Habarini wapendwa, Kuhusu swala la kuambiwa kutokufanya mapenzi kwa miezi sita nadhali halikuwa na ukweli (ushauri haukuwa sahihi kwa walengwa). Kawaida baada ya mimba kutoka kimamilifu (complete abortion) au kama haikutoka yote (incomplete abortion) na kuhitaji kusafishwa(D&C), swala la kufanya mapenzi zilinaweza kuendelea baada ya wiki mbili hadi nne ikiwa hakutakuwa na tatizo kwa mama mfano kutokwa damu, kutokwa uchafu unaotoa harufu au maambukizi. Cha msingi kinachosisitizwa ni kutumia njia ya kuzuia mimba ambayo mmekubaliana na baada ya maelekezo kutoka kwa mtumishi wa Afya(health care worker). Sababu ya kujizuia kupata mimba kwa kipindi hichi cha miezi sita ni kuhakikisha kuwa afya ya mama inakuwa njema kimwili na kiakili kabla ya kubeba ujauzito mwingine. Ni hakika kuwa kutokwa na mimba kunaweza kupelekea mama kupoteza damu nyingi na hata kupata msongo wa mawazo pia. Naomba kuwasilisha kwa nia njema kabisaaa.