Pre GE2025 Kwa utendaji huu uliotukukuka wa Rais Samia huenda 2026 bunge litakosa Wapinzani labda wapewe upendeleo maalumu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
chawa Sasa watumie umeme stiggler inazalisha wakutosha.
 
Oops ! Mkuu Pole Sana Sana Malipo Yako Huko Lumumba FC Buku Saba Huenda Yakasitisha Sababu Ulichoandika Wala Siyo Cha Nchi Hii Ya Tanzania
Jamaa mpaka kajichekq mwenyewe
 
Bila shaka unasubiri uteuzi
 
Utendaji bora upi?
Juzi tu hapo mtwara madaraja yamekatika mwananchi wanahangaika wanazungushwa njia ya Iringa Kwa gharama maradufu.
Yeye lipolipo tu eti amiri jeshi mkuu .
Kashindwa kuwatuma wanajeshi waende wakajenge madaraja ya muda ili mwananchi wapite waendelee na ratiba zao yeye amekaa kupiga siasa na mawaziri wake.
Kitambo hicho wanajeshi walijenga daraja la Kagera ndani ya siku moja
Wanachojua wao ni kuwatumia wanajeshi kufanya usafi wakisikia chadema wanaandamana.
Embu mshaurini apeleke jeshi likasafishe njia huko Kusini kwani serikali yake akina bashungwa wameshindwa kazi.
kulipo kukaa kumsifiasifia ujinga
 
Kwani hata sasa hivi Lina wapinzani? Kwahizi chaguzi zetu za kihayawani , nitashaangaa tume ya uchaguzi kuwatangaza wapinzani wameshinda.
 
chawa Sasa watumie umeme stiggler inazalisha wa kutosha.
 
Kwa ujasiri kabisa hutaki mawazo huru na mbadala yaingie bungeni. Hivi unajua hao wapinzani ndo kioo Cha serikali kujitazama na kujipima juu ya utendaji kupitia ukosoaji na mijadala isiyo na woga? Sikatai kuwa Kuna wabunge wa chama tawala wenye uthubutu wa kuihoji,kuipongeza na kuikosoa serikali pale bungeni,lakini vipi kuhusu uhakika wa uanachama wao na nafasi za uongozi zitokanazo na chama kwa siku za usoni?
Saivi Kuna malalamiko kuhusu kikokotoo Cha wastaafu, Hivi ni wabunge wa upinzani walikuwepo bungeni na kukipitisha?
Wabunge wa upinzani Wana umuhimu wao bungeni hivyo kama tunaiishi demokrasia tuwaache wananchi waamue nani wakuwawakilisha bungeni.
Nimaoni yangu kama mtanzania wa kawaida!
 
Hakuna awamu Wana ccm Wana vitu vingi vya kuonesha huko kwenye Majimbo na kata zao kama Sasa.

Kazi waliyonayo.kwa Sasa ni kupinga chuki za Lisu na uzushi kwamba Samia ameuza Mali za Tanganyika ambayo haipo na Chadema hawaelezi ameuza Kwa bei gani 😁😁
 
Hii ni sawa na baba kumpa mwanaume mwingine mkewe kwa kigezo cha kusaidiwa kuitunza familia, jambo ambalo yeye lilimshinda. Halafu baba huyo ajitanabaishe kama kiongozi bora wa familia kwa kuwa anajali ustawi wao na watanufaika na ujio wa mwanaume huyo. Hiki ni kiwango cha juu sana cha upumbavu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…