Kwa nini wanawake husalitiwa na mashoga zao kirahisi?


Labda kuna kitu kamzidi mkewe. Mwanaume huwa hamtokei hivihivi tu mwanamke. Mapenzi ya mwanaume yanaishi machoni, halafu mengine hufuata baadae.
 
mimi hiyo biashara sina nilishaifutia mbali siku nyingi maana unaweza hesabu hasara kuliko faida.

Another victim of ushoga. Pole bibie na huo uamuzi uloufanya ni mzuri zaidi, maana uimara wa meno ya fisi haujaribiwi kwa mifupa.
 
Wenyewe wanakwambia, '' kizuri kula na nduguyo, kibaya mtupie mbwa''.....Kwa hiyo lazima aonje anachofaidi shoga yake!
 

Hapo kwenye bluu hapo hapana. Busara unazozungumzia wewe ni zipi? Sisi wanaume ni wadhaifu zaidi ya wanawake linapokuja suala la ngono zembe. Yaani mwanamke akimtega mwaume, hata huyo mwanaume angekuwa jemedari wa jeshi lazima atainguia kingi tu. Busara na msisimko wa mwili vinahusiana vipi? Busara zake zitarudi akiwa kashamaliza kazi ya kuchakachua! Unafanya mchezo na uroda wewe eeeeh?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…