Kwa uelewa wangu, duniani kote Vyama vya Siasa huwa na wasanii maalum kutumbuiza wakati wa kampeni

Kwa uelewa wangu, duniani kote Vyama vya Siasa huwa na wasanii maalum kutumbuiza wakati wa kampeni

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Nimejaribu kuangalia ile mobilization iliyofanywa na wasanii kule nchini Nigeria kina Davido na wenzake wakiandamana kuomba kile kikosi maalum cha Polisi kinachotesa Raia kivunjwe na hatimaye mamlaka zimekivunja. Huku Bongo Wasanii wa kizazi kipya kina Diamond na kundi lake wanakata mauno kwenye kampeni za CCM wanaomba kura. Yaani hopeless kabisa na aibu.

Kwa uelewa wangu mimi ni kwamba duniani kote vyama vya siasa huwa na wasanii maalum kutumbuiza wakati wa kampeni badala ya kutumia wasanii maarufu ambao wanajua hawawezi kuitikia maombi yao kwa kuogopa kugawa mashabiki. Hivi leo unafikiri mwanachama Kindakindaki wa CHADEMA au ACT atampenda Alli Kiba au Diamond Platnumz?

Ukiona hivi ujue ni umaskini ndiyo umekithiri, msanii anayejitambua mwenye pesa zake hawezi kufanya kazi za siasa kwanza hana muda huo labda aamue kugombea yeye. Tuna wasanii 90% darasa la saba na form four failures ambao hawana skills za kuwafikisha mbali kusimama wenyewe. Maarifa ya kufikiria kuwa siasa ni tukio la Msimu hawana. Mtu akipewa mkono na Rais kesho kichwa kimevimba.

Diamond angekuwa na pesa asingehangaika na kampeni za CCM kulipwa pesa za madafu. Wengine wanakopwa na wapo wanaolipwa kiduchu sana.
 
Hawa wasanii nao ni wa kusamehe tu. Inasemekana wametishwa alafu hata posho wanalipwa kwa kusua sua kweli na hakuna anayeweza kufungua mdomo kulalamika.

Sasa ngoja uone uchaguzi uishe na itokee magufuli kashindwa. Wasanii watafunguka mengi.
 
Hawa wasanii nao ni wa kusamehe tu. Inasemekana wametishwa alafu hata posho wanalipwa kwa kusua sua kweli na hakuna anayeweza kufungua mdomo kulalamika.

Sasa ngoja uone uchaguzi uishe na itokee magufuli kashindwa. Wasanii watafunguka mengi.
Utakuwa unaota ww
 
Yule wa ccm ajaribu kufanya mikutano bila wasanii ili ajipime Kama wanafata wasanii au wanafata sera
 
fuatilia marekani kina jay z, rihanna,69, omarion,Rick loss, akon, Ashanti, Wayne, DJ khàleed etc..wanapiga kampeni za Republican daily
 
..Wasanii wetu bado wachanga.

..Hivi unafikiria Donald Trump au Joe Biden wanaweza kumtumikisha Jay-Z kama Jiwe anavyowatumikisha wasanii wa hapa bongo?

..Yaani Jay-Z atunge wimbo maalum kwa Trump, au Biden, na asifanye kazi yoyote zaidi ya kumnengulia kwa miezi mitatu ya kampeni?!!
 
..Wasanii wetu bado wachanga.

..Hivi unafikiria Donald Trump au Joe Biden wanaweza kumtumikisha Jay-Z kama Jiwe anavyowatumikisha wasanii wa hapa bongo?

..Yaani Jay-Z atunge wimbo maalum kwa Trump, au Biden, na asifanye kazi yoyote zaidi ya kumnengulia kwa miezi mitatu ya kampeni?!!
Wacha kabisa, tofauti iliyopo kwa hawa watu ni mbingu na ardhi, yani ni sawa na black & white.
 
Na ndiyo maana kazi zao hazivuki mipaka hasa hawa bongo movie ndiyo Utopolo kabisaaaaa
 
Wacha kabisa, tofauti iliyopo kwa hawa watu ni mbingu na ardhi, yani ni sawa na black & white.

..tuwape muda.

..utafika wakati wanasiasa watakuwa wanawaheshimu na kuwanyenyekea wasanii wetu.

..ila siyo wasanii hawa wa kizazi hiki, may be miaka 15 ijayo.
 
Back
Top Bottom