Kwa wana Diaspora tunavyomfahamu Zuhura Yunus, ni Mtanzania ila Salim Kikeke ni raia wa Uingereza

Kwa wana Diaspora tunavyomfahamu Zuhura Yunus, ni Mtanzania ila Salim Kikeke ni raia wa Uingereza

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Nimefuatilia taarifa zinazosambaa kwamba Zuhura Yunus ni raia wa Uingereza nachelea kuziamini na kama Zina ukweli basi atakuwa ameupata huo Uingereza Kwa Siri sana. Nafasi aliyopewa lazima tukubali mambo makuu matatu;

Kwanza, ni wazi kwamba si nafasi yakufanywa na Raia wa Kigeni hata kama raia huyo ana uzalendo kiasi gani na ikibainika kwamba umedanganya Utaifa wako basi vyombo vinavyohusika mara moja vinatakiwa kumshauri Mhe. Rais atengue uteuzi wako. Tukumbuke Uraia ni siri na uteuzi pia ni siri ila ukishateuliwa pamoja na vetting iliyofanywa awali kabla ya uteuzi lazima uwajibike kutoa taarifa za kweli kuingia kwenye mfumo wa utumishi. Hapa hakuna kudanganya lazima ueleze ukweli hivyo naamini Zuhura anaweza kuondolewa pale ikibainika anazo taarifa za ziada zinazomwondolea sifa.

Pili, kama tunakubaliana kwamba Zuhura hana utaifa mwingine lazima sasa tumpongeze Mhe. Rais Kwamba amemteua mtu sahihi na mwenye sifa. Zuhuru amekubalika na pande zote akiwa ajawaza kwenda kufanya kazi ikulu. Hakuwahi kuwaza angefika alipo na hivyo ni sahihi kwamba jamii ilimfahamu kabla hata mamlaka azijamfahamu. Kama yeye Mwenyewe akufanya juhudi kulikuza jina lake asingepata malipo haya. Tukubali huyu ni zao la utendaji kazi unaoacha alama.

Tati, Kwa vijana na wanafunzi mnalo la kujifunza. Kuna siku nilitoa mada kuhusu umuhimu wa Idara ya Uhamiaji kuhamasisha Watanzania wasambae Duniani wakajifunze na pale watakapochomoka nakuonekana miongoni mwa Mamilioni wa watendaji basi itatusaidia pale tutakapotaka kuwatumia basi tuwatumie vyema. Kuendelea kukaa humu Ndani kusifu na kuandika mitandaoni masuala ya umbea, kuanza kujifunza unafiki wa uzalendo wa vyama vya siasa utotoni ukaacha kujifunza uzalendo wa kitaifa na kimataifa nikuziba mishipa ya fahamu na kudumaza ubongo. Vijana ondokeni nchini katafteni fursa nje, kafanyeni kazi mashirika ya Kimataifa, kafanyeni kazi nchi jirani mtalisaidia Taifa huko mbele. Mtajifunza uzalendo wa nchi KULIKO uzalendo wa vyama.

Mwisho, niwaombe sana mnapofanikiwa msiukatae Utanzania komaeni na Utanzania. Nilitamani sana kumwona Like akitumikia nchi yake anapoelekea uzeeni lakini waliokua naye wananiambia anatumikia Uraia wa Uingereza kwa Sasa. Laiti asingepata fursa ya uraia wa Uingereza naamini few years to come angerudi kuongoza mashirika au taasisizetu na kuleta western and civilized culture ndani ya mashirika yetu akaondoa uvivu na watu kujiandikia madokezo ya fedha za kula na familia zao bila kuangalia mustakabali wa taasisi wanazokabidhiwa.

Hongera Zuhura Yunus, Hongera Hillary na Hongera Kikeke mmetutambulisha.
 
Nimeupenda ushauri wako kwa vijana wa kitanzania. Asante sana mkuu
 
Uzanzibari kwanza, uzalendo baadae. Kama hamkubali vunjeni huo mnaouita muungano Wazanzibari waendelee. Yaani ndugu zetu waliotapakaa dunia hii ambao wanaweza kutusaidia kuleta maendeleo tuwakatae kisa hawana uzalendo? Upuuzi mtupu.

#FreeZanzibar
 
Uzanzibari kwanza, uzalendo baadae. Kama hamkubali vunjeni huo mnaouita muungano Wazanzibari waendelee. Yaani ndugu zetu waliotapakaa dunia hii ambao wanaweza kutusaidia kuleta maendeleo tuwakatae kisa hawana uzalendo? Upuuzi mtupu.

#FreeZanzibar
Amka usingizini, mbona unacomment upumbavu!!!?
 
Nimefuatilia taarifa zinazosambaa kwamba Zuhura Yunus ni raia wa Uingereza nachelea kuziamini na kama Zina ukweli basi atakuwa ameupata huo Uingereza Kwa Siri sana. Nafasi aliyopewa lazima tukubali mambo makuu matatu...
Haya ndugu Spin doctor wake. Hakikisha basi sisi vijana turahisishiwe kupata pasi, s usafiri ili nasi twende huko majuu.
 
Kwani yule jamaa aliyepata Nobel ni mtanzania au ni mbrit. Yule mchezaji wa mpira aliyewakilisha denmark kwenye kombe la dunia ni mtanzania au ni mdani.

Tanzania tujifunze kwa nchi nyingine kuamini kuwa damu ya kitanzania ni ya kitanzania tu, haigeuki. Ona mifano hii: Naomi Osaka mchezaji wa tennisi, mama yake ni mjapan na yeye mwenyewe alizaliwa. lakini tangu akiwa na miaka mitatu hajaishi japan, amekulia Marekani, ila bado japana inamtambua kuwa ni mtu wao japokuwa sasa hivi ana uraia wa marekani.

Kuna jamaa Armand Gustav "Mondo" Duplantis amezaliwa na kukulia marekani wala hajwahi kuishi Sweden ila kwa kutembelea tu, ila kwa kutumia mama yake ambaye ni msweden, aliiwakilisha sweden kwenye mashindano ya olympic na kuzoa medali.

Lakini Tanzania mtu akishakuwa na link na nchi ya nje tu, anakuwa ni adui; hata kama wazazi wake wote ni watanzania, na huenda ana nyumba Tanzania.
 
Nimefuatilia taarifa zinazosambaa kwamba Zuhura Yunus ni raia wa Uingereza nachelea kuziamini na kama Zina ukweli basi atakuwa ameupata huo Uingereza Kwa Siri sana. Nafasi aliyopewa lazima tukubali mambo makuu matatu...
Wewe ni mwandishi mzuri lakini next time ukianzisha thread andika preamble kujulisha wasomaji nini kimetokea. Usiandike kwa kudhani kuwa wasomaji wote wanafahamu nini kimetokea kwa huyo Zuhura Yunus na huyo Kikeke. Watu tuna shughuli nyingi wiki nzima uko porini hakuna mtandao hata hujui nini kinaendelea duniani. Samahani lakini
 
Tati, Kwa vijana na wanafunzi mnalo la kujifunza. Kuna siku nilitoa mada kuhusu umuhimu wa Idara ya Uhamiaji kuhamasisha Watanzania wasambae Duniani wakajifunze na pale watakapochomoka nakuonekana miongoni mwa Mamilioni wa watendaji basi itatusaidia pale tutakapotaka kuwatumia basi tuwatumie vyema. Kuendelea kukaa humu Ndani kusifu na kuandika mitandaoni masuala ya umbea, kuanza kujifunza unafiki wa uzalendo wa vyama vya siasa utotoni ukaacha kujifunza uzalendo wa kitaifa na kimataifa nikuziba mishipa ya fahamu na kudumaza ubongo. Vijana ondokeni nchini katafteni fursa nje, kafanyeni kazi mashirika ya Kimataifa, kafanyeni kazi nchi jirani mtalisaidia Taifa huko mbele. Mtajifunza uzalendo wa nchi KULIKO uzalendo wa vyama.
Great Word
 
Kwani yule jamaa aliyepata Nobel ni mtanzania au ni mbrit. Yule mchezaji wa mpira aliyewakilisha denmark kwenye kombe la dunia ni mtanzania au ni mdani...
Duniani kote kinachoamua Maisha na tamaduni ya Taifa akitokani na dhaania Bali kinazalishwa kwenye mfumo wa katiba,Sheria na miongozo ya nchi husika.

Tanzania kama Taifa hakuna anayeweza kumkataa mtanzania aliyebadili uraia Kwa sababu duniani uraia wa makaratasi haujawahi kuondoa utaifa wa damu na ardhi.

Kuzaliwa Marekani tayari ni mmarekani bila kujali wazazi wako wana utaifa Gani. Kuzaliwa Tanzania na wazazi wasio Watanzania wewe siyo mtanzania na hakuna namna utakuwa raia kwa kuzaliwa labda uandikishwe uraia.

Nikigoogle nakutana na asili tatu za upatikanaji uraia Dunia. Kwanza ni ardhi au udongo (Soil means kwenye ardhi unayozaliwa katiba na Sheria zikitamka kiumbe unayezaliwa hapa anakuwa raia basi umekuwa raia since unazaliwa).

Namba mbili, ni uraia wa damu (wanaounganisha mbegu wakakuzaa wee walikuwa na uraia Gani tarehe mbegu zao zilipokutana zikakua na kikapatikana kiumbe? Huu ndio Utanzania ambao mtanzania wa kuzaliwa anapatikana Kwa tarehe aliyozaliwa na wazazi waliomzaa walikuwa na uraia Gani?).

Tatu, uraia ambao unaurithi kutokana kuzaliwa kiumbe kwenye mazingira ambayo blood na ardhi zanapatiwa tafsiri tofauti. Hapa utokea pale Mtanzania au Taifa jingine anajifungua mtoto kwenye ardhi ambayo Haina soil connection citizenship.

Nne, ni uraia wa kununua na ambao mfano mzuri wana upata vijana kama akina Kikeke. Huu utokea mara nyingi na mahitaji ya fursa mfano taratibu za ajira kwa mgeni zinapokinzana na taratibu za uraia wako basi unaweza sukumwa ununue uraia upunguze vikwazo.

Najua nimekujibu kitaalamu Sana lakini hii itawafumbua watu macho. Lakini pia itatusaidia wana CCM na vyama vingine kutambua kwamba Tanzania ni salama Kwa sababu misingi ya Uraia kikatiba iliyowekwa na Mwalimu Nyerere imeliponya sana Taifa letu. Bora tukachelewa kwenye maendeleo lakini tukawa salama kuliko kuiga mapokeo ya simplification kwenye eneo la Uraia tukalivuruga Taifa.

Mimi ni muumini wa Diaspora Kwa sababu nimekulia huko ila linapokuja suala la kumshauri au kulishauri Taifa kuhusu uraia na Utaifa napenda kusema Bora tubaki na Raia wachache kuliko kutamani kuufanya uraia WETU uwe utaifa .

South Afrika walifungulia koki Leo wanafanyamaendeleo lakini bila amani, sisi Tanzania tushukuru kwamba Hadi Leo anakabidhiwa nchi Mama Samia, hakuna Rais amewahi kufikia mahali akataka kufumua mfumo WETU wa uraia kwa accomodate mjukuuu au rafiki yake,. Naamini mama Samia atasimamia kutokugusa hiki unachotaka kukipendekeza cha kukubali kufanya uraia uwe vulnerable Kwa viumbe wavurugaji.

Raia wa Kigeni asikanyage Ikulu hata kama atakuwa genius kiasi Gani, raia wa Kigeni asitie mguu kwenye chombo Cha dola hata kama anaasili ya kwetu as long as ameukataa Utanzania abaki kwenye nafasi za bodi na mambo kama hayo ila jikoni asithubutu kutia mguu. Tukiweza kulinda Kwa wivu mkubwa uraia wa kuzaliwa Tanzania itakuwa salama 100 yrs to come.
 
Kwani yule jamaa aliyepata Nobel ni mtanzania au ni mbrit. Yule mchezaji wa mpira aliyewakilisha denmark kwenye kombe la dunia ni mtanzania au ni mdani...
Tunajuana waswahili. Mutu anasema ,"...wabarikiwe wazungu pekee, waafrika walaaniwe." huyo akiwa na uraia wa wazungu unadhani hali itakuwaje kwa waafrika?
 
Nimefuatilia taarifa zinazosambaa kwamba Zuhura Yunus ni raia wa Uingereza nachelea kuziamini na kama Zina ukweli basi atakuwa ameupata huo Uingereza Kwa Siri sana. Nafasi aliyopewa lazima tukubali mambo makuu matatu...
Una akili za kitoto sana

Bado una uelewa mdogo sana wa mambo

Maisha sio nafasi serikalini tu, Gerson Msigwa baada ya kuacha ile nafasi, Umewahi kutana nae ukamuona alivyo kwa sasa?

Huyo Zuhura hata angekataa hiyo nafasi ana exposure kubwa sana na yupo 100 steps more kuliko huyo alieachishwa Haniu au mstaafu Gerson Msigwa

Unaandika kama mtoto wa chekechea, Unachoandika hakijulikani ni hotuba, Risala, Ngonjera au Shairi

Uandishi wako umekaa kama mtu aliyezidiwa na pombe
 
Akikujibu nistue! Anatangaza uzalendo lkn yeye hataki kujulikana Ni Mhaya wa wapi na kujinasibu na uzalendo wa Uhayani. Watu Bwana na Mabibi
 
Umeandika mada tukidhani una taarifa za ziada kumbe huna.

Anapaswa kuukana Uraia wa uingereza ili tuweze kuendelea nae otherwise hata kama mamlaka ya uteuzi inampenda sana ila atakua hana sifa ya muhimu. URAIA.

Pili mamlaka iliyomteua isikae kimya baada ya kelele hizi bala izitolee ufafanuzi.
 
Nimefuatilia taarifa zinazosambaa kwamba Zuhura Yunus ni raia wa Uingereza nachelea kuziamini na kama Zina ukweli basi atakuwa ameupata huo Uingereza Kwa Siri sana. Nafasi aliyopewa lazima tukubali mambo makuu matatu...
Hakuna kusaidia Taifa Africa, Ni kusaidia tumbo lako. Huo ndio UKWELI
 
Back
Top Bottom