Kwa walio Dar es Salaam tu: Hili ndilo suluhisho la uhakika kukabiliana na gharama zilizopanda za internet

Kwa walio Dar es Salaam tu: Hili ndilo suluhisho la uhakika kukabiliana na gharama zilizopanda za internet

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Kama upo Dar maeneo ya Kariakoo, Mjini posta, Msasani, Peninsular, Upanga, Kinondoni ya Morocco, Mikocheni, Masaki, O'bey, n.k Kuna fiber za kutosha kama zuku, Raha, Gofiber, n.k

Fibre ni internet ya waya, unavutiwa waya hadi sehemu ulipo nyumbani kwako, ni internet ya waya lakini kuna kifaa utapewa kinaitwa wireless router, hiki kifaa kitakuwezesha utumie internet kwa wifi ya simu au laptop ama vifaa vingine vyenye wifi.

Kwa mfano internet ya fibre ya zuku inapatikana kino, kariakoo, msasani, peninsular, upanga,n.k utalipia elf 70 kwa mwezi (kifurushi cha chini) au zaidi (kuna vifurushi vina speed kali sana hivi ni kama watumiaji ni wengi na vina speed kali sana) pia hapo hapo utakuwa umelipia na channel za zuku utazocheki kwa kingamuzi.

A.10 Mbps = 69,000,
B.20 Mbps = 99,000
C.40 Mbps = 129,000
D.100 Mbps = 249,000.

Tukumbuke Mbps (Megabits per second) sio na zile megabytes ambazo huwa tunadownload, zile huwa na herufi kubwa ya "MB", ukitaka kujua unaweza kudownload MB ngapi kwa sekunde, hapa kilinganishi ni kwamba 1 Mbps ni sawa na MB 0.125 kwa hio mfano kifurushi A cha 10 Mbps ukifanya hesabu unapata uwezo wa kudownliad MB 1.25 kwa sekunde moja, ukija kifurushi B ni MB 2.5 kwa sekunde, n.k japo speed hushuka pale mnapokuwa watumiaji wengi mnaanza kugawana speed.

Utaweza kutumia internet bila kikomo, speed ni nzuri hata kwa kifurushi cha chini cha elf 70 ambacho unaweza kudownload mb 1 (nasikia sikuhizi ni 2) kwa sekunde, ni speed nzuri hata videos utaangalia bila kukwama na hata kwenye kudownliad utaweza kudownload muvi hata ya GB 1 kwa takribani dakika 18 tu, kitu kizuri zaidi ni hakuna kikomo, hakuna mambo ya ukifikisha gb kadhaa speed inashuka. Makampuni mengi gharama za vifaa na kuletewa waya wa internet hadi kwako ni bure ikiwa utalipia bando la mwezi au miezi kadhaa.

Changamoto ni kwamba haipo kila sehemu Dar na pia inabidi uwe mazingira ya nyumbani au ofisini ili kutumia wifi ya kifaa chao.

Kwa waliopo nje ya maeneo hayo au mikoani TTCL nao wana fibre sema nasikia ni gharama.
 
Dunia inaondoka kwenye mifumo ya analog kwenda wireless! Wewe unakuja na idea ya kuunganisha miwaya kama TTCL!
Ushaambiwa unapewa router ya wireless unaweza kutumia wifi, Fibre ndio internet yenye kasi kubwa, london asilimia zaidi ya 90 za nyumba na ofisi wanatumia fibre, vitu vingine uwe unafanya utafiti kabla ya kuropoka
 
Ni wakat sasa wa kutletea na mikoan hio ishu mie wakileta nakul maisha nitawapa na majiran walio karib nawachaj vi sent
 
Dunia inaondoka kwenye mifumo ya analog kwenda wireless! Wewe unakuja na idea ya kuunganisha miwaya kama TTCL!
Dunia pia inaondoka kwenye HDD inaelekea kwenye SSD. Lakini tunaotumia NAS hundreds of TBs tunatumia HDD. Kwa sababu kwa use case yetu kuweka kila kitu SSD si practical. Si cost effective.

Miwaya mbona hata Marekani tunatumia. Ulaya wanatumia.

Joe Biden rais wa Marekani kaanzisha mpango wa ku update internet, broadband, wanatumia miwaya (mind you, kusema wanatumia miwaya haumaanishi wanatumia miwaya tu).

South Korea walikuwa na fastest internet last time I checked. Wanatumia miwaya.

Hiyo internet ya wireless unayoitumia kwenye simu nayo mostly imetoka kwenye miwaya iliyopita chini ya bahari.

Ni hivi, hiyo waya inatumika kuleta internet ndani ya nyumba halafu internet ikifika nyumbani unaweka wireless router anayetaka kutumia wireless kwenye simu au laptop anaweza. Ila inakuwa fast na ya gharama nafuu ukilinganisha na internet ya simu.

Mtoa mada amekupa hii kama solution ya kukupa internet kwa gharama nafuu, kama wewe unapenda kupigwa ma bundle ya internet ya simu kuendelea kupigwa hivyo ni haki yako ya kikatiba pia.
 
Kama upo Dar maeneo ya Kariakoo, Mjini posta, Msasani, Peninsular, Upanga, Kinondoni ya Morocco, Mikocheni, Masaki, O'bey, n.k Kuna fiber za kutosha kama zuku, Raha, Gofiber, n.k

Fibre ni internet ya waya, unavutiwa waya hadi sehemu ulipo nyumbani kwako, ni internet ya waya lakini kuna kifaa utapewa kinaitwa wireless router, hiki kifaa kitakuwezesha utumie internet kwa wifi ya simu au laptop ama vifaa vingine vyenye wifi.

Kwa mfano internet ya fibre ya zuku inapatikana kino, kariakoo, msasani, peninsular, upanga,n.k utalipia elf 70 kwa mwezi (kifurushi cha chini) au zaidi (kuna vifurushi vina speed kali sana hivi ni kama watumiaji ni wengi na vina speed kali sana) pia hapo hapo utakuwa umelipia na channel za zuku utazocheki kwa kingamuzi.

Utaweza kutumia internet bila kikomo, speed ni nzuri hata kwa kifurushi cha chini cha elf 70 ambacho unaweza kudownload mb 1 (nasikia sikuhizi ni 2) kwa sekunde, ni speed nzuri hata videos utaangalia bila kukwama na hata kwenye kudownliad utaweza kudownload muvi hata ya GB 1 kwa takribani dakika 18 tu, kitu kizuri zaidi ni hakuna kikomo, hakuna mambo ya ukifikisha gb kadhaa speed inashuka. Makampuni mengi gharama za vifaa na kuletewa waya wa internet hadi kwako ni bure ikiwa utalipia bando la mwezi au miezi kadhaa.

Changamoto ni kwamba haipo kila sehemu Dar na pia inabidi uwe mazingira ya nyumbani au ofisini ili kutumia wifi ya kifaa chao.

Kwa waliopo nje ya maeneo hayo au mikoani TTCL nao wana fibre sema nasikia ni gharama.
Tujichange watu tunaoishi sehemu moja tununue starlink tuwe tunashare tu malipo ya mwezi
 
Back
Top Bottom