Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Gianna Ni Mweu wa Mwisho, Wakamwarabia Mwenzeo Sherehe Yake Kwa Bifu Lao..

Uyu Apo Ni Khantwe na I
 
Asante sana kwa kunijuza hili namuelewa sana huyu jamaa.
 
Zenye mandhari gani ?
 
Jo Jae Hyun Admits To Sexual Harassment, Removed From Drama “Cross”
muigizaji veteran jo jae hyun ambaye siku chache zilizopita naye pia alikumbana na shutuma za unyanyasaji wa kijinsia leo hii ametoa taarifa rasmi kuhusiana na shutuma hizo.
  • Jo jae hyun ameandika, kwa ufupi
mimi ni jo jae hyun
uvumi wa kwanza kusambaa ulikuwa unamuhusu muigizaji ambaye pia ni mmiliki wa theater kumlazimisha kumpiga busu staff member baada ya kukaa kwenye mapaja yake.
wakati taarifa hizi zilipotoka nilikuwa nimejiandaa kutoa taarifa kuhusiana na shutuma hizi kwani baadhi ya shutuma zilikuwa ni tofauti na kilichotokezea.
ninakubali ya kwamba kwenye maisha yangu ya sanaa ya takribani miaka 30 nimezungumza maneno machafu na pia nimefanya vitendo vingi vyenye kuchukiza kwa waigizaji wadogo, staff member na hata wanafunzi.
mimi ni mwenye dhambi na nalazimika kuinamisha kichwa changu chini na kuwaomba radhi waathirika wote wa vitendo vyangu nilivyovifanya, kiukweli najisikia aibu na naiomba radhi jamii nzima.
baada ya taarifa hiyo wasimamiaji wa drama ya cross wameamua kuuondoa uhusika wa jo jae hyun kwenye drama hiyo na mpaka sasa bado haijaulikana ni nani ataendelea kuigiza uhusika wake.


siku ya jana mwanadada choi yul ambaye ni muigizaji aliupload screenshot ya picha ya jun jae hyun na kuandika kwenye account yake ya instagram. nilikuwa naisubiri hii siku ya taarifa zako za unyanyasaji wa kijinsia kuwekwa hadharani na nimeshangaa sana kuona taarifa zako zimetoka mapema kuliko nilivyotarajia, huu ni mwanzo tu na kuna watu wengi ambao ni takataka,sina mengi ya kusema kwa sababu nina mengi ya kuyapoteza, mpaka siku ambayo pervert wote watakapopotea.


miongoni mwa drama alizoshiriki jo jae hyun

NB:
hizi taarifa za unyanyasaji wa kijinsia ndani ya mwezi huu zimeshamiri sana nchini korea na kwa jinsi hali ilivyo inaonekana kuna mambo mengi sana yaliojificha kwenye kazi hizi za burudani. siungi mkono vitendo hivi lakini pia siungi mkono waathirika kukaa kimya.
matumaini yangu watazidi kujitokeza wahanga wa unyanyasaji wa kijinsia na kutoa shutuma zao kwa waliokumbana nayo ili kurudisha nidhamu ya kuheshimiana kustahiana bila ya kuangalia jinsia ya mtu na umaarufu wa mtu. nimeipenda hii kampeni ya me too
[HASHTAG]#MeToo[/HASHTAG] movement
 
Duuh hii kali jamani naomba tu ninaowapenda wasikumbwe na kashfa hizi
 

EMPTY dongsaeng,mjr95 ,UHURU JR ,aminas noona na matajiri wengine ambao sijawataja munachokifanya hakipendezi kwenye usawa huu wa tanzania ya viwanda pamoja na kupigana mapanga na bunduki kama drama ya king gwanggaeto na joseon gun man.
munamiliki makampuni makubwa sana ambayo yanawaingizia faida kubwa baada ya kutozwa kodi na kulipia gharama za uzalishaji lakini nashindwa kuelewa kwa nini hamuwapi nafasi celebrities wetu kuwatangazia biashara zenu na matokeo yake munawaacha wanauza pilipili utafikiri watanzania ni wahindi. biashara ni matangazo acheni ubahili, toeni fedha mutangaziwe biashara zenu na wazawa ili consumer wazidi kuvutiwa na bidhaa zenu zinazozalishwa.
EMPTY unashindwa kumpa hata ofa wema sepetu akutangazie biashara yako ya kuuza vifaa vya michezo matokeo yake muda wote anakesha instagram akipost picha zinazomuonyesha kiuno chake kikubwa kama engine ya gari la hino , ukweli ni aibu na unapaswa ujitafakari na uthamini cha kwenu hata wakorea wanathamini cha kwao ndio maana wamefika hapo walipo.

aminas noona wewe ndio umezidi ubahili, unamiliki biashara ya mitindo lakini unashindwa kumpa hata ofa muigizaji mahiri anayekwenda kwa jina la Asha boko akutangazie bidhaa zako, au kwako wewe ni furaha unapomuona mpaka leo ameshindwa kununua hata kinyoleo kwa ajili ya kunyoa ndevu zake kama za mbuzi dume?




mapovu naruhusu sijafua nguo zangu wiki ya nne.
 
Duuh hii kali jamani naomba tu ninaowapenda wasikumbwe na kashfa hizi
hahahahahahhaaaaa mimi nasubiri shutuma za unyanyasaji wa kijinsia wanazofanyiwa wanaume, nitafurahi sana kusikia simulizi zao.
upande mwengine sijawahi kufikiria kama jo min ki atakuwa na tabia za kishenzi zilizopitiliza, aigooo nimesahau kuanza na cheo cha professor jo min ki.
ukorofi hauna sura wala kabila
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] nimecheka kama mwehu..kiuno kikubwa kama engine ya hino? Sunbae nani kakufundisha matusi lakini?
 
Duh! kweli usitazame sura tizama matendo.
 
[emoji102] [emoji102] [emoji102] Hapa kuna njama za kuitiana TRA....[emoji120]
 
heri ya kutimiza miaka 32 iwe kwako choi daniel,wakati wewe unatimiza miaka 32 mimi naelekea kutimiza miaka 105 kwa umri wa taifa la khitan lakini hata mbuzi wa kuazima sina,haya maisha yetu waafrika ni full maigizo ndio maana sishangai jambazi wa bongo movies kuvaa kanzu na kofia anapokwenda kuiba.
 
Mkuu wanasema kila mmoja apambane na hali yake.
 
Hahaaa ugomvi tena.! We si umesema kafundishwa na aminas. Wapi huko waliko fundishana?
Naona unazidi kupigilia msumari hivyo acha bora nikwambie tu.
Kwangua hapo chini kuna jibu limefichwa. LOL!

|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…