Huyo ni wa kumvumilia tu!
Pamoja na sababu au masuala mengine ni kutokana na kutofautiana kwa malengo na misimamo yao.
Hatimaye chuki, wivu na tamaa vinazaliwa na kusababisha mafarakano ambayo yanapelekea hayo mauaji n.k.
Kuna msemo wanapenda kuusema sana kwamba "Glory can not be shared".
Yaani, utukufu hauwezi kugawanywa pande mbili au zaidi hasa linapokuja suala la kutawala nchi.
Hii ni kuhofia mpasuko wa madaraka pale ambapo mpango mahususi wa kuanzishwa kwa taifa jipya utakapo kamilika. Hapa ndipo chuki, tamaa pamoja na wivu mbaya unapotawala ambao unaweza kupelekea hata mpango uliokusudiwa kutokamilika ipasavyo.
Lakini chanzo cha haya yote ni nini?
Kuna usemi unasema "Hakuna aliyekamilika ndio maana penseli zina vifutio".