Kwa wale ambao hatupendi kazi tunazofanya tukutane hapa

gasgas

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2015
Posts
1,092
Reaction score
986
Najua watu wengi sana ambao wapo katika kazi au ajira fulani ambayo kiukweli hawaipendi/hawaifurahii.

Je unapambana vipi na changamoto unazokumbana nazo? Umeweka mikakati ipi kuweza kujinasua?

Mimi nimesomea sekta ya afya na naimudu kiukweli upande wa ujuzi na utaalamu. Najitahidi sana kufanya kazi kwa weledi na uadilifu mzuri lakini najua kabisa moyo wangu uko kwingine.

Pona yangu ni kujiendeleza na elimu niweze kujikita zaidi kwenye field ninayoipenda.

Sent using .... who cares anyway
 
Dah...kwa kifupi ukifanya kazi usiyoipenda ufanisi huwa mdogo sana..hupati furaha..unakuwa na stilesi wakati wote... hata malipo yakiwa makubwa...[emoji2960]

Sent using Beretta ARX 160
 
Tatizo mnasoma fani taaluma ambazo mnaona zina soko la ajira sio taaluma zile mnazoona mna passion nazo
 
Katika hilo sina Bahati sijawahi kuifanyia kazi taaluma niliyoisomea na hata sina mpango nayo ...sikusoma kwa mapenzi yangu Bali matokeo ndio yaliyoamua nielekee huko...

Ila sijutii fani niliyosomea Japo haijawahi kuwa na msaada wa moja kwa moja katika maisha yangu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…