Ila wakorea wana ajira nyingi za ajabu ajabu. kwenye my daughter seo young nimeona mbaba kapata part-time job ya kwenda msibani kavaa nadhifu akifika nje anapewa hela kwenye bahasha kisha anaelekezwa kwenye msiba husika anatoa pesa hio kama pole pale mlangoni anasaini kitabu cha maombolezo na kuwapa pole wafiwa kisha anaenda kula na kukaa kwa muda aliopangiwa halafu analipwa pesa ya ajira hio. Hii ni kuonyesha msiba umefana kweli kweli
Ya pili akapata ya kwenda harusin kama mualikwa anatakiwa akae upande wa matajiri pasionekane hawana watu,apige makofi,kucheka pale panapotakiwa,msosi autandike wa nguvu mwishoni analipwa. Huyu mbaba akaenda kwenye hio harusi ya machaebol ile maharusi wanaingia akageuka kwa furaha na makofi juu ee kumbe bibi harusi ni binti yake(baba maskini na binti kadanganya kwa wakwe kuwa yeye ni yatima,halafu kwa baba yake alimdanganya anaenda kusoma ulaya)Baba mtu pozi likamuisha akabaki mkiwa hana la kufanya zaidi ya kumalizia part time yake.
Nyingine ya kwenda hotelin kama mgeni na mabegi huku ukisifia uzuri wa vyumba na ubora wa huduma ili kuongeza wateja hotel husika