Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Mtarban

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2015
Posts
3,858
Reaction score
5,101
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
 
Kama Msukuma Kuna muda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri?
 
Hivi hizo Sheria zinatungwa kwa lugha ya malkia alafu mbunge darasa la Saba hajui ht kutamka 1100 kwa kiswahili... Je hiyo Sheria ataijuaje zaidi tu ya kupitisha pasipo kupinga ili asiulizwe kasoro zilizomo...
 
Kama Msukuma Kuna mda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?????

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri????
Kama ni logic basi wote wenye logic tuwe wabunge, au sio. Tatizo mmewabinya watu kutoa maoni yao tofauti na kuwa mbunge.

Kina msukuma wangeweza kutoa maoni yao kwenye media mikutano nk..lakini sio kuwa wabunge. mbunge ni lazima awe msomi. Kingine hao kina Kabudi sio kwamba hawana uwezo bali wanaangalia chama hakitaki nini kwa hiyo na wao wanaonekana hawana tofauti na wasiosoma
 
Demokrasia Ni kuheshimu maamuzi ya wali wengi

Tanzania darasa la saba ndio walio wengi Huwezi wanyima haki Yao ya wao kuchagua mbunge miongoni mwao
Hatuangalii dunia tunaangalia walio wengi
 
Kama Msukuma Kuna mda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?????

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri????
Msukuma hajawahi kutoa Hoja yenye tija labda utaje kuwa amewahi kuishauri Serikali kitu gani cha muhimu.

Msukuma anachoweza Ni amejaliwa maneno ya kisanii ya kutoa mipasho kwa wapinzani kama ilivyo kwa Lusinde, basi
 
Kuona matatizo ya wananchi wako na kwenda kuwasemea bungeni hili halihitaji elimu kubwa, tatizo la wabunge darasa la saba wengi wao hoja zao huwa fupi, halafu wanazijazia na mipasho na umbea, hawa ndio mara nyingi hutumiwa na CCM kule bungeni kuzomea wapinzani, ni vyema wakafyekelewa mbali.
 
Demokrasia Ni kuheshimu maamuzi ya wali wengi

Tanzania darasa la saba ndio walio wengi Huwezi wanyima haki Yao ya wao kuchagua mbunge miongoni mwao
Hatuangalii dunia tunaangalia walio wengi

Ndiyo maana nimegusia kwa upande wa sheria ndo itamke kuwa candidate wa kiti Cha ubunge anatakiwa awe na elimu gani. Katiba ikishatamka huyo darasa la Saba anakosa sifa ya kuingia kwenye competition. Lakini pia hatuwezi kuangalia kuwa Ni tabaka lipi la watu wapo wengi Basi Lazima tupate kiongozi kutoka tabaka Hilo.
 
Msukuma hajawahi kutoa Hoja yenye tija labda utaje kuwa amewahi kuishauri Serikali kitu gani cha muhimu. Msukuma anachoweza Ni amejaliwa maneno ya kisanii ya kutoa mipasho kwa wapinzani kama ilivyo kwa Lusinde, basi
Amewahi sana! Moja ya hoja hizo ni kuruhusu kilimo cha bangi kwa ajili ya biashara na uchumi!!

Nakushauri fanya research duniani huko bangi inavyotumiwa kama dawa kwa wagonjwa mahispitalini na inavyoyaingizia mataifa fedha!!!
 
Demokrasia Ni kuheshimu maamuzi ya wali wengi

Tanzania darasa la saba ndio walio wengi Huwezi wanyima haki Yao ya wao kuchagua mbunge miongoni mwao
Hatuangalii dunia tunaangalia walio wengi
Sababu ndio mtaji wenu waende bungeni kupiga makofi
 
Sasa kama la Saba ana logic kuliko graduate kwanini tusiseme sasa hao lasaba wanaweza kuwa walimu, au Afisa rasilimali watu au hata mgavi au mtakwimu?

Hoja ya kiwango fulani cha Elimu ndio inatakiwa itangulie hizo hekima na busara zako. Ukiona zina umuhimu basi zipeleka kwenye familia yako au biashara zako

Ubunge ni kitu cha kushindania miongoni mwa watu wengi mambeleko haya hayasaiidii.
Na hivi kweli std VII anaweza kuchambua taarifa za kitaalamu za CAG, fiscal arenas kwa muono mpana kwani critical and analysis yake ni ndogo ukilinganisha na nafasi anayoitaka.

Kama form four tu kwenye uaskali wanaanza kuonekana wanapwaya ile mbaya ije kuwa std VII tena ile kazi wanatumwa tu lakini uwezo hata wa kuitekeleza maamuzi unaanza kuwa mgumu kwasababu ya shule aliyosoma.

Hawa ilitakiwa waondolewe hata kwenye udiwani sema Chama chenye hakipo serious
 
Hii ishu yaweza sound rahisi ila ni complicated kidogo. Demokrasia inasema kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Binafsi naona hata kuweka standards za elimu ni kumnyima mtu haki yake ya kidemokrasia.

Kama unaweka standards za mpigiwa kura tufanye ya kwamba na mtu yeyote aliyeishia la saba asipige kura pia. Maembe alisema "Pakiliwa kwa mwali na pa kungwi paliwe"
 
Ndiyo maana nimegusia kwa upande wa sheria ndo itamke kuwa candidate wa kiti Cha ubunge anatakiwa awe na elimu gani. Katiba ikishatamka huyo darasa la Saba anakosa sifa ya kuingia kwenye competition. Lakini pia hatuwezi kuangalia kuwa Ni tabaka lipi la watu wapo wengi Basi Lazima tupate kiongozi kutoka tabaka Hilo.
Itakuwa katiba ya kijinga mtu na inayokiuka haki za binadamu mtu ana haki ya kupiga kura nakupigiwa kura pia akitaka .Huwezi tengeneza katiba inayomnyima mtu haki zote mbili
 
Basi ingekuwa wasomi Ni wajinga kuliko wasiosoma Hakuna nchi ingekuwa inahangaika na Elimu bali wangejikita na mambo mengine tu. Ki ufupi wewe Ni mjinga ambaye haupaswi hata kujibiwa.
Nimesema kwa Tanzania. Kwa Tanzania wasomi ni wajinga kuliko watu wasiosoma. Mie kila nikimwangalia na kumsikiliza Kabudi huwa najiuliza hivi nisome PhD ili iweje sasa kama kabudi ana PhD na kajaa ujinga vile????
 
Sasa kama la Saba ana logic kuliko graduate kwanini tusiseme sasa hao lasaba wanaweza kuwa walimu, au Afisa rasilimali watu au hata mgavi au mtakwimu?

Hoja ya kiwango fulani cha Elimu ndio inatakiwa itangulie hizo hekima na busara zako. Ukiona zina umuhimu basi zipeleka kwenye familia yako au biashara zako

Ubunge ni kitu cha kushindania miongoni mwa watu wengi mambeleko haya hayasaiidii.
Na hivi kweli std VII anaweza kuchambua taarifa za kitaalamu za CAG, fiscal arenas kwa muono mpana kwani critical and analysis yake ni ndogo ukilinganisha na nafasi anayoitaka.

Kama form four tu kwenye uaskali wanaanza kuonekana wanapwaya ile mbaya ije kuwa std VII tena ile kazi wanatumwa tu lakini uwezo hata wa kuitekeleza maamuzi unaanza kuwa mgumu kwasababu ya shule aliyosoma.

Hawa ilitakiwa waondolewe hata kwenye udiwani sema Chama chenye hakipo serious

Hapo ndipo kiti Cha ubunge kilipodharaulika. Darasa la Saba anaweza kuwa Mbunge ila hawezi kuwa na vigezo vya kushika nafasi ndogo Sana za uongozi kwenye jamii
 
Nimesema kwa Tanzania. Kwa Tanzania wasomi ni wajinga kuliko watu wasiosoma. Mie kila nikimwangalia na kumsikiliza Kabudi huwa najiuliza hivi nisome PhD ili iweje sasa kama kabudi ana PhD na kajaa ujinga vile????
Ukimwangalia Kabudi Kama mwanasiasa na Tena mteule wa Rais unaweza kudharau usomi wake ika ukimwangalia Kabudi Kama Kama mtu Ni ya Siasa au uteule ndo utakapoweza kumuelewa. Hivyo sidhani Kama unaweza kudharau PHD yake. Jaribu kumfuatilia akiwa bado Yuko nje ya Siasa za uteule ndo utakapopata kumjuwa Kabudi halisi
 
Back
Top Bottom