Geita haijaumbwa ili iwe mashimo baada ya kuchimba madini bali inastahili maendeleo kama mikoa mingine.
Nimeona niseme hili maana ujenzi wa kimaendeleo wa uwanja wa ndege na hospitali ya Rufaa unawanyima usingizi Chadema ambao wamewahi kuwa na wabunge makini kutoka kanda ya ziwa.
Geita na mikoa mingine iliyosahaulika ni lazima ikumbukwe sasa kama kahawa ilivyoinufaisha Kilimanjaro.
Kupanga ni kuchagua.
Maendeleo hayana vyama!
Mkuu, kitu ambacho hukijui ni kwamba zao la Kahawa lilikuwa linanufahisha Taifa kwa jumla - kahawa inauzwa Ulaya na fedha kwenda hazina - wakulima wa kahawa kupitia vyama vyao vya ushirika ndio walikubaliana kwamba wanapo uza kahawa kwenye vyama vya ushirika wanakatwa fedha kidogo kidogo kwa ajiri ya maendeleo ya Mikoa yao including kugharimia elimu za watoto wa wakulima maskini.
Wakulima wote wa cash crops nchini Tanzania wengeweza kabisa kuiga/jifunza kutoka kwenye mifano ya vyama vya ushirika vya Kilimanjaro na Kagera ili wajiletee maendeleo bila ya kutegemea saana Serikali, kwa bahati mbaya Serikali ilihamuru kuvunjwa kwa vyama vya ushirika kisiasa na kuwa telekeza wakulima katika lindi la maskini wa kutupwa kwa muda mrefu, juzi juzi hapa ndio nimeanza kuona Serikali inajitahidi kufufua vyama vya ushirika, lakini kasi ya ufufuaji bado ni ndogo sana.
Ninacho taka kusema hapa ni: Sio kweli kwamba mikoa iliyo kuwa inalima kahawa ndio ilikuwa inanufahika kimaendeleo, kinyume chake kama nilivyo sema tangu mwanzo kahawa ilikuwa inauzwa huko Ulaya kwenye minada ya Kahawa na fedha kwenda Serikalini, vyama vya Ushirika vinapewa fedha ndogo sana, siku wahi kuona Serikali ikisema itawapa kipa umbele cha maendeleo Mikoa inayo zalisha kahama kwa wingi, kama suala lingekuwa ni kwamba mikoa/miji yenye natural resources na cash crops nyingi ndio ipewe kipa umbele cha maendeleo mbona Shinyanga ingekuwa kama Ulaya kwa maneno mengine ndio ingekuwa inaongoza Nchini katika masuala ya maendeleo.
Tuwe wakweli hapa, Mikoa mingine inasahurika sana sana - mfano: Jaribu kutembelea mkoa wa Kagera, hivi sasa umerudi nyuma karibu kwa kila sekta,kusema kweli hali inatisha sana, mtu huwezi amini kama Mkoa huo ni part ya Tanzania, Serikali na wizara ya Kilimo wanazungumzia mazao mkakati sijui kilimo mkakati predominantely kwa ajili kanda ya kusini, kanda ya kati na Kigoma lakini sijawahi kusikia Wizara ya Kilimo au viongozi wa Mkoa wa Kagera wakizungumzia kuhusu kusambaza miche ya kisasa ya zao la michikichi Mkoani Kagera, wakati wazaliwa wa huko wanajua kwamba michikichi inastawi sana Mkoani, hipo mpaka migombani which means climate inakubali sana zao hilo.
Nakumbuka nilipo kuwa mdogo wakati wazazi wana lima mtama mwekundu kwa ajili ya kutengenezea pombe, sasa katika ukuuaji wa mtama palikuwa panajitokeza zao la ziada lenye maua mapana sana yanayo pendeza, sisi hatukujua hilo ni zao gani tulishia kuitana tu, jamani eeh (ija mulebe ebiua okwo byashemela) - yaani njoo muone maua yanavyo pendeza - kumbe zao lenyewe ni ALIZETI, ninacho taka kumaanisha hapa ni kwamba kumbe hata zao la Alizeti linakubali sana Mkoani Kagera - kwa nini mazao ya michikichi,Alizeti na kahawa hayapewi msisitizo kama misisitizo inayo wekwa kwenye Mikoa inayo lima Korosho na michikichi.