Kwa nini Waisraeli hawataji mapiramidi kabisa katika maandiko yao ya Agano la kale?

Kwa nini Waisraeli hawataji mapiramidi kabisa katika maandiko yao ya Agano la kale?

Kwa kipindi kirefu na hata mpaka leo hii watu wengi sana wanashangazwa na piramidi za kale za Misri. Kuna mjadala mkubwa sana jinsi zilivyojengwa, ni nani waliozijenga na walipata hiyo teknolojia ya ujenzi. Piramidi ni sehemu ya maajabu saba makubwa zaidi ya dunia.

Jambo la kushangaza ni kwamba Waisraeli katika maandiko yao ya agano la kale hawataji kabisa kuhusu mapiramidi.

Inawezekanaje Pyramids zikakosena katika maandiko ya watu waliokaa utumwani kwa mamia ya miaka huko Misri? Kwamba hilo jambo halikuwa kubwa, la kushangaza, kufikirisha na uzito kwao wa kutajwa katika vitabu vyao?! Kuna jambo haliko sawa.
1. Maandiko yalilenga imani na ukombozi wa Waisraeli, si historia ya Misri.

2. Piramidi zilijengwa kabla ya kipindi cha utumwa wa Waisraeli.

3. Hakuna ushahidi kwamba Waisraeli walikuwa wa mwanzo kujenga na piramidi. Inawezekana Walihusishwa tu katika kuongezea mengine. Ila yalishakuwepo.

4. Piramidi zilihusishwa na dini za kipagani zisizofaa kwa simulizi za Waisraeli.

5. Ukimya unaouongelea kuhusu piramidi unadhihirisha msisitizo wa kiimani, si kihistoria
 
Ndege, computer vs pyramid kipi kimetumia akili kubwa ? Au pyramid kwa kuwa ni mawe makubwa. Kama uwepo wa compyuta tusingewakuta waliounda tungeamini kuwa ni aliens. Sawa hivi tunaenda na AI si kitoto haya mambo mnayachukulia poa kwa kuwa vinaundwa mkishuhudia ila they are amazing technology which prove the human capability.
Imagine karne ijayo watu watakuwa wanaenda MARS kama waendavyo USA.
Kwa nini hamuamini uwezo wa binadamu ?
Kaa chini tafakari mambo ambayo binadamu anayafanya.
We are aliens who built pyramid.
NAKAZIA
 
1. Maandiko yalilenga imani na ukombozi wa Waisraeli, si historia ya Misri.

2. Piramidi zilijengwa kabla ya kipindi cha utumwa wa Waisraeli.

3. Hakuna ushahidi kwamba Waisraeli walikuwa wa mwanzo kujenga na piramidi. Inawezekana Walihusishwa tu katika kuongezea mengine. Ila yalishakuwepo.

4. Piramidi zilihusishwa na dini za kipagani zisizofaa kwa simulizi za Waisraeli.

5. Ukimya unaouongelea kuhusu piramidi unadhihirisha msisitizo wa kiimani, si kihistoria

NAKAZIA
 
Hizi stories za kusingizia Kuna viumbe tofauti na binadamu wakifanya ujenzi dunian, huo ni upuuzi ulioanzishwa na wazungu kwa malengo ya kuficha ukuu wa mtu mweusi ktk sayansi ya ujenzi, ukitaka kuwakamata na uongo wao jiulize mbona hao viumbe hawarudi nyakati hizi? Mbona hakuna ushahidi wa hao viumbe?, msidanganywe muda wa uongo ushapita
Siyo upuuzi , ushahidi upo duniani kote labda kama hufuatilii tu, lazima akili yako iwe free Ili uweze kuchanganua baadhi ya mambo. Haya niambie wewe huyo mtu mweusi unayesemea Yuko wapi Sasa hivi?, nakuuliza mtu mweusi Yuko wapi Sasa hivi?. Ina maana miaka yote hiyo Bado tu tunalaumu wazungu Kwa upumbavu wetu wenyewe.

Si ndio sisi tunahangaika huku duniani, haya niambie fantastic structures kama pyramids za kule Peru, mexico, USA, Antarctica, Tibet, Lebanon na sehemu nyingine duniani zilijengwa na mtu mweusi? Si ndo tunasema walikuwa primitive, haya sema pyramids za mexico nazo za mtu mweusi wakati zinafanana na Kwa kiasi kikubwa na za Egypt... Tukubali tu Kuna maarifa mengi yalipotea au yapo mahali ambayo yangetusaidia Leo tungekuwa mbali, lazima Kuna sayansi kubwa mahali ipo.
 
Back
Top Bottom