Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Nakuunga mkono kwa asilimia kubwa mfano mfano mzuri series kama Whisper na The last ni drama ambazo zipo underrated Sana na hazijatazamwa na watu wengi lakini ni Kali ile mbaya kuna wakati mpaka nikajiuliza nilikuwapi muda wote kutozijua so hizo rate ni Maoni ya mtu na preference zake mfano mzuri hii ya lee min ho "Pachinko" ni ya kiboya ile mbaya lakini ina rate kubwa.Binafsi njia ninayotumia kupata drama nzuri ni kuangalia story yake kwanza
 
Mkuu njia nyingine ni kucheki Nielsen rating zao ikiwa above 5% huwa lazima iwe Kali hii kwangu ndofilter nayoitumia + baada ya hapo nacheki YouTube previews zake *PIA zile za zamani asianwiki kwa chini huwa ina rating zake www.kpopmap.com/korean-drama-ratings-2020-daily-update/
 
Hii panchiko unajua why imepata ratings kubwa sana?ni kwasababu story yake imetoka kwenye kitabu from one of New york times best selling authors,watu huwa wana notion kuwa movie ikitoka kwenye hizi novel huwa ni best mfano ile movie ya diary of a wimpy kid nayo sijawahi ielewa ila ina ratings kubwa nilifatilia nikaja kukuta imebase kwenye hiyo New york tìmes best selling authors hence lazima tu ratings zitakua kubwa!

 
Hizi script sijui huwa wanaandikiwa na nani tu, yani flow ya maneno iko poa na watu wanaongea points na falsafa za kimaisha. Ukija huku kwetu, mtu anaongea tu ilimradi anaijua lugha husika, muda mwingine mara wachanganye ENGLISH-SWAHILI.
kuna huyu bwana anayetamba kwenye dvd zetu anayeitwa mkojani.

huwezi amini juzi usiku alinifanya nichukue uamuzi usio wa kiungwana kwa kuwazimia televisheni waangaliaji.

jamaa ana kelele kama muongoza mnada wa samaki, kwa uandishi ule wa script bado tuna safari ndefu sana na hatumsaidii yule muigizaji kama tunavyojiaminisha

ukiangalia lugha yetu ina utajiri mkubwa sana wa maneno lakini bado tunashindwa kuitumia fursa hiyo
 
Hahahaa, nimecheka.
 
[emoji16][emoji16][emoji16] una tabia mbaya ndio nini kuwazimia wenzio burudani. Ila yule kaka sijui wanampendea nini, na magari ya mikoani wanampenda kweli
 
Eve nimeimaliza ila imeniachia sikitiko kama ambavyo drama aina zake zinavyoniacha vibaya. Nikifikiria zile familia za maisha halisi zinazopitia shurba za kutapeliwa,kudhulumiwa wazazi kuteswa na kuuliwa,watoto wanabaki wakiwa daah na bado watesaji wakirudishiwa hata robo ya walichokitwnda wanaona wameonewa sana

Wapenzi wa romance humu hamjaachwa nyuma,wapo fireeee
 

Yani Eve natizama kwa uvivu sana ila itaisha tu...
Bloody heart ni motooo, nilimiss historical za dizain hii
 
Bloody heart ni hatari, mle ndani vallain kafanya vyema, ingawa niliangalia episode nne tu (ilikuwa ni ongoing nikaona niisubiri).

Nikitoka kuangalia hii LAST, nitaruka nayo tena.

Mi nilishusha chache alafu sikuitazama siku nimesema niichungulie ah we asubuh ha tunnel ikahusika kumalizia kiporo

Ina vibe flaan hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…