Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Nilikua mlevi wa Korea drama nikapumzika nimekuja kurudi tena kuangalia big mouth aisee nilikua nakosa mambo ,naomba mwenye drama nyengine nzuri anipe za mwaka jana na mwaka huu.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] nimecheka ulivyoelezea ila nahisi kati ya waigizaji wa kibongo usiowapenda mkojani wa kwanza
 
Nilikua mlevi wa Korea drama nikapumzika nimekuja kurudi tena kuangalia big mouth aisee nilikua nakosa mambo ,naomba mwenye drama nyengine nzuri anipe za mwaka jana na mwaka huu.
Cheki hizi ni Kali mno ila si za mwaka Jana wala juzi nazani ni za 2019 na 2018 kama sikosei zinamaudhui ya kama big mouth ni hizi hapa "Whisper" na "Watcher"
 
Kuna siku nitakuja kuwasimulia safari yangu ya kuangalia wakorea ilianzia wapi.

Song ametimiza miaka 51 ya kuzaliwa.
View attachment 2374426
Kwa huku bongo na nchi nyingi za Africa, watu walianza kuwa walevi wa Kdrama baada ya kazi kubwa ya huyu jamaa (JUMONG) moja kati ya kazi ya kikorea zilizoonyeshwa mpaka kwenye mabanda ya video na zikapendwa. Baada ya hiyo watu ndo wakaanza kufuatilia kazi nyingine sasa.

Kiufupi ile kazi ilifungua kwa upana soko la Kdrama katika bara la Africa.
 
Kuna vibe flani huwezi kuzikuta popote zaidi ya kwenye kdrama.

Kuna scene za wazee wa kunywa unakuta team nzima ya kazini imetinga baa ni full kupiga vinywaji unakuta wanatoka wengine wakiwa tungi wanaenda round ya pili kwenye baa nyingine [emoji1316][emoji23][emoji23]
 
Hapo bado hawajaenda karaoke. Humo humo kuna chawa wa boss kalewa chakali na tai yake kichwani kumbe mbwembwe tu akitoka nje kuongea na simu hasa na mkewe unaona kabisa hajalewa hata tone
 
inayofuata nayo nitaifatilia. Family drama tamu sana.
Hiyo drama niliianzaga nikaipenda nikafika hadi ya 10 ila nikawa nna viporo vingi nikairuka kwanza.

Hapa nasubiria Golden Mask wiki ijayo iishe nimalizie ya 90-100

Inayofuata nayo inaonekana ya moto
 
Wenzetu hawana attachment na character na dedication yakufa mtu , Kuna dingi kacheza mkatili itaewon class saizi nimekutana nae kwenye vicenzo ni lawyer wakianza battle na binti yake 🤣🤣🤣🤣mpaka siamini Kama ni yeye wa itaewon
 
Hata mimi drama yangu ya kwanza kuiona ni Jumong ingawa niliangalia katikati tu
 
[emoji16][emoji16][emoji16] au wanaenda karaoke
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…