Kwa wale wanaotaka kufika mbali

Kwa wale wanaotaka kufika mbali

NANGA WA DEPO

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2014
Posts
917
Reaction score
1,201
Kama kuna vitu vipya vinavyoingia kwenye ubongo wako lazima kuwe na vitu vya zamani vinaondoka mfano:
Mtoto aliyezaliwa na kufikia hatua ya kutembea kuna akili mpya ilimjia na kuondoa jumla akili ya zamani ya kutambaa ndio maana huwezi kukuta mtoto wa miaka mitano bado anatambaa. Kilichotokea ni kwamba akili ya kutembea imechukua nafasi na akili ya kutambaa imeondoka.
Vilevile Ukisikia mtu ni msomi ujue zamani alikuwa mjinga kwahiyo maarifa mapya yamechukua nafasi ya ujinga.

Kinyume chake pia ni kweli;
Kwamba kadri unavyoingiza vitu vya kijinga kwenye ubongo wako ujue vitu vya maana vinaondoka kupisha ujinga .

Unapenda sana kuangalia komedi kwenye mitandao na mambo mengine ya hovyo.
Ni suala la muda tu utaanza kupoteza uwezo wa kujenga hoja kwenye mambo ya msingi au kuongea vitu visivyo vya maana mbele watu.

Unadai una
"Refresh mind"
Tafadhali usiite burudani chochote ambacho kinahusisha ubongo au kinahusisha akili yako;
Baada ya muda tutaona matokeo kwenye matendo yako na maneno.

NB: Hii ni ya kwa wale wanaotaka kufika mbali tu..
 

Attachments

  • ImageMerge_Collage_20240902_185144311.jpg
    ImageMerge_Collage_20240902_185144311.jpg
    963.4 KB · Views: 3
Ila mbona hujajipa jina zuri japo una mawazo mazuri
Je hiyo haiathiri ukuaji wako!?
 
Ujumbe umeeleweka Mkuu.

Toa huyo jamaa wa mwisho hapo weka Eliud Samwel.
 
Back
Top Bottom