajili ya marehemu
ISAYA 34:16 inasema "Tafuteni katika kitabu cha Bwana mkasome….." Tutafute kwenye Kitabu cha Bwana yaani Biblia, tuone, Je, kuna mahali popote Biblia imewahi kuagiza kuombea wafu?

Na YEREMIA 6:16 inasema Bwana asema hivi, "Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katika njia hiyo"
Swali langu hapa ni hili, je, kuna tukio lolote la mtu aliyekufa kuwahi kuombewa kwenye Biblia? Twende tusimame katika njia kuu, tuone, tuulize habari za mapito (walioenenda) zamani, je, kuna mtu aliyewahi kufa kwenye Biblia akaombewa ili atakaswe?

Wako watu ambao hawatakosa majibu, hata hivyo sidhani kama majibu yao yatazidi mawili, ambayo ni, kwanza watasema wafu ambao Yesu aliwaombea na Dorcas aliyeombewa na Petro. Katika hili itakuwa ni matumizi mabaya ya muda kujadili suala hili la Yesu kuombea wafu kama Binti Yairo, Lazaro na wengine. Ukweli ni huu, hawa watu hawakuombewa ili dhambi zao zitakaswe, waliombewa ili warudi katika maisha haya (uhai).

Jibu la pili wanaweza kujibu hivi; watasema kuwa maagizo ya kuombea wafu na kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi za wafu yanapatikana kwenye VITABU VYA MAKABAYO; wako wanaodai kuwa vitabu hivi ni vitabu vya Biblia vilivyopotea.

Ukweli ambao wengi hawaujui na wataendelea kufichwa ni huu; vitabu hivi havikuwahi kupotea, isipokuwa vilikataliwa kwa sababu HAVIKUWA NA UVUVIO wa KIMUNGU zaidi ya hadithi na simulizi za kweli zilizowahi kutokea zamani. Simulizi hizi zinawahusu mashujaa wa zamani wa KIYAHUDI walioitwa MAKABAYO.

Katika Kitabu 2MAKABAYO 12:43-46: kwa kiingereza inasema hivi "And making a gathering, he [Judas] sent twelve thousand drachms of silver to Jerusalem for sacrifice to be offered for the sins of the dead, thinking well and religiously concerning the resurrection, (For if he had not hoped that they that were slain should rise again, it would have seemed superfluous and vain to pray for the dead,) And because he considered that they who had fallen asleep with godliness, had great grace laid up for them. It is therefore a holy and wholesome thought to pray for the dead, that they may be loosed from sins."

Nimeipata hii kwa Kiingereza, maana sina vitabu hivyo kwa Kiswahili.
Hapa ndipo baadhi ya watu wanachukulia fundisho la kuombea wafu kuwa ni sahihi; lakini sio kweli, kwa sababu kitabu hiki na vingine vine sio vitabu vya BIBLIA. Vilikataliwa kuingizwa katika orodha ya vitabu vya Biblia kwa sababu vilijaa hadithi kuliko uvuvio wa ROHO MTAKATIFU. Ziko sababu zaidi ya 21 za vitabu hivi kukataliwa, lakini kwa sababu sio somo lake, tuendelee na kuangalia kwa nini MISA ZA KUOMBEA WALIOKUFA NI IBADA ZA KIPAGANI.

WAEBRANIA 9:27 "Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu" Kumbe mtu anapokata roho tu anakutana na hukumu yake instantly, kuwaambia watu eti wamuombee na kumtolea marehemu sadaka ili atakaswe ni kuwaibia watu pesa zao na tena ni kuwaibia muda wao.

UFUNUO WA YOHANA 14:13 inasema "Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA TANGU SASA. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao"
Yesu anajua fika kwamba, hakuna nafasi ya mtu kutengeneza na Mungu baada ya kufa, baada kuachana na maisha haya ya duniani, ndio maana anatangaza kwenye andiko hilo, ili watu wajiandae wakiwa bado duniani, na ni angalizo kwa wale ambao wanangoja kuingia Mbinguni kwa lifti ya sala za marehemu.

JE, KUNA MAHALI PANAITWA PUGATORI?
Kuna dini zinafundisha kwamba kuna sehemu inaitwa purgatory au toharani ambapo mtu anapokufa huenda huko kwanza, na wakati ndugu, jamaa na marafiki wanamuombea huku duniani dhambi zake zinatakaswa kule aliko, na zikishatakaswa zote ndipo sasa anaweza kupokelewa na Mungu. Na ili kutakaswa kwake kuwe kwa haraka, kuna pesa ambayo inatakiwa kutolewa kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya marehemu.

NI AJABU SANA!!! kama mambo haya yangekuwa ya kweli sioni ni kwa nini Yesu alikuja kupoteza muda wake hapa duniani ahubiri Injili ya watu kutubu na kuacha dhambi wakiwa bado wako duniani. Sioni ni kwa nini basi aliacha heshima na Utukufu Mbinguni kama dhambi zingekuwa zinaondolewa kwa shilingi za Tanzania au dola za Kimarekani, Yen ya Japan na Faranga za Kifaransa.

Kwenye Biblia hakuna kitu kinaitwa PURGATORI, HAKUNAAAA!!!!!! Inasadikiwa kwamba Gregory ndiye aliyeanzisha uzushi huu na wengi wakaufuata baadae. Hii ni kama miradi ya watu kujipatia Pesa kutoka kwa masikini na matajiri. Na YESU aliliona na akaonya katika MATHAYO 23:14 akisema;

" [Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.]"
NDUGU ZANGU: Sadaka za misa za wafu haziwezi kutusaidia, ZABURI 49:6-7 inasema hivi "Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao; Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake"

WARUMI 6:23 inasema "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" Je, ni lini pesa ya mtu inaweza kutakasa dhambi ya mtu kama hakutakaswa na damu ya Yesu alipokuwa duniani?

NUSU HITIMISHO:
Misa za kuwaombea wafu, au arobaini, au hitima ya msiba, kama zinahusisha masuala ya kuombea watu waliokufa hizo ni ibada za KIPAGANI na sio ibada za Wakristo. Haijalishi zinafanywa na nani, ana wadhfa gani na ni maarufu kiasi gani. Ukweli ni kwamba sala hizi hazipo kwenye Maandiko Matakatifu.

MBINGUNI HAKUNA LIFTI: Yesu alikuja duniani ili tuhubiriwe, tutubu, maombi ya waliobaki duniani hayawezi kuwa lifti ya mimi kuingia Mbinguni kama nilikufa katika maisha ya dhambi.
Sadaka za kutoa kwa ajili ya kuwaombea marehemu ni batili, ni watu wasiojua maandiko ndio watakaoendelea kuliwa, maana tumesoma katika ZABURI 49:6-7 "Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao; Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake"
AKILI KICHWANI KWAKO,
SEHEMU YA PILI YA SOMO HILI ITAFUATA.

MLIMA WA MAKIMBILIO - BOKO Basiyaya (Basihaya??)
DAR ES SALAAM TANZANIA
 
Source:

KWA NINI TUNASEMA IBADA ZA WAFU NI IBADA ZA KIPAGANI SEHEMU YA I
ANGALIZO:
a. Ninajua, tena nina uhakika sio wote ambao watakubaliana na mafundisho haya, wapo ambao ni kwa sababu hawaujui ukweli, wapo ambao ni kwa sababu tu wamekaririshwa na dini zao na wapo ambao ni mawakala typically wa Ibilisi kwa hiyo wako kwa kazi maalumu ya kumsaidia shetani kuipindisha kweli ya Neno la Mungu.
b. Jambo la pili nimegundua kwamba, kuna watu ambao wanajiita Wakristo na nafsi zao zimeshiba dini na madhehebu yao, wako tayari kuchinjwa kwa ajili ya kufia madhehebu yao, lakini kamwe hawajui kilichoandikwa kwenye Biblia, wao wamekaririshwa historian a heresies na viongozi wao wa madhehebu, kwa hiyo itikadi za dhehebu ndizo wanazodhani ni fundisho la Neno la Mungu, hawa ni wasumbufu, wanasimamia wasivyovijua, na watakwambia viko kwenye Biblia wakati ukweli ni kwamba havipo na havijawahi kuwepo.
Hapa ninakuja na somo kuhusu IBADA ZA WAFU. Ibada hizo ziko sehemu mbili, ya kwanza ni ile ya kuwaomba Watu (au watakatifu) waliokufa zamani nay a pili ni ile ya kuwaombea watu waliokufa. Kwa mujibu wa Neno la Mungu ibada zote hizi mbili hazikubaliki na neno la Mungu.
KUWAOMBEA WAFU
Mnamo tarehe 24 Januari 2013, Askofu mmoja wa dhehebu fulani hapa Dar es salaam aliwahi kusema kwamba Kanisa linawaombea marehemu ili WATAKASWE, IKIWA WANAHITAJI KUTAKASWA kabla ya kupokelewa mbinguni wakati miili yao inapobaki ardhini ikingoja kurudi kwa Kristo na ufufuko wa wafu.
Hii ndiyo sababu kanisa linatolea sadaka ya misa kwa ajili ya marehemu. Pia kanisa linasali na kuwaombea marehemu kusudi wapate msaada wa kiroho na waamini walio bado hai wapate matumaini ya uzima ujao mbinguni
KATIKA KAULI HII YA ASKOFU HUYU TUNAPATA YAFUATAYO;
1. Anakiri kwamba Kanisa huwa linawaombea wafu
2. Anakiri kwamba Kanisa huwa linatoa sadaka kwa ajili ya marehemu
ISAYA 34:16 inasema Tafuteni katika kitabu cha Bwana mkasome.. Tutafute kwenye Kitabu cha Bwana yaani Biblia, tuone, Je, kuna mahali popote Biblia imewahi kuagiza kuombea wafu?
Na YEREMIA 6:16 inasema Bwana asema hivi, Simameni katika njia kuu, mkaone, mkaulize habari za mapito ya zamani, I wapi njia iliyo njema? Mkaende katika njia hiyo, nanyi mtajipatia raha katika nafsi zenu. Lakini walisema, Hatutaki kwenda katika njia hiyo
Swali langu hapa ni hili, je, kuna tukio lolote la mtu aliyekufa kuwahi kuombewa kwenye Biblia? Twende tusimame katika njia kuu, tuone, tuulize habari za mapito (walioenenda) zamani, je, kuna mtu aliyewahi kufa kwenye Biblia akaombewa ili atakaswe?
Wako watu ambao hawatakosa majibu, hata hivyo sidhani kama majibu yao yatazidi mawili, ambayo ni, kwanza watasema wafu ambao Yesu aliwaombea na Dorcas aliyeombewa na Petro. Katika hili itakuwa ni matumizi mabaya ya muda kujadili suala hili la Yesu kuombea wafu kama Binti Yairo, Lazaro na wengine. Ukweli ni huu, hawa watu hawakuombewa ili dhambi zao zitakaswe, waliombewa ili warudi katika maisha haya (uhai).
Jibu la pili wanaweza kujibu hivi; watasema kuwa maagizo ya kuombea wafu na kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi za wafu yanapatikana kwenye VITABU VYA MAKABAYO; wako wanaodai kuwa vitabu hivi ni vitabu vya Biblia vilivyopotea.
Ukweli ambao wengi hawaujui na wataendelea kufichwa ni huu; vitabu hivi havikuwahi kupotea, isipokuwa vilikataliwa kwa sababu HAVIKUWA NA UVUVIO wa KIMUNGU zaidi ya hadithi na simulizi za kweli zilizowahi kutokea zamani. Simulizi hizi zinawahusu mashujaa wa zamani wa KIYAHUDI walioitwa MAKABAYO.
Katika Kitabu 2MAKABAYO 12:43-46: kwa kiingereza inasema hivi "And making a gathering, he [Judas] sent twelve thousand drachms of silver to Jerusalem for sacrifice to be offered for the sins of the dead, thinking well and religiously concerning the resurrection, (For if he had not hoped that they that were slain should rise again, it would have seemed superfluous and vain to pray for the dead,) And because he considered that they who had fallen asleep with godliness, had great grace laid up for them. It is therefore a holy and wholesome thought to pray for the dead, that they may be loosed from sins."
Nimeipata hii kwa Kiingereza, maana sina vitabu hivyo kwa Kiswahili.
Hapa ndipo baadhi ya watu wanachukulia fundisho la kuombea wafu kuwa ni sahihi; lakini sio kweli, kwa sababu kitabu hiki na vingine vine sio vitabu vya BIBLIA. Vilikataliwa kuingizwa katika orodha ya vitabu vya Biblia kwa sababu vilijaa hadithi kuliko uvuvio wa ROHO MTAKATIFU. Ziko sababu zaidi ya 21 za vitabu hivi kukataliwa, lakini kwa sababu sio somo lake, tuendelee na kuangalia kwa nini MISA ZA KUOMBEA WALIOKUFA NI IBADA ZA KIPAGANI.
WAEBRANIA 9:27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu Kumbe mtu anapokata roho tu anakutana na hukumu yake instantly, kuwaambia watu eti wamuombee na kumtolea marehemu sadaka ili atakaswe ni kuwaibia watu pesa zao na tena ni kuwaibia muda wao.
UFUNUO WA YOHANA 14:13 inasema Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA TANGU SASA. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao
Yesu anajua fika kwamba, hakuna nafasi ya mtu kutengeneza na Mungu baada ya kufa, baada kuachana na maisha haya ya duniani, ndio maana anatangaza kwenye andiko hilo, ili watu wajiandae wakiwa bado duniani, na ni angalizo kwa wale ambao wanangoja kuingia Mbinguni kwa lifti ya sala za marehemu.
JE, KUNA MAHALI PANAITWA PUGATORI?
Kuna dini zinafundisha kwamba kuna sehemu inaitwa purgatory au toharani ambapo mtu anapokufa huenda huko kwanza, na wakati ndugu, jamaa na marafiki wanamuombea huku duniani dhambi zake zinatakaswa kule aliko, na zikishatakaswa zote ndipo sasa anaweza kupokelewa na Mungu. Na ili kutakaswa kwake kuwe kwa haraka, kuna pesa ambayo inatakiwa kutolewa kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya marehemu.
NI AJABU SANA!!! kama mambo haya yangekuwa ya kweli sioni ni kwa nini Yesu alikuja kupoteza muda wake hapa duniani ahubiri Injili ya watu kutubu na kuacha dhambi wakiwa bado wako duniani. Sioni ni kwa nini basi aliacha heshima na Utukufu Mbinguni kama dhambi zingekuwa zinaondolewa kwa shilingi za Tanzania au dola za Kimarekani, Yen ya Japan na Faranga za Kifaransa.
Kwenye Biblia hakuna kitu kinaitwa PURGATORI, HAKUNAAAA!!!!!! Inasadikiwa kwamba Gregory ndiye aliyeanzisha uzushi huu na wengi wakaufuata baadae. Hii ni kama miradi ya watu kujipatia Pesa kutoka kwa masikini na matajiri. Na YESU aliliona na akaonya katika MATHAYO 23:14 akisema;
[Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.]
NDUGU ZANGU: Sadaka za misa za wafu haziwezi kutusaidia, ZABURI 49:6-7 inasema hivi Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao; Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake
WARUMI 6:23 inasema Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu Je, ni lini pesa ya mtu inaweza kutakasa dhambi ya mtu kama hakutakaswa na damu ya Yesu alipokuwa duniani?
NUSU HITIMISHO:
Misa za kuwaombea wafu, au arobaini, au hitima ya msiba, kama zinahusisha masuala ya kuombea watu waliokufa hizo ni ibada za KIPAGANI na sio ibada za Wakristo. Haijalishi zinafanywa na nani, ana wadhfa gani na ni maarufu kiasi gani. Ukweli ni kwamba sala hizi hazipo kwenye Maandiko Matakatifu.
MBINGUNI HAKUNA LIFTI: Yesu alikuja duniani ili tuhubiriwe, tutubu, maombi ya waliobaki duniani hayawezi kuwa lifti ya mimi kuingia Mbinguni kama nilikufa katika maisha ya dhambi.
Sadaka za kutoa kwa ajili ya kuwaombea marehemu ni batili, ni watu wasiojua maandiko ndio watakaoendelea kuliwa, maana tumesoma katika ZABURI 49:6-7 Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao; Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake
AKILI KICHWANI KWAKO,
SEHEMU YA PILI YA SOMO HILI ITAFUATA.

MLIMA WA MAKIMBILIO - BOKO Basiyaya (Basihaya??)
DAR ES SALAAM TANZANIA

Aminia utingo...maelezo haya ndo nayotaka ili katika kila lipitalo nijifunze,sio tu mtu anasema nenda kasome mahala fulani,unatakiwa kutoa utetezi wa ujuacho kwa faida ya wote,nasubili somo lijalo
 
ni wazi ya kua MUNGU ni mwenye huruma na upendo na anasikiliza maombi yetu,nasi tumemjua MUNGU kwa kupitia vitabu vyake vitakatifu,kwa upande wetu tumemjua MUNGU kwa Biblia takatifu, na katika Biblia hio tumeambiwa kila kilichoandikwa kule kimetoka kwa MUNGU na kimeakikishwa na kinatufaa sisi katika mafundisho,

katika Biblia takatifu kitabu cha wamakabayo 12;38-45 ukisoma kwa makini na kwa minajili ya kuelewa hautakuwa na sababu ya kuwa na shaka kumuambea marehemu msamaha kwa MUNGU kwa yale alioyafanya yalio kinyume na mapenzi yake MUNGU kama alivyofanya huyo Yuda katika kitabuhicho cha wamakabayo, na kusauri G'taxi ukakisome kwa vyovyote vile kitafute katika Biblia ile iliokamilifu na sio ile yenye vitabu pungufu. kila la heri ndugu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom