Kwa ujinga huu, sitamuamini mtu hasa vijana

Tatizo atakamatwa akiwa hana kitu au kama ni mwerevu huwezi kumpata
Ni swala la muda tu kiongozi niamini mimi. Na hivi picha yake ipo humu ni swala la muda tu. balibabambonahi ungeweka RB namba hapa pamoja na jina kamili la huyu jamaa ili akionekana pahali mtu aweze kutoa taarifa kwa kuitaja na hiyo RB namba yako.

Pia kama alikuambia mkoa anaotokea au hata stori yoyote ya alipotokea au inayomhusu ziweke hapa kwa kutengeneza profile yake hii itasaidia zaidi maana pengine humu utakutana na waliosoma naye walioishi mtaa mmoja na hata ndugu zake pia. Dunia ni ndogo sana hii. Weka hadi namba za.simu alizokuwa akitumia.

Kamilosha taarifa zote.kumuhusu usiweke nusu nusu kama ulivyoweka hapa.
 
Pole sana mkuu, huo ndio mtindo wa dunia, so umetumika kama kafara ili wengine tupone (kuibiwa kwako wewe kunafanya na sisi wengine tuwe makini kwenye mitego ya aina hiyo)... Hopefully utampata ila kwa muonekano wa huyo kijana hata ukimpata sijui kama atakua na chakukupa lakini hakikisha unakua ulimwengu wake(mfunze).
 
bila shaka kopi ya kitambulisho cha nida unayo? mfuatilie mfundishe abadu siku hizi watu hawaibi kiboya ivoo!?
 
Wakati natafuta kazi nilikutana sana na hii changamoto ya kutoaminika. Vijana tunalilia sana connection lakini kiukweli hatuaminiki.

Nilipopata mtu wa kunishika mkono nilipiga kazi kwa juhudi na uaminifu mpaka siku ambayo namwambia boss naacha kazi ili nipige mishe zangu binafsi aliniambia kama naweza kum-recommend kijana muaminifu kama mimi ninayejuana nae ili azibe nafasi

Kijana yoyote ukishikwa mkono lazima ujue wewe ni balozi wa vijana wenzako jobless ambao wapo mtaani. Uchapa kazi wako, uaminifu wako na ubunifu wako ndio utakaotengeneza taswira ya wenzako ambao bado hawajapata nafasi kama wewe
 
Sema watu mnaamini haraka sana anyway ni vema umejifunza na umefundisha wengine bila we tungejuaje!?
 
RB nitaiweka.Anatokea Arusha.
 
RB nitaiweka.Anatokea Arusha.
sawa Mkuu, sasa weka taarifa vizuri labda nikusaidie kukupa format hapa chini:-

Jina kamili: _________
Namba ya simu aliyotumia: ______
Mahali alipotokea: ____________

Elezea kwa kifupi stori yoyote mliyopiga pamoja kuhusu yeye mfano, shule aliposoma, mtaa alioishi Arusha n.k

Ambatanisha RB Na.: __________
Kosa lililoripotiwa: ____________
Namba yako ya simu: _________

Eleza taarifa itolewe wapi endapo ataonekana popote


Ambatanisha picha yake/zake
Eleza ulimuajiri mtaa upi: _____
Eleza alianza lini kazi: ________
Eleza tukio limetokea lini: _____

Mkuu balibabambonahi jaribu kuishi na huu mfumo hapo juu
 
Yaani umekutana na mtu huku kwenye mtaa wa JF unamwamini kiasi hicho? Je, ulikuwa unamfahamu ndugu yake yeyote? Je, nani alimdhamini kwako? Au ulimwajiri kienyeji tu?
Huyo alishaanza kuonesha dalili za ukibaka tangu awali ulipomtumia nusu nauli. Kwanini pia alifuta picha alizotuma? Hapo alikuwa anaficha ushahidi.
Hata hivyo pole kwa yote yaliyokupata.
 
Hakika kaka wewe ndio mwenye kosa

Hakika nakuambia ndugu,

Kuna matapeli humu, kuna makahaba humu, kuna vibaka humu,

HOW COULD YOU JUST TRUST SOMEONE SO EASILY??
Moyo wa upendo umemghalim, ukweli hum wamejaa hao uliowaorodhesha hapo juu.. Kuna kipindi niliweka Uzi kuomba ufafanuzi namna bonus account ya nmb inavyofanya kazi nikidepost mil 15.

Kuna mdau akakomet kwamba kuweka pesa yote fixed ukisubiri laki nne kwa miezi mitatu ni uvivu wa kufikiri akaniomba aje inbox tuongee mchongo! Nikamwambia njooo akaja bhn!

Akashusha gazet akisema hii biashara tunayoenda kufanya yeye nimmegee mil 1 tu atakuwa anawasilisha lak mbili kwa siku kwamba hata hivyo hiyo milion sitamtumia yeye nitakuwa nayo Mimi atanielekeza tu jinsi biashara inavyoconectiwa,,, hapo Mimi namchora tu akaniomba namba ya wtsap kwa maongezi ya kina nikampa chap akanidm.

Embn ee siakaniingizia mambo sijui ya forex sijui ni kama forex ila betting mara bonyeza link hapo ujisajiri mara nimewahi fanya kazi clouds fm sema mtaji ndio unaniamgusha kwamba hii aidia ninzuri sana ...sikutaka kumsikiliza Tena wala siku link up link aliyotuma nikamlamba block hapo hapo... Kwahiyo mkuu hum Kuna matapeli kibao ukikaa vibaya wanakuumiza pakubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…