Mwenzenu nimekaa na kutathimini historia ya mapenzi yangu tangu nilivyoanza mahusiano ya kimapenzi, nikagundua kuwa wanaume ambo niliwapenda sana hatukuweza kudumu kwa mda mrefu, ila ambao sikuwapenda ile kiukweli ndo niliodumu nao sana na mimi ndo nilikuwa nawaacha kwa sababu sikuweza kujilazimisha kuwa nao wakati siwapendi, nikawa najiuliza maswali mengi kwa nini mwanaume ninaempenda sana ananiacha, sikupa jibu sahihi baadae nikaamua kuanza kusoma tabia za wanaume wawapo kwenye mahusiano katika website mbali mbali na vitabu. Waandishi wengi waliandika kwamba wanaume wanapenda sana kutoa I mean kutoa caring, attension na mambo yote yatakayomfanya aonekane kwa mwanamke wake kwamba anajali, lakini inapotokea mwanamke wake akafanya hayo niliorodhesha hapo juu basi mwanaume huyu atajiona kama anadhalaulika,na kuanza ku pull away, je wanaume ni kweli kwamba mnapopendwa huwa mnatabia ya ku pull away, je hampendi wanawake zenu wawaoneshe mapenzi ya dhati, akupe caring attension na vingine vyote? je mnapenda wanawake zenu wabehave vip mnapokuwa kwenye mahusiano.