Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Mwanadada anatisha kweli!
Kwenye dramas ziijazo hope watampa hiyo nafasi.
Hwaiting!
 
Excellence in acting in a mini-series (kbs drama)
hongera tena park seo joon kwa ushindi

ametoa tena shukrani zake kwa Kim Ji Won, Ahn Jae Hong, Song Ha Yoon, na "Fight My Way" family.siku hizi watu wakimuona baba yangu hawamwiti tena kwa jina lake ila wanamwita park seo joon father,kama si familia yangu basi leo nisingelikuwa hapa

pia hongera kwako jang nara kwa kuibuka ushindi wa kwanza wa tunzo hii kwa upande wa wanawake.ushindi huu ni zawadi kwa timu nzima ya go back couples, kiukweli uwezo wangu wa kuigiza nahisi bado upo chini ila nitafanya kazi kwa bidii zaidi.

pia hongera kwa kim ji won kwa ushindi, nimetokwa na machozi nilipokuwa namsikiliza jang nara,nikabaki nikifikiria je nizungumze kwa haraka ili niondoke ila kwa sasa nahisi hapana sihitaji kuwa na haraka kwani nafasi hii ni adimu kuipata,
namshukuru director, timu nzima ya fight my way,family naahidi kufanya kazi kwa bidii zaidi na kuwa mtu bora mwenye heshima
 
Top Excellence in Acting Male(kbs drama)

hongera nam goong min kwa kuibuka mshindi kupitia chief kim drama, wakati nasoma taarifa nilitamani kuigiza uhusika huu japo kuwa ni uhusika mgeni kwangu, namshukuru sana junho.nilikuja kwenye sherehe nikiwa mikono mitupu ila narudi nikiwa mshindi,huwa sipati usingizi ninaporudi nyumbani haliyakuwa nimeshindwa.hivyo basi ushindi huu iwe ni kwetu sote hususani kwa walioshindwa iwe ni chachu ya ushindi wao hapo baadae

hongera jung rye won kwa kushinda tunzo hii kwa wanawake.
nilikuwa nina furaha sana 2017 na nawashukuru sana wenzangu kwa kazi kubwa tulioifanya.drama ilikuwa ikizungumzia zaidi unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu wa kingono hivyo basi tegemeo langu kwa wale wote wanaofanya makosa haya basi wapewe adhabu kali sana.nategemea drama hii atawaliwaza waathirika wote wa matukio haya, mwisho nitoe shukurani zangu za dhati kwa director
 
Kwaiyo Bae Ajachukua Lol!!!!! Aya Banah Tukutane Mwakani Tena.
Kazi Nzuri Wamestahili walochukua Na Wasochukua Ndo Kukoma tena
Defendant Inastahili ni kati ya drama Ambayo Ilikuwa na Ratings Nzuri Najutia Kwa Nini Niliachia Kati Sasa Yabidi Niirudia kuanzia Sasa
Hongera Zake Sana Sana.
 
kbs daesang awards (grand prize)
song joong ki amewatangaza waigizaji wawili wakongwe kim young chul na chun ho jin kuwa ni washindi wa daesang.

kim young chul: nashukuru sana kwa kushinda tunzo hii, father is strange imekuwa ni drama bora sana mwaka huu,nitoe shukurani zangu za dhati kwa mwandishi na timu nzima kwa kazi ngumu tuliofanya kwa pamoja,pia niwashukuru watazamaji kwa kuipenda KBS na drama ya father is strange.

chun ho jin: kiukweli drama yetu haijaisha mpaka muda huu hivyo basi zawadi hii sitaichukua kwa sababu naogopa nitabweteka na kutokujituma tena.tunzo hii iwe ni zawadi kwa wazazi wote duniani kwani mimi binafsi bado ni mtoto kwa wazazi wangu.
ahsante sana mke wangu ila nakuomba radhi kwani imenichukua muda mrefu kushinda tunzo hii.
tafadhalini endeleeni kuiangalia MY GOLDEN LIFE DRAMA.

WAZEEEE MANSEEEEEEEEEEEEEE
 
Duh Kweli ni wakati Wao Haya Hongera Zao.
 
wazee endeleeni kutufundisha maana ya sanaa, bahati mbaya sanaa ya korea imevamiwa na vibishoo uchwara.



ngoja nisherehekee ushindi wa wazee kwa kujisevia chupa saba za sojuuuuu

wazeeee manseeeeeeee
 
aigoooo ila kbs drama wamekula pesa yangu,
EMPTY donsaeng, aminas noona anyeong.
tokea nilipokaa kwenye computer saa tano asubuhi sijainuka mpaka muda huu.
log off kwa muda.
nawatakia kheri ya mwaka mpya uwe na baraka kwetu sote
Ahsante kwa kutumua muda mwingi kiasi hicho kuhakikisha na sisi hizi sherehe hazitupiti.

You worked hard, sunbae. Job well done!
 
Shukrani na pongezi nyingi ziwaendee nyinyi watu mlio tupatia kile kilicho kuwa kinaendelea huko kwenye Tunzo za KBS na SBS. Nawapenda sana nyote kwa ujumla, pia samahani sana wapendwa Sikuwa na nyinyi kwa mda mrefu toka tunzo zinaanza kutolewa hii ni kutokana na majukumu. Mda ule wanaanza toa tunzo kuna Mahala nilienda kimajukumu, nilikasilika sana na kutaka kuto kwenda maana hata tunzo za MBC jana zilinipita pia. Nikatamani nitume mtu ili akaniwakilishe huko lakin nikaona sio kesi ngoja niende maana natafuta Grisi ya kulainisha vyuma.

Imenichukua lisaa moja kusoma hiz comments za kilicho kuwa kinaendelea kwenye hizo tunzo. Aisee Korea wako vizuri sana, Japo mtu wangu wa nguvu Song Seung Hun hajachukua wala sijamuona sio kesi sana. Kilicho nifurahisha sana kwenye hiz tunzo za leo ni Best couple ya Suzy na Jong suk ile ya kwenye While you were sleeping. Yapo mengi ya kuandika lakini ngoja niishie hapo, ata kuandika nimechoka aisee maana nimefika tu kisha nikazama kwenye huu uzi. Big up Damushin
 
Machozi yananitoka wakuu. So Goodbye!

Hii Nyimbo now ndo Naisikilza Nikiangalia Date imekuwa released Juzi Wengi Wansema SM wameamu kutoa hii Nyimbo na Video kwa Ajili ya Jonghyun.
Mi Naona Waache Aya Yote wasirudishe memory izi kwa Watu tena wakati tunjarbu kusahau,Waache Kila MTU amkumbuke kivyake.!
Wawapa Watu hard time Hasa Team yake.
This is Sad Naona Machozi Yanitoka tena.
 
Ina ujumbe mzito ndani yake na at the same time inatia huzuni.

Tuombe Mola atuepushie mbali!
 
Ina ujumbe mzito ndani yake na at the same time inatia huzuni.

Tuombe Mola atuepushie mbali!
Ila Sm Ina Vipaji Sana..
Music is Ma Life.
Ma life is Music.
Always.
It's bring People's Together kwa kila Lugha na kila Nation.
Music is Music.
 
Naona Mwaka Mupya Huoooooooo,
HERI YA KUONA
Mbarikiwe Wote na Mola akaweke Baraka Zake kwenye Maisha yenu InshaAllah.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…