Kwa Propaganda za aina hii tutaizidi Korea Kaskazini haraka

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Tumeanza tabia ya kumsifia kiongozi mkuu wa nchi kwa kila jambo hata yale ya kawaida kabisa. Kule kwa Kim, Korea kaskazini hali ndio hii kwamba ni sifa tuu na sifa isipotolewa mtu anaweza kuadhibiwa hata kufikia adhabu ya kifo na wote wakaona kawaida.

Sasa hata mshahara ukiongezwa kidogo sifa ni nyingi kwa Rais lakini bei zikipanda haya ya nyanya lawama ni wengine hadi Urusi.

 
Hayo ni madhara ya mlengo wa Siasa za Ujamaa,

Siasa za Kidumu Chama Cha Mapinduzi, na ...


Zidumu fikira za Mwalimu... (Hazipingwi)

Alafu yote hayo yakaungwa na Uswahili.

N.B Uswahili ni uwasilishaji wa hoja kwa kujiamini bila utafiti thibitishi wa yanayoongelewa.

(Lacking Objectivity).

(mere words).

Mfano kusema "Kuupiga mwingi", ni Uswahili.
 
Kwani shida Iko wapi?
 
Na nyie 'magreat thinkers' hebu wakati mwingine jikiteni kwenye kujadili mambo ya maana na makubwa aisee......vikitu vingine vidogo vidogo hebu tuvipotezee kule! Isitoshe hizo t-shirt hazijaonekana mtaani, inawezekana ni mtu anacheza Tu na computer zake
 
Wa kusifia, waache wasifie, hii ni nchi huru
 
Simba na Yanga huwa ni mali ya chama na Serikali, zilianzishwa kwa malengo maalum..
 
Inawezekana meejesho toka kwa matajiri wa Royo tuwa.
 
Kuanza kulalamikia jambo dogo kama hili ni kujifananisha na Mutungi kama vile anakomolia bunge La Wananchi la mitandaoni la CHADEMA.

Hizo siasa tu na nyie pigeni siasa zenu.
 
Nimeanza kushtuka, inatumika nguvu nyingi kuitangaza hii asilimia 23.
Nia itakua ovu.
 
Wa kusifia, waache wasifie, hii ni nchi huru
Hata Korea Kaskazini ni nchi huru kimakaratasi lakini uhuru imeupoteza baada ya kumjengea Rais wao udikteta bila kujua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…