Kwa nini vitu vingi vinapatikana Nairobi?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Kuanzia madawa, spea za magari, huduma mbambali mbali na bidhaa kadhaa wa kadhaa, huwa inasemwa vinapatikana Nairobi. Kama mtu umewahi kuuguliwa na Mgonjwa wako kufikia ngazi ya rufaa ya Kitaifa Muhimbili, lazima maelezo ya kununua dawa Nairobi ni lazima umewahi kuyasikia.

Hata vile vitu vinavyonunuliwa toka Arusha, mara nyingi ni kwa kuwa ni rahisi kuvileta Arusha toka Nairobi, Ni kwa nini Nairobi?
 
Siyo kweli kwamba kila kitu na itakuwa eneo na watu ulio nao karibu ndiyo wanye huruka ya kusema hivyo vitu vinapatikana Nairobi.
 
Mizigo mingi unayoiona nairobi kina story ndefu sana.
Vitu ni bei chee kwasababu ya wasomali, wasomali wanapata sana hela eg zile za waharamia, wengine wapo ulaya wanawatumia ndugu zao dola. Wasomali wanaagiza mali wanasema zinaenda somalia na somalia hakuna serekali hivyo mizigo yote inabaki kenya kistail na inakuwa haijalipiwa kodi. Bei inakuwa karibia na bure. Kuna sehemu panaitwa islii, hapo kuna kilakitu ambacho kipo ulaya.
 
Nchi imeathiriwa kwa kiasi kikubwa kwa taifa na chama tawala kukumbatia uchawi na ushirikina.
Mwenge ni ibada ya kishetani.
Mwenge ni laana inasababisha tulale kwa huzuni na tusifanikiwe.
Soma Isaya 50:11
 
kuhusu hili naomba tu ufungue uzi sababu ni mada pana sana ...ila naunga mkono
Nchi imeathiriwa kwa kiasi kikubwa kwa taifa na chama tawala kukumbatia uchawi na ushirikina.
Mwenge ni ibada ya kishetani.
Mwenge ni laana inasababisha tulale kwa huzuni na tusifanikiwe.
Soma Isaya 50:11

Sent using Jamii Forums mobile app
 
WaTanzania ni WAJAMAA wenzetu waKenya ni WAJASRIAMALI tofauti kubwa sana, Raslimali zoote tulizonazo tunawatuzia waKenya tu sisi ni koloni lao kiuchumi kila kizuri kilichopo TZ kinapatikana kenya na wao ndio wanakimiliki KIMATAIFA (AIBU KUBWA SANA INANIKERA SANA) na sasa hii miaka ya hivi karibuni ndio tumeua kabisa ujasriamali wetu uliokuwa ndio kwanza unachipukia..
 
Hata hizo mbalimbali ni wingi wa bidhaa zote.
 
Nguvu ya hela ndio inasababisha hivyo, uuzaji wa bidhaa nje ya nchi na hard currency kurudi ndani
Ingawa vitu vingi wanavyosafirisha wanaiba kwetu lakini potelea ya mbali ni uzembe wetu na ujinga wetu wenyewe ndio maana kahawa na kila kitu kitapita kwao na kuuza kwa jina lao

Na sisi tutabaki kuwatukana tu mpaka kiyama

Sent from my SM-G570F using Tapatalk
 
Nadhani wafanyabiashara wa kitanzania wapo discouraged na taratibu za kibiashara hapa nchini vitu kama kodi huwarudisha nyuma ku import Sababu nyingine kubwa wenzetu wa kenya katika sector ya viwanda wamepiga hatua wamejikita katika uzalishaji wa mafuta, nguo, vyakula,madawa na kadhalika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
naweza unga mkono hoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sababu kubwa ni ya kihistoria. Ni tofauti ya kihistoria kati ya Nairobi na Dar es Salaam na Pia Kampala, Bunjumbura na Kigali. Moja ni kwamba Waingereza walijua wanakaa Kenya milele kama Zimbabwe. Yaani walisettle...walilowea.
 
Sababu kubwa ni ya kihistoria. Ni tofauti ya kihistoria kati ya Nairobi na Dar es Salaam na Pia Kampala, Bunjumbura na Kigali. Moja ni kwamba Waingereza walijua wanakaa Kenya milele kama Zimbabwe. Yaani walisettle...walilowea.
Sababu ya pili ni athari ya vita vya kwanza vya dunia. Kenya haikupata athari kwa sababu Uingereza ilishinda vita na kuendelea na sera zake Kenya hasa Nairobi.
Sababu ya tatu ni historia baada ya kupata uhuru. Waliendelea na ubepari bila kuhubiri ujamaa au kutaifisha mali za matajiri kwa hiyo watu waliendelea kuwa na uwezo was kifedha.
Sababu ya NNE ni watu weupe kupendelea kuishi na kufanya biashara kubwa kubwa huko kutokana na sababu 1-3.
Tano ni uwezo na sera za uchumi kutobadilika badili
Sita ni purchasing power ya watu wake ni kubwa kutokana na sababu namba 5.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…