Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

MBC Announces It No Longer Plans To Air New Drama “Prometheus
kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka shirika la habari la MBC wamethibitisha kutokuendelea na mipango ya kuisimamia action spy drama itakayokwenda kwa jina la prometheus ambayo inakadiriwa kugharimu 26 million dollar ambazo ni wastani wa 60 billion za kitanzania.
chanzo hicho kutoka MBC kimedai ya kwamba maamuzi ya kuachana na mpango wa kuisimamia drama hiyo umefikiwa muda mrefu kabla hata muigizaji Ha Ji Won hajatangaza uamuzi wa kutokushiriki kwenye drama hiyo.
1540131259789.png
 
MBC Announces It No Longer Plans To Air New Drama “Prometheus
kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka shirika la habari la MBC wamethibitisha kutokuendelea na mipango ya kuisimamia action spy drama itakayokwenda kwa jina la prometheus ambayo inakadiriwa kugharimu 26 million dollar ambazo ni wastani wa 60 billion za kitanzania.
chanzo hicho kutoka MBC kimedai ya kwamba maamuzi ya kuachana na mpango wa kuisimamia drama hiyo umefikiwa muda mrefu kabla hata muigizaji Ha Ji Won hajatangaza uamuzi wa kutokushiriki kwenye drama hiyo.
Bogoshipseyo
 
OK nimekuelewa.
kwa mawazo yangu uyo DJ alitakiwa ahakiki kwanza taarifa zake kabla hajaamua kuiweka sokoni project yake aliyoitafsiri ila bahati mbaya ameshindwa kufanya hivyo au pengine amesahau.
Alitakiwa afahamu ya kwamba hiyo project itaangaliwa na jamii ya watu tofauti wakiwemo wafuatiliaji wa korean entertainment na wasiofuatilia hallyu star kwenye mitandao.
Tatizo linakuja pale kwa wasiofuatilia habari za mitandaoni atakuwa amewadanganya kwa kitendo chake cha kuweka maelezo yasiokuwa sahihi kwenye project yake na kusababisha kujipotezea heshima yake kwenye kazi.
Hakuna sehemu yoyote iliyoandikwa ya kwamba land of war ni jina jengine la gwanggaeto drama ndio maana nilikuuliza land of war ndio ipi?
Profile
  • Drama: Gwanggaeto, The Great Conqueror (English title) / King Gwanggaeto the Great (literal title)
  • Revised romanization:Kwanggaeto Taehwang
  • Hangul: 광개토태왕
View attachment 906154
Mi Kuna Aina Hii Pia Ya Watu huwaga Nabishana Nao kuhusu Izi Drama.

Hawa Wanaoziamisha Hizi Drama Kuingia Katika CD Huwaga Wanawachanganya Sana Watu.
 
1540133643851.png
namsubiri Go Aeshin wangu au kudo hina wangu azaliwe na wazazi wale nisiyowafahamu mpaka muda huu, kwa sisi wanaume unapobahatika kuwa na mwanamke mwenye sifa za lady Aeshin au kudo hina utakuwa na uwezo hata wa kuzuia hata matukio ya utekaji wa wananchi wasiokuwa na hatia pamoja na mauaji ya kishenzi yaliofanya na mfalme wa nchi ile anyejifanya mtakatifu.
  • urembo wa sura na maarifa
  • asiyeona aibu kujifunza
  • jasiri na mwenye huruma
  • mzalendo wa ukweli
  • mpambanaji
  • mwenye mapenzi ya dhati kwa waliokaribu naye
  • aliyetayari kutoa sadaka mali yake kwa ajili ya nchi yake
Writer Kim Eun-sook na Director Lee Eung-bok kwa mara ya tatu wanafanya kazi nyengine nzuri kupitia mikono yao ilio salama, ilifika wakati kila episode niliyokuwa naitazama nilijihisi kama naangalia movie mpya na ost zake zilizidi kuichochea hii drama kuwa nzuri. Ahsante sana Mungu kwa kutuletea huyu mwanamama kim eun sook anayetufanya tusahau dhiki zetu za maisha kupitia ubongo wake uliojaa madini ya maarifa na ubunifu, huyu mama anatuthibitishia jinsi gani wanawake walivyo makini pindi wanapoamua kuacha ujinga na uzembe wa kujidai kama makeup.
1540132745535.png
pichani ndio njia pekee ambayo inapaswa itumiwe na wale wasiokuwa na uwezo wa kupambana na watu wenye tabia za kimungu mtu, hatuwezi kumshinda mtesaji na muuaji bila ya kuonyesha umoja wetu pasina kuangalia vyeo na ubora wa familia zetu tunapotokea, tunapaswa kuonyesha umoja wetu pindi mlala hoi anapokumbana na uonevu na pia tunapaswa kuonyesha umoja wetu pindi tajiri anapokumbana na uonevu na hapo ndipo tutakapo mshinda mtenda dhambi anayetumia kisingizio cha shetani kumtia ujinga.

drama zangu bora nilizoziangalia hadi mwisho mwaka huu wa 2018
  1. mr sunshine = TvN
  2. my mister(ahjussi) = TvN
  3. secret forest =TvN
  4. signal =TvN
  5. welcome to waikiki =Jtbc
  6. Life = Jtbc
  7. whats wrong with secretary kim =TvN
  8. Life on mars =OCN
  9. lawless lawyer =TvN
  10. suits =KBS
  11. wok of love =SBS
  12. grand prince = TV CHOSUN
  13. the miracle we met =KBS
  14. misaeng =TvN
  15. a poem a day =TvN
  16. voice season 2 = OCN
 
Devilish joy kamera wanayotumia duh utadhan wanashutia kwa tecno zetu


On going inayonitesa kuisubiria kila mwisho wa week


100days my prince ,another ongoing tamu
ahjummaaa mtarajiwa miaka 20 ijayo hii avatar yako naomba uiondoe tafadhali.
inanifanya niwe uncomfortable kwa sauti ya won deuk.
utani
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]damushin,yes you damushin of all the people u choose to scam a kid(avatar) in meok goo's voice and lines

Haka katoto nimekapenda kama njaa ya meok mpaka kumtapeli governor,chezea ndoto ya kula bakuli zima la supu na wali
ahjummaaa mtarajiwa miaka 20 ijayo hii avatar yako naomba uiondoe tafadhali.
inanifanya niwe uncomfortable kwa sauti ya won deuk.
utani
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]damushin,yes you damushin of all the people u choose to scam a kid(avatar) in meok goo's voice and lines

Haka katoto nimekapenda kama njaa ya meok mpaka kumtapeli governor,chezea ndoto ya kula bakuli zima la supu na wali
hahahahahaaaaaaa meok goo ana vituko kama watu wa south african walio ondoka juzi baada ya kumrudisha tajiri wao aminas.
lakini sijafurahishwa kiupande fulani kitendo cha yule bwana mdogo kutokupewa muda wa kutosha kwenye drama, alipaswa apewe screen time ya kutosha apate kuzidi kujiamini na kukuza kipaji chake cha uigizaji.
mfano mdogo angalia jinsi gani ko woo rim alivyokuwa anapewa screen time ya kutosha kwenye drama ya Mr Sunshine mpaka inafikia kipindi ule uoga wa kufanya kazi na waigizaji wakubwa kama lee byung hun unaondoka.
1540147631882.png
 
Ila kwa nafasi ndogo alizopewa kazitendea haki hope atapata dili jingine mbeleni la kumkuza zaidi
hahahahahaaaaaaa meok goo ana vituko kama watu wa south african walio ondoka juzi baada ya kumrudisha tajiri wao aminas.
lakini sijafurahishwa kiupande fulani kitendo cha yule bwana mdogo kutokupewa muda wa kutosha kwenye drama, alipaswa apewe screen time ya kutosha apate kuzidi kujiamini na kukuza kipaji chake cha uigizaji.
mfano mdogo angalia jinsi gani ko woo rim alivyokuwa anapewa screen time ya kutosha kwenye drama ya Mr Sunshine mpaka inafikia kipindi ule uoga wa kufanya kazi na waigizaji wakubwa kama lee byung hun unaondoka.
 
UPCOMING DRAMA

Mama Fairy and the Woodcutter / Tale of Gyeryong Fairy
05/11/2018
beautiful lady moon chae won amerudi tena na stori ya kusadikika kupitia kituo pendwa cha TvN pindi itakapomaliza 100 days my prince drama
acha tu nianze na paukwa na nyinyi mutaitikia pakawa ila sijui maana yake ni nini na anayehisi anadanganywa akwende zake gymkhana au colassium guest house akapumzike (natania tu)
omo omo omo
1540155604775.png

hapo zamani za kale kwenye utawala wa Goryeo dynasty alikuwepo mwanadada mmoja anayeitwa Sun Ok-Nam ambaye ujio wake hapa duniani ulikuwa ni wa kimaajabu (fairy).
sasa basi siku moja huyu bidada alikwenda kwenye maporomoko ya maji yaliopo maeneo ya Gyeryong kwa dhumuni la kusafisha mwili wake (kukoga). Wakati akiendelea kukoga alitokezea mvulana mmoja ambaye kazi yake ilikuwa ni kutafuta nishati ya kuni au mbao akazichukua nguo zake kwa dhumuni la kuzificha.

Tukio hilo lilisababisha mwanadada Sun Ok-Nam kushindwa kurudi peponi hivyo basi akaamua kuishi maisha ya ulimwengu huu wa kidunia na bwana mkata kuni na hatimaye walifanikiwa kupata watoto wawili lakini bahati mbaya sana mume wake alifariki dunia baada ya kuanguka kwenye maporomoko ya milima. Sun Ok-Nam alihangaika sana kuzitafuta nguo zake alizokuja nazo ili aweze kurudi kwenye maisha yake ya asili lakini hakufanikiwa kuziona. Sun ok Nam aliamua kuendelea kuishi kwenye ulimwengu huu huku akiwa na matumaini ya kwamba siku moja mume wake atazaliwa tena kupitia mwili mpya (reincarnated).

baada ya miaka takribani 699 kupita siku moja akiwa kwenye milima ya gyeryong ambako alifungua biashara ya kuuza kinywaji aina ya kahawa alitembelewa na wavulana wawili hivyo basi akapata hisia ya kwamba mmoja kati ya wavulana hao wawili amebeba nafsi ya aliyekuwa mume wake ambaye ameshamsubiri kwa karne 7 tokea afariki dunia bahati mbaya sana kati ya wale vijana wawili hakujua ni yupi hasa aliyebeba nafsi ya mume wake, hivyo basi aliamua kuwafuata vijana wale hadi mji mkuu wa korea (seoul) kwa dhumuni la kuwachunguza.

hadithi yangu imeishia hapo na mwenye maswali akamuulize da mange 😡😡
1540155442536.png

nimemkumbuka Khantwe natumai ni mzima wa afya.
 

Attachments

  • 1540157597326.png
    1540157597326.png
    237.6 KB · Views: 57
Kwa takwimu gani zilizofanyika? Watu wanajua wengi ila ni wachache wenye moyo was kusaidia watu! Chief he's too quite good
yes majibu yako yapo sahihi dongsaeng.
kwenye michuano ya miss world anapotokezea mwanadada amepewa heshima ya kuwa mrembo wa dunia haimaanishi ya kwamba eti amewazidi wanawake wote waliopo duniani kwa urembo aliokuwa nao, isipokuwa amepewa heshima ile kwa kuwazidi warembo walioamua kushiriki kwenye michuano ile (sampling).

hivyo hivyo kwa muheshimiwa chief mkwawa kama ulivyosema anastahili heshima hiyo kwa sababu ni mshiriki pekee ambaye ana takwimu nzuri sana za kusaidiwa wadau mbali mbali, ndio maana Inna akaamua kumpa heshima hiyo japo kuwa sentensi yake haikunyooka. Wapo watu humu ndani ni mahodari sana kwenye ishu nzima za computer hardware, software, network, database,programming language tofauti, system analysis and design (SAD) lakini ushiriki wao ni mfu mbele ya chief mkwawa kwenye jukwaa la teknolojia.

ni sawa sawa na kusema labda Damushin ndio best korean drama fans JF nzima, itakuwa unakosea ila mtu akisema inawezekana damushin ndiye mchangiaji mkuu wa stori za korean drama kwenye thread hii ukilinganisha na wengineo pengine atakuwa yupo sahihi.
 
  1. katikati ya wiki simba walikunyima furaha ila manchester united walikupa furaha
  2. leo hii nasikia simba wamekupa furaha ila manchester united wamekunyima furaha
kama ni mtihani wa darasani alama zako ni 50%.

yap nimejikuta napata mapumziko ya kuangalia korean drama bila ya kutarajia, wiki inamalizika nimeangalia episode 6 tena kwa siku moja jambo ambalo ni nadra kutokezea.
natamani hii hali ninayokumbana nayo wiki hii iendelee kiupande wangu japo kwa wiki moja nyegine.
dah huwezi amini nimeamua kufukua makaburi muda huu humu ndani ila bahati nzuri marehemu wote wamebaki vile vile na harufu yenye kuvutia, inaonekana safari yao ni mapumziko ya peponi kama wafiwa wa mv nyerere.

july 5 / 2017 ndio ilikuwa ni mara ya kwanza kusoma comment zako, daebak. Ni mwaka mmoja na miezi 2 tokea nikufahamu japo kwa maandishi ila umekuwa zaidi ya rafiki ambaye tunaonana kila siku.
unazikumbuka hizi comment zako?
  • Yaani naomba uangalie iyo Queen of Seven days ni Nomaaa yaani utaichoka inasisimua balaa,Na ina Ost nzuri sana kam ni mpenzi wa zile nyimbo
  • Hivi na lee seung gi naye bado ajatoka ???
  • Uyo alocheza kwenye bridal Mask si ndo anacheza now kwenye My sassy girl....
  • Naombeni Muangalie FIGHT FOR MY WAY Hii drama kama kurelax na kuenjoy yaani apa ndo mahala pake, Ina vichekesho sana na ni nzuri pia, Forever Korean Drama
kupitia comment ya mwanzo ulinifanya na mimi niitafute hii drama ya queen for seven days na sikujutia maamuzi yangu.

naomba uondoe khofu kwenye nafsi yako,namshukuru Mungu ni mzima wa afya mpaka muda huu
ahsante sana kwa kuwa zaidi ya rafiki dada yangu.
utabaki kuwa ni malikia wa kila siku tofauti na yule malikia wa siku 7
jeongmal gomabseubnida
ahsante sana
View attachment 875689
Uko makini
 
UPCOMING DRAMA

Mama Fairy and the Woodcutter / Tale of Gyeryong Fairy
05/11/2018
beautiful lady moon chae won amerudi tena na stori ya kusadikika kupitia kituo pendwa cha TvN pindi itakapomaliza 100 days my prince drama
acha tu nianze na paukwa na nyinyi mutaitikia pakawa ila sijui maana yake ni nini na anayehisi anadanganywa akwende zake gymkhana au colassium guest house akapumzike (natania tu)
omo omo omo
View attachment 906698
hapo zamani za kale kwenye utawala wa Goryeo dynasty alikuwepo mwanadada mmoja anayeitwa Sun Ok-Nam ambaye ujio wake hapa duniani ulikuwa ni wa kimaajabu (fairy).
sasa basi siku moja huyu bidada alikwenda kwenye maporomoko ya maji yaliopo maeneo ya Gyeryong kwa dhumuni la kusafisha mwili wake (kukoga). Wakati akiendelea kukoga alitokezea mvulana mmoja ambaye kazi yake ilikuwa ni kutafuta nishati ya kuni au mbao akazichukua nguo zake kwa dhumuni la kuzificha.

Tukio hilo lilisababisha mwanadada Sun Ok-Nam kushindwa kurudi peponi hivyo basi akaamua kuishi maisha ya ulimwengu huu wa kidunia na bwana mkata kuni na hatimaye walifanikiwa kupata watoto wawili lakini bahati mbaya sana mume wake alifariki dunia baada ya kuanguka kwenye maporomoko ya milima. Sun Ok-Nam alihangaika sana kuzitafuta nguo zake alizokuja nazo ili aweze kurudi kwenye maisha yake ya asili lakini hakufanikiwa kuziona. Sun ok Nam aliamua kuendelea kuishi kwenye ulimwengu huu huku akiwa na matumaini ya kwamba siku moja mume wake atazaliwa tena kupitia mwili mpya (reincarnated).

baada ya miaka takribani 699 kupita siku moja akiwa kwenye milima ya gyeryong ambako alifungua biashara ya kuuza kinywaji aina ya kahawa alitembelewa na wavulana wawili hivyo basi akapata hisia ya kwamba mmoja kati ya wavulana hao wawili amebeba nafsi ya aliyekuwa mume wake ambaye ameshamsubiri kwa karne 7 tokea afariki dunia bahati mbaya sana kati ya wale vijana wawili hakujua ni yupi hasa aliyebeba nafsi ya mume wake, hivyo basi aliamua kuwafuata vijana wale hadi mji mkuu wa korea (seoul) kwa dhumuni la kuwachunguza.

hadithi yangu imeishia hapo na mwenye maswali akamuulize da mange 😡😡
View attachment 906697
nimemkumbuka Khantwe natumai ni mzima wa afya.
View attachment 906718
dah hizi hanbok siku za mbeleni itanilazimu nimtafutie my only one, itapendeza sana tukizivaa mtoko wa jioni kwa ajili ya chakula, natumai hatoniuliza
honey mbona unatumia sana, hivi umeshaweka hela ya kununua umeme na malipo ya watoto kwa ajili ya skuli na madrasa.
Nitaitafuta Hii
 
Back
Top Bottom