Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

MBC Announces It No Longer Plans To Air New Drama “Prometheus
kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka shirika la habari la MBC wamethibitisha kutokuendelea na mipango ya kuisimamia action spy drama itakayokwenda kwa jina la prometheus ambayo inakadiriwa kugharimu 26 million dollar ambazo ni wastani wa 60 billion za kitanzania.
chanzo hicho kutoka MBC kimedai ya kwamba maamuzi ya kuachana na mpango wa kuisimamia drama hiyo umefikiwa muda mrefu kabla hata muigizaji Ha Ji Won hajatangaza uamuzi wa kutokushiriki kwenye drama hiyo.
 
Bogoshipseyo
 
Mi Kuna Aina Hii Pia Ya Watu huwaga Nabishana Nao kuhusu Izi Drama.

Hawa Wanaoziamisha Hizi Drama Kuingia Katika CD Huwaga Wanawachanganya Sana Watu.
 
namsubiri Go Aeshin wangu au kudo hina wangu azaliwe na wazazi wale nisiyowafahamu mpaka muda huu, kwa sisi wanaume unapobahatika kuwa na mwanamke mwenye sifa za lady Aeshin au kudo hina utakuwa na uwezo hata wa kuzuia hata matukio ya utekaji wa wananchi wasiokuwa na hatia pamoja na mauaji ya kishenzi yaliofanya na mfalme wa nchi ile anyejifanya mtakatifu.
  • urembo wa sura na maarifa
  • asiyeona aibu kujifunza
  • jasiri na mwenye huruma
  • mzalendo wa ukweli
  • mpambanaji
  • mwenye mapenzi ya dhati kwa waliokaribu naye
  • aliyetayari kutoa sadaka mali yake kwa ajili ya nchi yake
Writer Kim Eun-sook na Director Lee Eung-bok kwa mara ya tatu wanafanya kazi nyengine nzuri kupitia mikono yao ilio salama, ilifika wakati kila episode niliyokuwa naitazama nilijihisi kama naangalia movie mpya na ost zake zilizidi kuichochea hii drama kuwa nzuri. Ahsante sana Mungu kwa kutuletea huyu mwanamama kim eun sook anayetufanya tusahau dhiki zetu za maisha kupitia ubongo wake uliojaa madini ya maarifa na ubunifu, huyu mama anatuthibitishia jinsi gani wanawake walivyo makini pindi wanapoamua kuacha ujinga na uzembe wa kujidai kama makeup.
pichani ndio njia pekee ambayo inapaswa itumiwe na wale wasiokuwa na uwezo wa kupambana na watu wenye tabia za kimungu mtu, hatuwezi kumshinda mtesaji na muuaji bila ya kuonyesha umoja wetu pasina kuangalia vyeo na ubora wa familia zetu tunapotokea, tunapaswa kuonyesha umoja wetu pindi mlala hoi anapokumbana na uonevu na pia tunapaswa kuonyesha umoja wetu pindi tajiri anapokumbana na uonevu na hapo ndipo tutakapo mshinda mtenda dhambi anayetumia kisingizio cha shetani kumtia ujinga.

drama zangu bora nilizoziangalia hadi mwisho mwaka huu wa 2018
  1. mr sunshine = TvN
  2. my mister(ahjussi) = TvN
  3. secret forest =TvN
  4. signal =TvN
  5. welcome to waikiki =Jtbc
  6. Life = Jtbc
  7. whats wrong with secretary kim =TvN
  8. Life on mars =OCN
  9. lawless lawyer =TvN
  10. suits =KBS
  11. wok of love =SBS
  12. grand prince = TV CHOSUN
  13. the miracle we met =KBS
  14. misaeng =TvN
  15. a poem a day =TvN
  16. voice season 2 = OCN
 
Devilish joy kamera wanayotumia duh utadhan wanashutia kwa tecno zetu


On going inayonitesa kuisubiria kila mwisho wa week


100days my prince ,another ongoing tamu
ahjummaaa mtarajiwa miaka 20 ijayo hii avatar yako naomba uiondoe tafadhali.
inanifanya niwe uncomfortable kwa sauti ya won deuk.
utani
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]damushin,yes you damushin of all the people u choose to scam a kid(avatar) in meok goo's voice and lines

Haka katoto nimekapenda kama njaa ya meok mpaka kumtapeli governor,chezea ndoto ya kula bakuli zima la supu na wali
ahjummaaa mtarajiwa miaka 20 ijayo hii avatar yako naomba uiondoe tafadhali.
inanifanya niwe uncomfortable kwa sauti ya won deuk.
utani
 
hahahahahaaaaaaa meok goo ana vituko kama watu wa south african walio ondoka juzi baada ya kumrudisha tajiri wao aminas.
lakini sijafurahishwa kiupande fulani kitendo cha yule bwana mdogo kutokupewa muda wa kutosha kwenye drama, alipaswa apewe screen time ya kutosha apate kuzidi kujiamini na kukuza kipaji chake cha uigizaji.
mfano mdogo angalia jinsi gani ko woo rim alivyokuwa anapewa screen time ya kutosha kwenye drama ya Mr Sunshine mpaka inafikia kipindi ule uoga wa kufanya kazi na waigizaji wakubwa kama lee byung hun unaondoka.
 
Ila kwa nafasi ndogo alizopewa kazitendea haki hope atapata dili jingine mbeleni la kumkuza zaidi
 
UPCOMING DRAMA

Mama Fairy and the Woodcutter / Tale of Gyeryong Fairy
05/11/2018
beautiful lady moon chae won amerudi tena na stori ya kusadikika kupitia kituo pendwa cha TvN pindi itakapomaliza 100 days my prince drama
acha tu nianze na paukwa na nyinyi mutaitikia pakawa ila sijui maana yake ni nini na anayehisi anadanganywa akwende zake gymkhana au colassium guest house akapumzike (natania tu)
omo omo omo

hapo zamani za kale kwenye utawala wa Goryeo dynasty alikuwepo mwanadada mmoja anayeitwa Sun Ok-Nam ambaye ujio wake hapa duniani ulikuwa ni wa kimaajabu (fairy).
sasa basi siku moja huyu bidada alikwenda kwenye maporomoko ya maji yaliopo maeneo ya Gyeryong kwa dhumuni la kusafisha mwili wake (kukoga). Wakati akiendelea kukoga alitokezea mvulana mmoja ambaye kazi yake ilikuwa ni kutafuta nishati ya kuni au mbao akazichukua nguo zake kwa dhumuni la kuzificha.

Tukio hilo lilisababisha mwanadada Sun Ok-Nam kushindwa kurudi peponi hivyo basi akaamua kuishi maisha ya ulimwengu huu wa kidunia na bwana mkata kuni na hatimaye walifanikiwa kupata watoto wawili lakini bahati mbaya sana mume wake alifariki dunia baada ya kuanguka kwenye maporomoko ya milima. Sun Ok-Nam alihangaika sana kuzitafuta nguo zake alizokuja nazo ili aweze kurudi kwenye maisha yake ya asili lakini hakufanikiwa kuziona. Sun ok Nam aliamua kuendelea kuishi kwenye ulimwengu huu huku akiwa na matumaini ya kwamba siku moja mume wake atazaliwa tena kupitia mwili mpya (reincarnated).

baada ya miaka takribani 699 kupita siku moja akiwa kwenye milima ya gyeryong ambako alifungua biashara ya kuuza kinywaji aina ya kahawa alitembelewa na wavulana wawili hivyo basi akapata hisia ya kwamba mmoja kati ya wavulana hao wawili amebeba nafsi ya aliyekuwa mume wake ambaye ameshamsubiri kwa karne 7 tokea afariki dunia bahati mbaya sana kati ya wale vijana wawili hakujua ni yupi hasa aliyebeba nafsi ya mume wake, hivyo basi aliamua kuwafuata vijana wale hadi mji mkuu wa korea (seoul) kwa dhumuni la kuwachunguza.

hadithi yangu imeishia hapo na mwenye maswali akamuulize da mange 😡😡

nimemkumbuka Khantwe natumai ni mzima wa afya.
 

Attachments

  • 1540157597326.png
    237.6 KB · Views: 57
Kwa takwimu gani zilizofanyika? Watu wanajua wengi ila ni wachache wenye moyo was kusaidia watu! Chief he's too quite good
yes majibu yako yapo sahihi dongsaeng.
kwenye michuano ya miss world anapotokezea mwanadada amepewa heshima ya kuwa mrembo wa dunia haimaanishi ya kwamba eti amewazidi wanawake wote waliopo duniani kwa urembo aliokuwa nao, isipokuwa amepewa heshima ile kwa kuwazidi warembo walioamua kushiriki kwenye michuano ile (sampling).

hivyo hivyo kwa muheshimiwa chief mkwawa kama ulivyosema anastahili heshima hiyo kwa sababu ni mshiriki pekee ambaye ana takwimu nzuri sana za kusaidiwa wadau mbali mbali, ndio maana Inna akaamua kumpa heshima hiyo japo kuwa sentensi yake haikunyooka. Wapo watu humu ndani ni mahodari sana kwenye ishu nzima za computer hardware, software, network, database,programming language tofauti, system analysis and design (SAD) lakini ushiriki wao ni mfu mbele ya chief mkwawa kwenye jukwaa la teknolojia.

ni sawa sawa na kusema labda Damushin ndio best korean drama fans JF nzima, itakuwa unakosea ila mtu akisema inawezekana damushin ndiye mchangiaji mkuu wa stori za korean drama kwenye thread hii ukilinganisha na wengineo pengine atakuwa yupo sahihi.
 
Uko makini
 
Nitaitafuta Hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…