Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kuna series inaitwa kill me,heal me ni noma ni ya 2019 inahusu jamaa mmoja ambaye ana tatizo la kuingiliwa na nafsi mbaya
thanks brother kwa hii zawadi,
hiyo drama sijawahi kuiangalia japokuwa niliwahi kuwa nayo completed, halafu ni project ya mwaka 2015 na si 2019 kama ulivyowasilisha hapo juu.
ji sung kwa mwaka huu wa 2019 ameigiza drama inayoitwa DR JOHN​
 
thanks brother kwa hii zawadi,
hiyo drama sijawahi kuiangalia japokuwa niliwahi kuwa nayo completed, halafu ni project ya mwaka 2015 na si 2019 kama ulivyowasilisha hapo juu.
ji sung kwa mwaka huu wa 2019 ameigiza drama inayoitwa DR JOHN​
Yah upo sahihi ni ya 2015 ile we jamaa sikuwezi unafuatilia sana series za kikorea.
 
trh.24

Mhhhhh!
hivi ulifikiri hii siku nitaisahau?
heri ya kuzaliwa iwe juu yako na natumai hukunidanganya kwa njia ya keyboard kwa sababu sidhani kama una tabia hiyo ya kuongopa,

Asubuhi nilipoamka jambo kwanza nililiangalia jua llililokuwa linajiandaa kuchomoza kwa dhumuni la kuiangaza dunia na vilivyomo ndani yake, nikabaki najisemea huenda yule binti aliyezaliwa tarehe kama ya leo miaka telee iliopita hata wazazi wake walikuwa na ndoto ya kumuona binti yao pindi atakapopevuka awe na uwezo wa kuiangaza dunia yake na wenzake kwa kutumia kifikra zake zitakazoongozwa zaidi na utulivu wa nafsi iliojaa furaha ndani yake.

kama mpaka leo umeshindwa kuiangaza dunia yako unaonaje ukaianza siku ya leo kwa kufikiria zaidi yajayo kuliko matukio yale yote yaliopita yaliokufanya ushindwe kuing'arisha dunia kwa mikono yako miwili, kama aliweza Oprah Winfrey aliyekuwa na historia mbovu pengine kuliko wewe kwa nini iwe vigumu kiupande wako?

unadhani Mungu anakuchukia?
unadhani Mungu amekupangia uwe hivyo maisha yako yote?
unadhani Mungu amekupangia uteswe na wajinga wajinga kama daemusin kihisia?
hapana hapana sitaki kuamini hivyo kwa sababu Mungu hana wivu wa kijinga jinga na roho mbaya ya mafanikio kama aliyonayo daemusin.
tafadhali anza upya kuanzia leo naamini kwa nguvu na uwezo wakebwana Mungu hatakupuuza.​

hizi zawadi ninazokutumia usije ukazivamia zote kwa siku kama mfungwa aliyelazwa na njaa kwa wiki nzima, kufanya hivyo utalipelekea tumbo lako liwe kubwa kama pipa la lami.

🍏🍎🍐🍊🍋🍌🍉🍇🍓🍈🥦🥑🍅🍅🥝🥥🍍🥭🍑


japokuwa ulimtuma dada yako Prishaz aje anirushie kichambo na vitisho juu siku ile kama mwanamume niliyefumaniwa na mbuzi meee kwa sababu dhaifu ya kukuita ahjummaaa naomba ufahamu ya kwamba mjinga mimi sikuchukia lile tendo na kiukweli sitoacha kukuita ahjummaaa mpaka itakapofika siku ya harusi yako na yule niliyemuota usingizini mwenye upara kichwani kama zidane 🏇🏇🏇.
mfikishie taarifa hii yule dada yako aliyekuja na mishale yake kama jumong pamoja na sindano kama daktari wa wanyama , mwambie mimi ni mbabe na mtemi nisiyeogopa hata hashuo la kuku mzazi.

==============================================

HAPPY BIRTHDAY aminas
 
Mai Chingu.🙏

Mungu tu Anajua.

Ahsante Na Shukalni Sana Sana Kwa Wishes Hizi.

Mola Wangu Azidi kukubariki Mpendwa Wangu Mara Dufu.
Nimeongeza Mwaka Mwengine tena Leo Wala Sijakuongopea.
 
Daemusin umeamua kumchamba noona tena kabisa! Kwa leo sitasema sana ila Amina ujue tu niko hapa kupigania haki yako, bado hujafaa kuitwa hilo jina na huyu dogo nitakomaa nae. Happy birthday Amina, leo tusherehekee huyu mpinzani namuweka kiporo🍾🍾🎂
 
ok, ok mic test
nimeona sitopata faida na fungu la baraka endapo nitaendelea kutofautiana kifikra na dada mkubwa hivyo basi kuanzia leo rasmi nafuta neno ahjummaa kwenye kamusi langu la maneno na nitaliweka neno nae yeoja (my lady).

happy friday noona:
wenyewe wanasema siku ya Ijumaa ni siku muhimu zaidi kwa wafanyakazi, wasiofanya kazi na hata waajiri na ndio siku inayo simbolize mapumziko ya nafsi baada ya kuzipokea kelele, stress, dhihaka za wiki nzima. Pia ndio siku ya kuikaribisha weekend ya kujitathmini kwa yale yote ulioyatenda au kupanga kuyatenda mbeleni.

geonbae (건배) = cheers.
kama ni mnywaji sana wa maji pendwa basi wiki hii naomba upunguze, sipendi kumuona dada yangu mpendwa anakunywa maji kama samaki.
 
Mai Chingu.🙏

Mungu tu Anajua.

Ahsante Na Shukalni Sana Sana Kwa Wishes Hizi.

Mola Wangu Azidi kukubariki Mpendwa Wangu Mara Dufu.
Nimeongeza Mwaka Mwengine tena Leo Wala Sijakuongopea.
upo sahihi Mungu pekee ndio ajuaye tunayoyapitia kwenye harakati zetu za kila siku za maisha, ni jambo la furaha zaidi kujikuta tunakutana kwa pamoja maeneo kama haya na kuchati pamoja jambo linalopelekea kwa pamoja tuyasahau yale yote mabaya tunayokumbana nayo japokuwa ni kwa muda mfupi.

happy friday.
heri ya kuzaliwa kwa mara nyengine tena.
ila na wewe punguza kushabikia mikia FC, ukiendelea kushabikia mikia FC tutakupeleka mbugani alipo faru khadija.

yanga oyeeee nasikia wiki hii wanacheza
 
Song Triplets Suit Up To Support Song Il Gook As He Becomes Honorary Ambassador For ChildFund Korea

October 25, kampuni ya C-JeS Entertainment’s kupitia official Instagram account waliweka picha zinazoonyesha familia ya song il kook na watoto wake watatu wakiwa pamoja.
mbele ya picha pakiandikwa maneno yafuatayo:

song il kook, malaika wa watoto ameteuliwa kuwa balozi wa ChildFund Korea, ni jambo la heshima kuwa sehemu muhimu kama hii, tutaendelea kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuwasaidia watoto wote dunia kuishi kwa furaha.

sherehe hizo zilifanyika oktoba 24.

song il kook amejizolea umaarufu mkubwa sana duniani baada ya kushiriki kwake variety show inayoitwa return of superman pamoja na watoto wake kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2016.

 

What a good news? [emoji173]️[emoji173]️[emoji173]️
Nafurahi kumuona Oppa Bae akipata offers kama hizi.
Huyu siku akija na drama mpya atanipa wazimu, nitakuwa silali kabla sijaangalia episode mpya tena na vile wanawekaga bila episode ikiwa ya moto nitakoma!
 
tuna mpango wa kujiingiza kwenye ulingo wa siasa bibieeee kama walivyo our ancestors.
mama, babu, baba wa babu
teh teh natania.

halafu sielewi kwa nini song amekuwa kimya sana kwenye ulimwengu wa drama haliyakuwa hiyo kampuni inayomsimamia kazi zake kwa sasa ina nguvu kubwa sana kwenye huu ulimwengu wa burudani nchini korea na asia kwa ujumla.
 
Ahsante Sana.

Mpinzani Analeta Kiburi Sana.
 
Yaani Kiukweli Hii ni Drama Nzuri Sana Ila Inanichanganya Ninapoifananisha Na Six Flying Dragons

Yaani Naona Waigizaji Wake Wananichaganya Inabidi Nigoogle Kila Muda.
 
Yaani Kiukweli Hii ni Drama Nzuri Sana Ila Inanichanganya Ninapoifananisha Na Six Flying Dragons

Yaani Naona Waigizaji Wake Wananichaganya Inabidi Nigoogle Kila Muda.
  1. yi seong gye
  2. yi bang won
  3. queen sindeok na watoto wake wawili akiwemo (yi bang seok)
nafikiri ni characters hao tu ndio unaweza kuwaona ndani ya six flying dragons drama.
director pamoja na muandishi wameinyonga mapema love triangle.
 
  1. yi seong gye
  2. yi bang won
  3. queen sindeok na watoto wake wawili akiwemo (yi bang seok)
nafikiri ni characters hao tu ndio unaweza kuwaona ndani ya six flying dragons drama.
director pamoja na muandishi wameinyonga mapema love triangle.
Ila Hii Drama Inaelezea Maisha ya Yi Bang Won Zaidi Ama!?

Yaani Dhamira Yake Kubwa!?
 
Ila Hii Drama Inaelezea Maisha ya Yi Bang Won Zaidi Ama!?

Yaani Dhamira Yake Kubwa!?
inawahusu zaidi vijana wawili waliojijengea urafiki wa shida na raha tokea udogoni mwao, bahati mbaya sana mitazamo tofauti ya kisiasa ikapelekea kusambaratika kwa urafiki wao.

kwa kuangalia mtiririko wa hii drama kivyovyote huko mbeleni Seo Hwi atajijengea uaminifu mkubwa sana kwa lee bang won japokuwa kwa sasa anajipendekeza kwake kwa dhumuni maalum na huenda ndiye atakayemsaidia kumkomboa mdogo wake wa kike kwenye makucha ya baba yake Nam Sun-Ho.

ukimuangalia Nam Sun-Ho yeye moja kwa moja ameamua kujificha kwenye mwamvuli wenye nguvu kwa sasa (royal family) wakiongozwa na mfalme yi seong gye , queen sindeok, baba yake na yule binti anayeitwa Han Hee-Jae

Nam sun ho na baba yake wanashinikiza crown prince awe lee banseok ambaye ni mtoto wa nane wa mfalme yi seong gye, kiupande wao wanaamini bwana mdogo ndiye atakayeweza kulifanya taifa changa la joseon liweze kujijenga (kwa akili ya kawaida unagundua ya kwamba wanakhofu kubwa sana na nguvu ya lee bang won endapo atabeba yeye madaraka jambo itawapelekea wapoteze ushawishi wao ndani ya serikali)
 
Njooni tushee japo kidogo kwa hicho kilichowatia busy.
Mfano miye, WANG GUN ep.134, SOLDIER (god of war) ep.37 , Memorial of Imjin War( Jingbirog) ep.38
 
Zote hizo kwa wakati mmoja???
Siwezagi aiseeee
Nina wiki mbilii zimesalia kabla ya kuanza kuwa busy kwahiyo Huu muda wacha niutumie vizuri, najua nikishaanza kuwa busy huenda kwa wiki nikatazama ep. 3 - 5.
Ila kwa kawaida Episode 2 -4 huwa zinanitosha.
Lakini tangu Oktoba imeanza kwa siku ni Episode 5-7.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…