Kwa nini wajumbe wa CCM mabaraza ya Katiba wanang'ang'ania Serikali mbili?

Kwa nini wajumbe wa CCM mabaraza ya Katiba wanang'ang'ania Serikali mbili?

Ulimakafu

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2011
Posts
31,248
Reaction score
13,244
Wengi kama sio wote kati ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba Mpya toka CCM-kwa mujibu wa vyombo vya habari wanapingana na mapendekezo ya Tume ya Katiba ya Jaji Mstaafu J.S.Warioba kuwa Muundo wa Serikali Tatu na wanataka tuendelee na mbili kama ilivyo sasa kwa visingizio vya ajabu kama gharama,kwani sasa hawaoni jinsi serikali ya sasa inavyoendeshwa kwa gharama kubwa sana?
 
Kwa nini hawatoi mchanganuo wa hizo gharama utakavyo kuwa? wana generalize tu kuwa gharama kubwa, how?
Kuna kitu kinafichwa ndani ya hii issue ya serikali mbili, kwanini CCM hawataki kusikia chochote?
Kama kuna mwanachama yeyote wa CCM humu atupe mchanganuo wa hizo gharama za serikali tatu wanazoziogopa ili tufanye comparison?
 
Wengi kama sio wote kati ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba Mpya toka CCM-kwa mujibu wa vyombo vya habari wanapingana na mapendekezo ya Tume ya Katiba ya Jaji Mstaafu J.S.Warioba kuwa Muundo wa Serikali Tatu na wanataka tuendelee na mbili kama ilivyo sasa kwa visingizio vya ajabu kama gharama,kwani sasa hawaoni jinsi serikali ya sasa inavyoendeshwa kwa gharama kubwa sana?

Hayo ndiyo maelekezo waliyopewa na chama chao. Kwa ujumla wajumbe wa mabaraza wanaccm wamekwenda kuwakilisha maoni ya ccm na si maoni ya wananchi waliowachagua.

Lakini naamini kuwa wanaccm hawana nguvu ama uwezo wa kutuchagulia nini kiwemo na nini kisiwemo katika katiba mpya kwakuwa watanzania tuko wengi kuliko wanaccm. Kwahiyo tukiamua kwa umoja wetu na wingi wetu hakuna suala la ccm kutuamria mfumo wetu wa maisha katika katiba mpya.
 
Wamepata hizo nafasi ili kupinga serikali tatu. Huko Iringa (kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi) mtifuano umeshaanza. Njaa na kutojitambua ni sumu mbaya sana.Chama tawala kimekuwa chama pinzani.
 
MADAI YA SERIKALI 3 NI MATUNDA YA UDINI NA UARABU. Kwa kiasi kikubwa wale vinara wa kudai Serikali tatu wanasukumwa, hasa mambo makuu mawili:
1. Kwanza, ni Wazanzibari wenye msimamo mkali, na ambao wengi wao wanadhani wakipata Serikali ya Zanzibar yenye mamlaka kamili wataweza kupata manufaa kutoka nchi za kiarabu.
2. Pili, ni Watanganyika wakristo (wenye msimamo makali wenye udini)
na ambao wengi wao wanadhani kwa kutengana na Zanzibar watapata
nguvu zaidi ya kukamata nchi kwa ukamilifu na watanufaika zaidi
kama dini, hawa wanadhani hivi sasa Wazanzibar wanawaletea kiza.
Hapa kibaya zaidi kampeni hizi zinaendeshwa hata kwenye nyumba za ibada, na upande mwingine hata baadhi ya viongozi wa kisiasa na wanataaluma wakubwa wenye kutegemewa wameshanaswa kwenye mtego huu. Hii ndiyo hali halisi tuwe waangalifu kuzicheza karata hizi tusifuate mkumbo. Ukiangalia mfano, waliokuwa viongozi wa G.55 na Mchngaji ‘Mtaka kesi' n.k. walitaka pawepo na Serikali ya Tanganyika kwa mlengo wao wa udini kwa upande wa Bara, na kwa upande wa Zanzibar kuna wafuasi wa iliyokua chama cha Hizbu na hivi sasa Uamsho wana mlengo wa kiarabu. Hivyo zinahitajika juhudi za ziada kujinasua hapa la sivyo hawa wenye uchu wanauua Muungano wetu mzuri kwa sababu ya Udini na Uarabu.
 
Wengi kama sio wote kati ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba Mpya toka CCM-kwa mujibu wa vyombo vya habari wanapingana na mapendekezo ya Tume ya Katiba ya Jaji Mstaafu J.S.Warioba kuwa Muundo wa Serikali Tatu na wanataka tuendelee na mbili kama ilivyo sasa kwa visingizio vya ajabu kama gharama,kwani sasa hawaoni jinsi serikali ya sasa inavyoendeshwa kwa gharama kubwa sana?

kama wao unawashangaa na wewe itabidi wakushangae kwa nini unadai serikali tatu kila mtu anauhuru wa kutoa mawazo yake.
 
Wengi kama sio wote kati ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba Mpya toka CCM-kwa mujibu wa vyombo vya habari wanapingana na mapendekezo ya Tume ya Katiba ya Jaji Mstaafu J.S.Warioba kuwa Muundo wa Serikali Tatu na wanataka tuendelee na mbili kama ilivyo sasa kwa visingizio vya ajabu kama gharama,kwani sasa hawaoni jinsi serikali ya sasa inavyoendeshwa kwa gharama kubwa sana?
Kwa hiyo kwa vile sasa tunaendesha serikali kwa gharama unataka tuwe na serikali nyingine ili tuendeshe kwa gharama zaidi
 
Wamepata hizo nafasi ili kupinga serikali tatu. Huko Iringa (kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi) mtifuano umeshaanza. Njaa na kutojitambua ni sumu mbaya sana.Chama tawala kimekuwa chama pinzani.

mkuu sijui kama unafahamu maana ya kutoa maoni,yaonekana kichwa chako kimejaa ushabiki na umbea tu wala huna lolote.
 
Pia hawaungi mkono serikali tatu kwa vile hawaielewi. Huwezi kuacha mke ambaye umeishi naye muda mrefu mkiwa mmepitia katika aina tofauti za mafanikio na matatizo hadi mmefikia takriban miaka 49. Bado mwaka mmoja tusherehekee Jubilei ya miaka 50 ya ndoa yetu. Leo hii mnaachana kwa kutegemea mwenza ambaye hamjuani. Au umeishi na mke mmoja kwa muda mrefu. Baada ya kuona kuwa migogoro ya ndani imezidi, we unakimbilia kuongeza mke wa pili eti ndo unatatua kero za ndoa ya kwanza. Huo si utakuwa ulofa?
 
Yan dah!!!Una uhakika au ni hisia zako? Na ww pia usi ukawa ndo unatugawa.
 
Pia hawaungi mkono serikali tatu kwa vile hawaielewi. Huwezi kuacha mke ambaye umeishi naye muda mrefu mkiwa mmepitia katika aina tofauti za mafanikio na matatizo hadi mmefikia takriban miaka 49. Bado mwaka mmoja tusherehekee Jubilei ya miaka 50 ya ndoa yetu. Leo hii mnaachana kwa kutegemea mwenza ambaye hamjuani. Au umeishi na mke mmoja kwa muda mrefu. Baada ya kuona kuwa migogoro ya ndani imezidi, we unakimbilia kuongeza mke wa pili eti ndo unatatua kero za ndoa ya kwanza. Huo si utakuwa ulofa?

Yaani hapo mke ni mama ako ama vp?
 
hyo hata wafanye nn lazima serikali tatu iwepo kwa sababu sisi wananchi atutaki serikal mbili
 
Pia hawaungi mkono serikali tatu kwa vile hawaielewi. Huwezi kuacha mke ambaye umeishi naye muda mrefu mkiwa mmepitia katika aina tofauti za mafanikio na matatizo hadi mmefikia takriban miaka 49. Bado mwaka mmoja tusherehekee Jubilei ya miaka 50 ya ndoa yetu. Leo hii mnaachana kwa kutegemea mwenza ambaye hamjuani. Au umeishi na mke mmoja kwa muda mrefu. Baada ya kuona kuwa migogoro ya ndani imezidi, we unakimbilia kuongeza mke wa pili eti ndo unatatua kero za ndoa ya kwanza. Huo si utakuwa ulofa?
unadhan huo ni mfano mzuri kuutoa? Mind you, hizi ni nchi mbili sio watu wawili! Afu uko tayari kuwa contain watu wenye kutaka kujitenga? Utatumia mbinu gani? Usikaririshwe vitu siku za usoni unaweza kuja kujiona mjinga! Ikianza revolution struggle ya watu kujitenga utaopt nini? Vita? Mabomu? au? Tafakali na utumie akili saana, narudia usukaririshwe vitu!
 
Wengi kama sio wote kati ya wajumbe wa mabaraza ya Katiba Mpya toka CCM-kwa mujibu wa vyombo vya habari wanapingana na mapendekezo ya Tume ya Katiba ya Jaji Mstaafu J.S.Warioba kuwa Muundo wa Serikali Tatu na wanataka tuendelee na mbili kama ilivyo sasa kwa visingizio vya ajabu kama gharama,kwani sasa hawaoni jinsi serikali ya sasa inavyoendeshwa kwa gharama kubwa sana?

Mkuu, hivyo ndivyo walivyoelekezwa na wakubwa wao!! taifa likifika hapo ni hatari sana!! yaani wananchi hawatoi mawazo yao isipokuwa matakwa ya watu wachache kwenye uongozi wa juu wa chama tawala na hapa matokeo yake ni kwamba tutaandika katiba nyingine baada ya miaka michache sana, maana sioni Tanzania ya sasa ikiendelea na muungano wa nchi mbili!! Muundo huo ambao wanachama wa CCM wanautetea hata wao hawautaki isipokuwa wanyeje maana wakifanya kinyume vibarua vitaota nyasi!!!!
 
Back
Top Bottom