Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Kabisa mkuu 🤝
 
Fani zipi ndo uhakika mkuu?
Maana tuna walim,famasia huku mtaani pia sijawaona hapo?
Changamoto ziko kada zote lakini kwa Afya na Elimu kuna auheni kubwa ya kupata Ajira ya uhakika serikalini, japokuwa kunahitaji subira ya wastani wa miaka 3-5 kabla ya mfumo kumpa muhitimu ajira. Na hiyo ndio inaingia kwenye hiyo 10% ya wanaobahatika kupata ajira baada ya kuhitimu.

Changamoto kubwa nayo iko hapa.
1. Mshahara sio mkubwa (ni wastani)
2. Mazingira ya kuanzia ajira huwa ni magumu na mapya.
 
Ninaumia sana nikikumbuka jinsi nilivyokuwa nikiteseka usiku kucha ninasolve hesabu ngumu k.m Laplace transform, abstract algebra, topology, Fourier series, fluid mechanics,rigid body mechanics, advanced complex analysis, data structure, functional analysis e.t.c ili niweze kupata GPA nzuri na nikafanikiwa kuwa na 4.6 ambayo ni first class, lakini nimezunguka mpaka nikanyosha mikono huu ni mwaka wa 10. NINAUMIA SANA MOYONI MWANGU KWA NINI NILIPOTEZA MUDA KIASI HICHO KUHANGAIKIA KUSOMEA DEGREE HII YA .... AMBAYO NINATESEKA KIASI HIKI MTAANI. Hata hivyo Mungu ni mkuu siku Moja serikali watatukumbuka na tutapata ajira
 
Kufanya hizo kazi zinazofanywa na wasio na elimu sio vibaya hata kidogo.

Ila kwa kuwa ni 'msomi' namna atavyozifanya hizo kazi kutakuwa Kuna utofauti na wale wengine, Kama mfano ni Kilimo au biashara huyu 'msomi' akichanganya hiyo shughuli yake na maarifa aliyonayo tegemea matokeo mazuri mno na endelevu kuliko asiye na elimu kabisa.
 
Nina 12 yrs kitaa mkuu!
Acha kabisa!
Kwanza nilishaachana kabisa na mambo ya kuomba kazi mie
Tunapambana kivingine
Ni kweli inaumiza mno..

Lakini maadamu umeshatafuta 'plan B' hiyo elimu yako haijapotea bure, ufahamu wako umepanuka mno na uwezo wako wa kufikiri ni mzuri.

Namna unavyotekeleza hiyo 'plan B' hata kama haihusiani kabisa na elimu uliyosomea haiwezi kuwa sawa na yule asiyekuwa na elimu kabisa.

Hata 'maarifa' tu ya kitaa namna ya kuendesha shughuli ndogo ndogo ni elimu pia japo sio elimu rasmi.
 
20. Mineral processing engr
21. Bachelor of art with education
22. Fine art and design
23. Statistics
24.Mathematics
25.Physics
26. Civil engr
27. Chemistry
28. Agroeconomy
29. Biochemistry
30. French
31. Arabic
32.
33.
34.
Itoe 22 hadi 29
 
20. Mineral processing engr
21. Bachelor of art with education
22. Fine art and design
23. Statistics
24.Mathematics
25.Physics
26. Civil engr
27. Chemistry
28. Agroeconomy
29. Biochemistry
30. French
31. Arabic
32.
33.
34.
economics,agro economy,civil
ajira zipo mazee.

sema nini,ajira ni bahati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…