Kwa wacheza Drafti wezangu!Tupia Jargon yoyote uliowahi kuisikia

Kwa wacheza Drafti wezangu!Tupia Jargon yoyote uliowahi kuisikia

pia kuna style ya kugogoe uliyeko nje unamwambia mchezaji wako acheze kete fulani lkn kimafumbo. (mfano ruka na sprite ) hii maana yake ashukume kete ya mbele kabisa ya kushambulia. 2 mfano wa pili ni hii ( kutoka tabora ni mi T Risasi majira radio tanzania) Hapa maana yake kuna tumbo unatakiwa utumbue ama anakuonya utatumbuliwa.T risasi alikuwa riporter wa RTD zamani akiitwa Tumbo Risasi. Pia kuna kakisu ka mkujo.nk
 
...Dogo nakuchezea kete jiwe,nishawai kupewa jogoo kwa mchezo huu...
 
pia tuambieni kuna visa watu walipigana kwa maneno hayo au wote huwa wanavumilia???/
 
pia tuambieni kuna visa watu walipigana kwa maneno hayo au wote huwa wanavumilia???/
Hahahahaha katika draft ukisikia ngumi ujue hapo kuna mshamba mmoja kaingia katika mabewe
Ila wajuzi wa mabewe huwa wamefanyiwa operation na kutoelewa kitu kinachoitwa hassira katika nyoyo zao
 
pia tuambieni kuna visa watu walipigana kwa maneno hayo au wote huwa wanavumilia???/
Huwezi kuta ngumi kwenye drafti licha ya maneno na matusi yote hayo. Ukiona ngumi jua kuna sababu zingine.
 
Mkuu uliwahi kuwaona watu kama akina mangwelele akina amani siri na watu wengi watu wanalicheza lile dude mpaka we unaeangalia unapagawa
Daaah mangwelele ana kasheshe sijaona kuna mwanafunzi wake alifariki mwaka jana anaitwa juma mchafu aisee alikua hatari sana yani hashikiki

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
"naona unajaribu kuzuia mafuriko na makalio" apo mpinzani amezidiwa anatafta sare..."unatupa mtoto sababu ya upele"apo mpinzani anatoa kete bure ili apate ahueni...." ukitoa droo najing'ata mgongoni' apo unafunga kilaza mwanzo mwisho
Hahaaa

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom