sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
Kama upo Dar maeneo ya Kariakoo, Mjini posta, Msasani, Peninsular, Upanga, Kinondoni ya Morocco, Mikocheni, Masaki, O'bey, n.k Kuna fiber za kutosha kama zuku, Raha, Gofiber, n.k
Fibre ni internet ya waya, unavutiwa waya hadi sehemu ulipo nyumbani kwako, ni internet ya waya lakini kuna kifaa utapewa kinaitwa wireless router, hiki kifaa kitakuwezesha utumie internet kwa wifi ya simu au laptop ama vifaa vingine vyenye wifi.
Kwa mfano internet ya fibre ya zuku inapatikana kino, kariakoo, msasani, peninsular, upanga,n.k utalipia elf 70 kwa mwezi (kifurushi cha chini) au zaidi (kuna vifurushi vina speed kali sana hivi ni kama watumiaji ni wengi na vina speed kali sana) pia hapo hapo utakuwa umelipia na channel za zuku utazocheki kwa kingamuzi.
A.10 Mbps = 69,000,
B.20 Mbps = 99,000
C.40 Mbps = 129,000
D.100 Mbps = 249,000.
Tukumbuke Mbps (Megabits per second) sio na zile megabytes ambazo huwa tunadownload, zile huwa na herufi kubwa ya "MB", ukitaka kujua unaweza kudownload MB ngapi kwa sekunde, hapa kilinganishi ni kwamba 1 Mbps ni sawa na MB 0.125 kwa hio mfano kifurushi A cha 10 Mbps ukifanya hesabu unapata uwezo wa kudownliad MB 1.25 kwa sekunde moja, ukija kifurushi B ni MB 2.5 kwa sekunde, n.k japo speed hushuka pale mnapokuwa watumiaji wengi mnaanza kugawana speed.
Utaweza kutumia internet bila kikomo, speed ni nzuri hata kwa kifurushi cha chini cha elf 70 ambacho unaweza kudownload mb 1 (nasikia sikuhizi ni 2) kwa sekunde, ni speed nzuri hata videos utaangalia bila kukwama na hata kwenye kudownliad utaweza kudownload muvi hata ya GB 1 kwa takribani dakika 18 tu, kitu kizuri zaidi ni hakuna kikomo, hakuna mambo ya ukifikisha gb kadhaa speed inashuka. Makampuni mengi gharama za vifaa na kuletewa waya wa internet hadi kwako ni bure ikiwa utalipia bando la mwezi au miezi kadhaa.
Changamoto ni kwamba haipo kila sehemu Dar na pia inabidi uwe mazingira ya nyumbani au ofisini ili kutumia wifi ya kifaa chao.
Kwa waliopo nje ya maeneo hayo au mikoani TTCL nao wana fibre sema nasikia ni gharama.
Fibre ni internet ya waya, unavutiwa waya hadi sehemu ulipo nyumbani kwako, ni internet ya waya lakini kuna kifaa utapewa kinaitwa wireless router, hiki kifaa kitakuwezesha utumie internet kwa wifi ya simu au laptop ama vifaa vingine vyenye wifi.
Kwa mfano internet ya fibre ya zuku inapatikana kino, kariakoo, msasani, peninsular, upanga,n.k utalipia elf 70 kwa mwezi (kifurushi cha chini) au zaidi (kuna vifurushi vina speed kali sana hivi ni kama watumiaji ni wengi na vina speed kali sana) pia hapo hapo utakuwa umelipia na channel za zuku utazocheki kwa kingamuzi.
A.10 Mbps = 69,000,
B.20 Mbps = 99,000
C.40 Mbps = 129,000
D.100 Mbps = 249,000.
Tukumbuke Mbps (Megabits per second) sio na zile megabytes ambazo huwa tunadownload, zile huwa na herufi kubwa ya "MB", ukitaka kujua unaweza kudownload MB ngapi kwa sekunde, hapa kilinganishi ni kwamba 1 Mbps ni sawa na MB 0.125 kwa hio mfano kifurushi A cha 10 Mbps ukifanya hesabu unapata uwezo wa kudownliad MB 1.25 kwa sekunde moja, ukija kifurushi B ni MB 2.5 kwa sekunde, n.k japo speed hushuka pale mnapokuwa watumiaji wengi mnaanza kugawana speed.
Utaweza kutumia internet bila kikomo, speed ni nzuri hata kwa kifurushi cha chini cha elf 70 ambacho unaweza kudownload mb 1 (nasikia sikuhizi ni 2) kwa sekunde, ni speed nzuri hata videos utaangalia bila kukwama na hata kwenye kudownliad utaweza kudownload muvi hata ya GB 1 kwa takribani dakika 18 tu, kitu kizuri zaidi ni hakuna kikomo, hakuna mambo ya ukifikisha gb kadhaa speed inashuka. Makampuni mengi gharama za vifaa na kuletewa waya wa internet hadi kwako ni bure ikiwa utalipia bando la mwezi au miezi kadhaa.
Changamoto ni kwamba haipo kila sehemu Dar na pia inabidi uwe mazingira ya nyumbani au ofisini ili kutumia wifi ya kifaa chao.
Kwa waliopo nje ya maeneo hayo au mikoani TTCL nao wana fibre sema nasikia ni gharama.