Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Hii drama kila sehemu inasifiwa.
 
Hata maelezo sijasoma maana sio zangu hizi
 
Kill Me, Heal Me

Hii Drama niliitazama kipindi fulani hivi na niliipenda kiukweli na kinachonivutia zaidi ni jinsi ambavyo walivyojaribu kutuonesha kwa jinsi gani huu ugonjwa wa Multiple Personalities ama Dissociative Identity Disorder (DID) ulivyo na unavyoweza kumuathiri binadamu pale ambapo anapojaribu kuyakabili mawazo mabaya ya zamani hususani kipindi cha utoto akilini mwake hatimaye kupelekea kuzalishwa kwa nafsi nyingine.

Wikipedia


Unaweza usiamini lakini hili tatizo ni la ajabu sana na ni ngumu sana kulitibia ama kumrudisha mgonjwa katika hali yake ya kawaida aliyokuwa nayo kabla ya kuupata huu ugonjwa.

Katika Kill Me, Heal Me nakumbuka matatizo aliyoyapata Cha Do-Hyun (Ji Sung) wakati wa utoto ndiyo yalipelekea kuzalishwa kwa nafsi nyingine kadhaa ndani yake na kila nafsi ilikuja na jina lake, tabia zake, faida na hasara zake.

Kuna wakati nafsi moja wapo inapochukua 'usukani' na kuuendesha mwili unaweza ukafanya mambo makubwa sana yenye faida lukuki kitu ambacho kwa nafsi ya kawaida ya muhusika asingeweza kufanya mambo makubwa kama hayo. Hebu pata picha mtu ana huu ugonjwa wa DID alafu ndani yake ana nafsi mojawapo yenye tabia za Bill Gates hahaha! Just Kidding!

Hii Project ya Kill Me, Heal Me ilikuwa ichezwe na Lee Sung-Ki kama muhusika mkuu ama Cha Do-Hyun lakini haikuwezekana kutokana na 'Ubize' kwenye Projects nyingine na hatimaye ikachukuliwa na Ji Sung. Ila Ji Sung ameicheza vizuri hii Character kiukweli ama wengine mliopata kuitazama hii Drama sijui mnaonaje? Je Le Sung-Ki angeongeza kitu cha ziada zaidi kuliko Ji Sung?
 
Huu 'Ubize' nao umeanza kushika kasi kama 'Upepo wa Kisulisuli'.

Umepelekea mpaka wengine tumejipa 'Suspension' ya kilazima ya kutotazama Drama hata hiyo Episode moja inakubidi upige mahesabu ya kaupenyo ka muda kwa kutumia zana kama Scientific Calculator bila kusahau Four Figure.
 
"Tanzania Yangu Tunakosea Wapi?"

Hilo ni swali pengine 'Gumu' sana na labda itahitajika kuwakusanya Maprofesa kama 700 hivi wafanye Discussion ili watupe jibu la pamoja la swali hilo.

Ila kiukweli inafurahisha sana na inatia hamasa kutazama kitu cha kiasili kutoka mahali fulani ambacho ndiyo utamaduni wao wa kiasili na si ule wa kuletwa na 'Upepo wa Kisulisuli'.
 
Nahitaji mnitajie season kali kuzidi six flying dragon
Mzitoe
Greet queen, empress ki na flower in prison.
Sawa, Hebu jaribu hii inayoitwa; Cruel Palace: War Of Flowers.

Hiyo ni Historical na humo ndani kuna vita kali sana 'Mjengoni' kati ya wanawake wa Mfalme Injo wa Joseon. Hiyo vita kali nadhani ndiyo imepelekea kwa Drama hiyo kupewa jina hilo.

Vita hiyo kali inaongozwa na Royal Concubine Soyong Jo ambaye anatumia kila jitihada ili kumuweka mwanaye katika kiti cha Ufalme. Sasa, ili kufanya hivyo inambidi amsafishie njia na hapo sasa analazimika kufanya mauaji kwa wale wote anaowahisi ni kikwazo kwa mwanaye kukifikia kiti hicho cha Ufalme.

Itafute.
 
[emoji27][emoji27][emoji27][emoji27][emoji27][emoji27][emoji27]
 
Kwenye hiyo telegram kumbe ukipakua series haiingii kwenye simu inabaki huko huko at a time inajifunga?? Ndio kilichonitokea baada ya kujaribu leo.. what to do? Sio mwenyeji sana wa telegram
 
Once again MB zangu zimepotea

Hii Golden garden ilitakiwa iwe na episode 16 tu zikizidi sana 20 sio mpaka 60 huko wakati hata haina mwanga mzuri,story mbovu

When the camellia blooms ipo slow inafaa muda ambao upo eneo lisilo na network porin huko umeboreka weee halafu movie unayo hio hio moja.

Empress KI nzuri ila ilifaa ipunguzwe episode basi tu enzi hizo ilikua mwendo wa episode nyingi
 
Miye namisi drama zenye Episode nyingi.

Wivu ndo unanisumbua au Nina fikra zenye makengeza why hiyo Drama ya Empress Ki karibia kila mtu anaisifu, halafu miye naiona kama Historical Drama mbovu kuliko zote nilizowahi kuziona. SIJUI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…