Kwa wanaojiandaa kubeba ujauzito, matatizo ya uzazi, wajawazito na watoto wachanga tu

Miss Natafuta

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
27,031
Reaction score
49,928
Hii thread maalumu kwa ajili ya kupeana uzoefu mbalimbali kwenye mambo ya uzazi

Mimi ninaanza na swali la kwanza;

Ninamuomba Mungu nipate ujauzito nipo kwenye harakati za kumpata mzazi mwenzangu, kwa kipindi hiki nifanye maandalizi gani kimwili, sijui kama nina tatizo, sijawai kupima au kukosa ujauzito maana sijawai kutafuta.

Ni sawa nikitumia follic acid kila siku wakati sijajua nitapata ujauzito lini? Hazina madhara zikitumika sana?

Mwenye swali lolote aulize hapa nitakuwa naapdate mara kwa mara.
 
Kula chakula chenye afya...

Fanya mazoezi......

Prenatals zinakuhusu
 
Iyo follic acid ndio nini ebu tujuze wengine ndo tunaickia inaweza kua wapenz we2 wanaitumia bila sisi kujua
 
Ni iron tablets au vidonge vya kuongeza damu.
Kwanza kabisa folate or folic acid sio Iron tablets .

Ni B vitamin ambayo inasaidia ukuaji wa mtoto miezi mitatu ya mwanzo. Kama unajitayarisha kupata mimba huwa Dr wana recommend kuchukua folic acid mwezi kabla hujashika mimba na mpaka wiki 12 ndani ya ujauzito. Lakini kama umeshapata mimba na iko chini ya miezi mitatu huwa wakupa folic acid ya miezi mitatu na unachukua kidonge Mara moja kwa siku kwa muda wa miezi mitatu.

Folic acid inasaidia nini ?
Inasaidia ukuaji na uungaji wa viungo vya mtoto ndani ya ile miezi mitatu ya mwanzo. Ukuaji wa vitu muhimu kabisa kama brain, spinal cord, etc. ugonjwa mkubwa unaotokea Mara kwa Mara unaitwa Spina bifida. Huu unatokana na spinal cord kutojiunganisha vema. Na hii itasababisha mtoto kuwa paralysis of their lower limbs na watoto wengine huwa kwenye wheelchair na pia mtoto anaweza kuwa na tatizo ya njia kubwa na njia ndogo .

anencephaly Ni ugonjwa unaotokana na ubongo ambao haujakuwa na watoto wengine wanazaliwa na fuvu ndogo (incomplete ) watoto wanaoAliwa na huu ugonjwa wengi wao wanaishi masaa machache tu na wanaofikia ukubwa huwa wana kuwa na disability fulani.

Kwa kifupi kabisa kila siku binadamu tunachukua folate/ folic acid kwa sababu tunakula mboga za majani, machungwa na citrus fruits nyinginezo, wholemeal bread, yeast, maini etc .

Mtu mzima anatakiwa kuchukua 400 micrograms Ya folic acid kwa siku . Lakini ukiwa mjamzito unatakiwa kuchukua 600 micrograms. Na saa nyingine ni vigumu kujua kama unachukua kiasi hicho ukiwa mjamzito ndio maana wanakupa vidonge kuhakikisha unachukua the right amount kwa ujauzito .

Nchi zote zilizoendelea ukienda tu kumuona Dr. Mara ya kwanza ukiwa mjamzito au kama unajiandaa kupata ujauzito wanakupa (Folic acid na iodine tablets)

Nitaaeleza kuhusu iodine kwa kirefu baadaye.
 
Folic acid, another form of which is known as folate, is one of the B vitamins. It is used as a supplement during pregnancy to prevent neural tube defects. It is also used to treat anemia caused by folic acid deficiency
 
Folic acid, another form of which is known as folate, is one of the B vitamins. It is used as a supplement during pregnancy to prevent neural tube defects. It is also used to treat anemia caused by folic acid deficiency
Ndio ukosahihi sasa.

Ulikosea hapo mwanzo uliposema ni iron tablets au vidonge vya kuongeza damu.
 
Jamani naombeni msaada mke wangu baada ya kuona dalili za ujauzito kama kichefuchefu, kutapika na maziwa kuuma hasa maeneo ya chuchu, akapima mimba mara mbilu kwa kutumia kale kakipimo ka kujipima mwenyewe popote na vipimo vimeonyesha ana ujauzito. Shida iliyopo ni kwamba kuna maumivu makali yametokea chini ya kitovu kuelekea kiunoni upande wa kulia kiasi hata kuinama ni shida. Na kuna siku ilitoka kitu kama hedhi kiasi kidogo. Baada ya hapo tumeenda hospital dr akashauri tucheki UTI ikanyesha hakuna na akashauri tufanye Ultra Sound hainyaonesha kitu, akatushauri kwamba tufanye tena ultra sound baada ya wiki mbili. Wasiwasi wangu naona hii hali si ya kawaida na ni ujauzito wake wa kwanza. Je inaweza kuwa ni nini na kama kuna mama ashawahi kukutana na changamoto kama hyo alifanyaje kumaliza tatizo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…