Kwa Simba hii tutegemee aibu huko Caf Super League

Kwa Simba hii tutegemee aibu huko Caf Super League

Ushauri wangu hii timu ingejikita zaidi kwenye kombe la Azam Federation
Tatizo Azam Federation Cup halikupi tiketi tena ya kucheza CAF maana michuano yote inafutwa inabaki Super League. Sasa utachagua nini ukipewa hivyo viwili, upewe tiketi ya CAF au ucheze michuano ya kutafuta tiketi ya CAF? 🤣 🤣 🤣
 
20230301_161343.jpg
 
Huo woga wenu ndiyo unaowafanya mcheze kombe la losers palipo na timu vibonde .Maana mnajua CAFCL kuna timu bora mtakula 6 hadi 8 kila mechi
 
Timu inayopigwa 3-0 nyumbani kwake, timu ambayo haina uwezo wa kubeba kombe lolote nchini mwake, timu isiyo na mfumo wa uchezaji kiwanjani zaidi ya kucheza mpira wa butua butua leo hii ishiriki ligi Moja na timu ambazo ni Mabingwa wa Afrika na pia ni mabingwa wa nchi zao, Je hamuoni taifa linaenda kufedheheshwa kwa aibu kubwa?

Yaani uwaweke Raja Casablanca, Mamelodi Sundowns na Simba kundi Moja unategemea nini hapo? Hawa kina Boco si wanaweza goma kurejea uwanjani kipindi cha pili?

Ushauri wangu hii timu ingejikita zaidi kwenye kombe la Azam Federation angalau inaweza kufika nusu fainal kuliko kwenda kubugizwa magoli na kuliaibisha taifa la Tanzania huko Superleague
Kwani super league inaanza lini
Hata TP Mazembe wamepigwa 2 - 0 nyumbani
 
Back
Top Bottom