Kwa wanawake; uko huru kutembea peke yako mtaani wakati wa mchana au usiku?

Kwa wanawake; uko huru kutembea peke yako mtaani wakati wa mchana au usiku?

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Wakuu,

Kila mtu anapenda akitoka kwenda mahali fulani ajisikie salama na awe huru kutoka sehemu moja au nyingine bila bugudha yoyote.

Hii ni changamoto kidogo kwa wasichana/wanawake wanapotoka kwenda sehemu mbalimbali iwe ni kwaajili ya kutafuta riziki au mtoko wa sherehe, huku wakati wa usiku ukiwa changamoto zaidi.

Baadhi ya changamoto wanazokutana nazo ni kushikwashikwa/kutomaswa hovyo bila ridhaa yao, matusi, na hali ya usalama kwa ujumla ni mambo ambayo yanafanya wanawake wengi kuwa na uoga, kwa ujumla kero kubwa ni usumbufu unaoletwa na wanaume njiani.

Kuna sehemu ukienda inabidi mtu avae kigumu ili apunguze kero za kuzongwa zongwa, au ukitaka ujihisi salama kabisaaa unaongozana jamaa au rafiki yako wa kiume.

Tukirudi kwenye swali, wakati gani wewe dada/mama unajihisi salama zaidi na huru kutembea peke yako mtaani/kwenda kwenye shughuli zako?

Nini kikibadilika kitafanya ujihisi salama kutembea peke yako mtaani?

Wanaume mna maoni gani kwenye hili?
 
Wanawake wengi wanao nyanyaswa hua wanajitakia wenyewe kwa sababu ya mavazi yao wanayo vaa, tena sasa hivi ndio imekua "too much oooooh" wanavaa hadi skintight ambazo huwaliwa ndani ya nguo nyingine wanatembea nazo hadharani bila wasi wasi kabisa, unaepuka vipi kusumbuliwa katika hali kama hiyo, mimi kwa binafsi yangu nikimuona mwanamke wa namna hiyo hua najua ni malaya, na wataendelea kusumbuliwa hadi watie akili
 
Wanawake wengi wanao nyanyaswa hua wanajitakia wenyewe kwa sababu ya mavazi yao wanayo vaa, tena sasa hivi ndio imekua "too much oooooh" wanavaa hadi skintight ambazo huwaliwa ndani ya nguo nyingine wanatembea nazo hadharani bila wasi wasi kabisa, unaepuka vipi kusumbuliwa katika hali kama hiyo, mimi kwa binafsi yangu nikimuona mwanamke wa namna hiyo hua najua ni malaya, na wataendelea kusumbuliwa hadi watie akili
Kwahiyo unasema ni sawa kunyanyaswa kwakuwa wamevaa hivyo? Huoni kama ni kisingizio tu cha kufanya unyanyaji? Na unyanyasaji huu haupati hau uliosema "Wanajitakia" pekee
 
Kwahiyo unasema ni sawa kunyanyaswa kwakuwa wamevaa hivyo? Huoni kama ni kisingizio tu cha kufanya unyanyaji? Na unyanyasaji huu haupati hau uliosema "Wanajitakia" pekee
Wanao jitembeza kiuchi uchi hadharani hata wakinyanyaswa kwa kiasi gani kwangu sioni shida yoyote wamejitakia wenyewe acha wanyanyaswe tuu
 
Back
Top Bottom