Kwa Tukio lililomtokea Mama yangu 2009, Nimetokea kuuheshimu sana Ukristo na Wakristo wote

Kwa Tukio lililomtokea Mama yangu 2009, Nimetokea kuuheshimu sana Ukristo na Wakristo wote

Dini yangu mimi Ni Muislam,ila wazazi wangu Baba ni Muislam na mama ni Mkristo , walifahamiana mwaka 1989 kipindi wanafanya kazi serikalini wakapendana na 1992 wakaoana kwa ndoa ya kiserikali na maisha yakaendelea japo malezi yetu Mzee alihakikisha tunaifuata dini yake watoto wote tumebase kwenye Uislam tokea watoto hadi sasa

TUKIO LENYEWE LILIVYOTOKEA 2009

Ilikuwa ni mwezi wa 7 kipindi hicho nakumbuka ndio nilikuwa namaliza Olevel , Mama ndio alikuwa anajifungua mdogo wetu wa mwisho so katika utaratibu wa kujifungua akapangiwa kujifungua kwa (OP), Alijifungua Hospitali kubwa ya Serikali ipo hapo kibaha mbele ya Mailimoja,Baada ya kujifungua kwa Op akawa hospitali kwa siku chache then akaruhusiwa kwenda nyumbani hivyo akaaza kuuguza Kidonda kile

Kidonda baada ya siku kadhaa kikafunga vizuri ila akawa anapata maumivu makali sana sehem ya ndani alipofanyiwa upasuaji yaani kukawa na kitu kama kinamchoma ndani kwa ndani usiku halali analia tu, hivyo kukawa na safari za kurudi pale hospitali kwa uchunguzi, wakawa wanampa dawa tu ila hawakushtukia nini kinamsumbua,

Mwezi wa 9 2009 nakumbuka ilikuwa ni usiku mama akawa analia maumivu makali akawa anapiga kelele usiku hadi majirani walishtuka ikabidi akimbizwe hospitali nyingine ya Private wakampa kitanda na huduma zote za kwanza ili Asubuhi wampige Xray wachunguze sehem aliyofanyiwa upasuaji ndani kuna nini hadi anapata yale maumivu

kulivyokucha akapigwa Xray, wale madokta wanakuja kuisoma ile Xray wakakuta ndani kuna mkasi ulisahaulika, vile vimkasi vya kufanya upasuaji wale majamaa walionfanyia upasuaji kipindi anajifungua waliusahau ndani alafu wakashona na ndio uliokuwa unamchoma ndani kwa ndani, cha kwanza wale madocta pale kwnye ile Hospitali walishtuka sana na wakaogopa kufanya upasuaji kuuondoa ule mkasi wakashauri mzee aende chap pale kwenye ile Hospitali ya Gov kibaha akawape taarifa wale waliomhudumia bi mkubwa walichofikifanya ili waangalie watafanya nn kuokoa maisha yake

Mzee akarudi pale na mama, ikabidi wampige Xray nyingine wahakikishe wakakuta kweli ndanii kuka mkasi mdogo wameusahau so ikabidi ufanyike upasuaji mwingine kuuondoa ule mkasi tena.

Ulivyofanyika upasuaji mwingine balaa ndio kikaanzia hapo mama baada ya kuruhusiwa kurudi nyumbani kile kidonda kikawa hakiponi baada ya mwezi mmoja kikaanza kutoa harufu kali sana yaani ukiingia chumba cha mama utasema kuna kitu kimeoza or mtu kaanza kuoza akiwa mzima mzima hali ilianza kutisha mzee akahangaka hadi alifilisika, Ikafika kipindi ukichungulia lile donda hadi viungo vya ndani unaviona hali likuwa tete.

Wakawa wakiwatafuta wale madokta waliomfanyia upasuaji wanamkimbia inshort walishajua kifuatacho kwa mama ni kifo kila wakipigiwa simu wakawa wanakimbia, Mzee akienda pale hospitali kuomba msaada wanamkwepa, Mama ikafika kipindi tumboni pale akawa anafungwa kibandeji kupunguza harufu kali maana kidonda kilishaoza kikawa kinatoa usaa na uchafu matumaini yakawa yamepotea

Ilipofika mwezi wa 11 Mama akaaza kuacha kitu kama wosia kwa mzee alishajua anaenda kufa, Mama akawa anamwambia mzee kuwa mimi najua naondoka ila naomba uwaangalie sana hawa watoto, uendelee kuwalea vizuri wasiteseke, Mzee akawa anachanganyikiwa zaidi, ilifika kipindi mzee akawa haendi kazini anashinda na mama tu analia, badhi ya watu walishadhani huenda yupo kwenye saa zake za mwisho watu wakawa wanasubiri Taarifa tu maana hata kumsogelea alikuwa anatoa harufu kali

Ilipofika mwezi wa 12 nakumbuka ilikuwa ni Tarehe 20/12/2009.. Hii siku kulikuwa kuna mkutano wa Injili pale viwanja vya Biafra kinondoni kuna mtumishi ambae huwa anafanya semina sehem nyingi Tanzania hii siku ndio alikuwa anasemina na maombezi pale Biafra, kabla ya hii tarehe nakumbuka mama alimwambia mzee ampeleke kipindi hicho mzee akawa kama hataki ila ikabidi anyooshe mikono juu ilipofika hiyo siku ikabidi wamwandae vizuri then tukampeleka

Baada ya semina ndefu ikafuata kipindi cha maombezi, yule Mwalimu akasema namnukuu " naambiwa na roho mtakatifu kuwa yupo mama mmoja katikati yetu anasumbuliwa na kidonda na hakiponi kama yupo apite hapa mbele" akayarudia hayo maneno kama mara 2, Ikabidi mama anyooshe mkono juu maana hata kutembea kupanda jukwaani hakuweza

Ikabidi yule mtumishi amsogelee karibu kisha akamwambia asimame,akaaza kuomba akimshika kichwani, kati kati ya maombezi kwa mshangao lile libandeji alilokuwa amefungwa Mama Tumboni kuzuia harufu lilkakatika pale pale kimiujiza kisha likadondoka chini,maana alikuwa amevaa kitu kama joho skuizi wanayaita madela, baada ya hapo akajihisi mwili mzima kama umepatwa na baridi kali kisha akakaa akawa kama amepoteza faham

Kuja kushtuka akakuta watu wanampepea baada ya hapo yule mtumishi akamwambia mama Imani yako itakuponya Amin, baada ya hapo tukamrudisha Mama nyumbani

Mshangao ukaanza wiki iliyofuata lile Donda pale tumboni likaanza kukauka kimaajabu, ile harufu ikakata kidonda kikaanza kufunga chenyewe kila mtu akawa anashangaa kinachoendelea, ilipofika tarehe 15 mwezi wa 1 mwaka 2010 kile kidonda kilikuwa kimeshafunga kabisa kimaajabu na hakuna mtu ambae aliamini kuwa atapona hadi leo wale madokta walishikwa na mshangao kuwa aliwezaje kupona lakini sisi tunasema ni Mungu tu

Kwa sasa Mama ni mzima wa afya kabisa na yule mtoto aliejifungua now ana afya njema na sasa yupo Form one anapiga kitabu akiwa na Afya Njema kabisa, nafurahia sasa bado naita Mama, Alhamdulilah[emoji120][emoji120]

Na baadhi ya Ndugu ambao walishaanza kudhani kuwa mama anaenda kufa naowajua kuna baadhi kama 6 tushawazika ila mama leo ana afya tele

Kunazia hapo kwa haya mambo yaliyotokea yalibadili sana maisha yangu na misimamo yangu kuhusu wakristo japo sometime unakuta unamezeshwa sumu mara wale Makafiri, niskiaga mtu anamuita Mkristo kafiri huwa namskitikia sana

Miujiza ya hawa wanaoitwa Makafiri ndio leo inanifanya naita mama, mama yangu kaponyeka kimaajabu

Nikikuta sehem mkristo au kanisa huwa naheshimu sana yaani kitu huwezi kiheshimu hadi yakukute ila kwa hili kila mtu abaki na imani yake ila kila mmoja aheshimu imani ya mwenzie yapo mambo ya kweli kwenye hizi imani mm ni shahidi,

Ukimtukana mtu kafiri unatakiwa ujue kuwa hakuna mwislam aliyekufa akarudi kukupa taarifa kuwa huko peponi wapo watu wa aina gani ukishalijua hilo basi heshimu sana imani za wengine Maisha baada ya kifo ni Siri kubwa na mitihani ya maisha ndio inatufanya tujue ukweli hukusu hzi Dini

Asanteni..
Huyo mtumishi atakuwa ni Mwl Christopher Mwakasege.

Nashukuru kwa ushuhuda🙏🙏🙏

Mungu wetu ni wa upendo. Anawapenda wote na anatamani kujifunua kwa kila kiumbe.

Anawapenda wote, wewe ukiwemo. Anakufahamu kwa jina lako na anakupenda vilivyo.

Nashukuru sana kwa ushuhuda🙏🙏🙏
 
Anyway nimeingia Jukwaa linaloruhusu kuandika uwongo. Samahani natoka.

Hakuna mtu mwenye akili yake anaeeza kuandika maradhi ya mama yake hata kama anatumia fake ID
Hajaandika maradhi, amemtumkuza Mungu kwa kile alichokifanya.
Huko mahospitalini Mungu pia anatenda kazi kupitia hao madaktari na manesi, ama unazani ni madaktari ndio huponya? Tafakari maneno/fikra zako kabla hujazitoa hadharani kama Ibrahim ni baba wa imani nacc wato tu watoto wake kwanini uchukie imani ya nduguyo? Je hujioni kama wewe ndio unamatatizo?
Tafakari njia zako matatizo yanatabia ya kukupeleka sehem ambazo hujawahi kuzania.
AMANI IWE NAWE.
Madaktari wana falsafa yao maarufu: "Sisi tunatibu, Mungu anaponya"
 
Uponyaji wa Imani unafanyika Kwa Imani. Sasa anaendaji Ocean road Kwa wagonjwa ambao hawajawa na Imani hiyo????
Hata Yesu alishindwa kuwaponya watu wa nyumbani kwao Nazareth kwa sababu ya kutokuamini kwao. Alitamani kuwafanyia miujuza mikubwa lakini wakamfunga breki kwa kutokuamini kwao.
 
Mimi ni Mkristu tena Mkatoliki, dini ilikoanzia yapata miaka 2000 iliyopita lakini huniingizi kwenye huo upuuzi wenu wa kudanganya eti mnaponya watu.

Nyie walokole mumekuwa frustrated halafu manakutana na watoto wa mjini kutoka Tukuyu akina Mwamposa, Lusekelo na Mwakasege. Lazima mudanganyike sana na mpagawe
Mbona na Wakatoliki nao siku hizi wanombea wagonjwa?

Unawafahamu wana Karismstik wa Katoliki?
1. Wanakemea mapepo!
2. Wanawaombea wagonjwa!
 
Miujiza ya Mwenyezi Mungu ipo na inafanyika kila iitwapo leo, kikubwa ni kuamini kwa moyo mmoja. Nb Mungu azidi kumtia nguvu mtumishi wake. Mwl. Christopher Mwakasege
Amina!

Kupitia huduma ya Mwl Mwakasege watu wengi sana mimi nikiwemo wamesaidika sana.
 
Umesimulia tukio vizuri mno kiasi Cha kuinua hata Imani inayolega lega utafikiri nilikuwa naona Kila unachoeleza
Mungu aendelee kumtunza mama yetu
 
Back
Top Bottom