Kainetics
Senior Member
- Jun 20, 2022
- 135
- 276
Niende moja kwa moja kwenye mada ya kichwa cha uzi. Kadri siku zinavyokwenda idadi ya wanaofanikiwa kufaulu mtihani wa kidato cha nne, ule wa kidato cha sita, wale wanao hitimu mavyuoni ambao mwisho wa siku wanakua waajiriwa au wanajiajiri, au wapo tu mtaani, ni kubwa na inayoendelea kukua.
Ila hawa, ambao walipaswa sasa kuwa walau ndiyo wana ile elimu, kuna mambo bado wanayo ambayo yanatia aibu, unajiuliza sasa huyu ndiyo kasomea nini?
Kama unafaa kwenye kipengele kimoja wapo kati ya hizo hapo juu na unafanya yafuatayo, badilika maana sasa hiyo elimu yako ni sawa na kazi bure.
1. Unalipa kutengenezewa e-mail
Nilikua sijui kama na hiki ni kitu ambacho huwa kipo, hadi jana nikiwa nanunua simu, akaingia mtu dukani kapiga zake nguo za heshima, ana simu nzuri tu mkononi, halafu anamuuliza kijana wa pale, "Kutengeneza email shingapi?" Mie niko nahisi labda ni kama utani fulani, naona anajibiwa "elfu tano email ya kawaida, kumi na tano ya matumizi yote", mbaba wa watu akatoa kumi na tano. halafu anapokea simu na kuanza kuongea kwa misamiati, na misamiati yote hio hujui kufungua email?! Badilika.
2. Unalipia kuwekewe filamu/nyimbo kwenye laptop
Hawa wako wengi, unakuta mtu anachofahamu kwenye laptop ni kutumia Microsoft Word, Excel na PowerPoint. Mbali na hapo ni kubrowse mafile, kuplay muvi na miziki, kucopy na kupaste, basi. Haichukui hata dakika tano kujifunza kudownload audios au videos mwenyewe. Changamsheni ubongo.
3. Unasikiliza "The StoryBook" na kumeza kila kitu kama sahihi 100%
Hii nimekutana nayo na wanawake na wanaume wa umri 40+. Yaani mtu anakaa ananielezea jinsi Michael Jackson alivyouwawa kisa ni Illuminati sijui, au sijui siri ganigani na yuko serious. Muda wote unakua unajitahidi kubana kicheko usije kuwa fired. Kutafuta facts ni muhimu pia. Ukisikia kitu, fanya research ujiridhishe sio kumeza kisa kimeelezewa vizuri kwenye TV.
4. Unaendeshwa kirahisi na 'Watu wa Mungu'
Sikuhizi huko mtaani kuna manabii na mitume kibao, na wana brainwash watu wengi. Inatia huruma na kutisha kidogo kukuta umesoma na bado unaweza kuwa manipulated kirahisi hivyo.
Kwa mambo yanavyoelekea taratibu, dini ndiyo inageuka kuwa aina mpya ya imani potofu. Mchungaji akitaka gari mnamchangia, akitaka nyumba mnamjengea, akiugua anatulia kwanza apone, wewe ukitaka gari, unaenda kumpelekea sadaka ya shukrani akuombee. Unaweka mipango yako sawa, lakini kabla ya kuexecute unaenda sikiliza nabii anasemaje. Hii inatisha.
Nb. Naamini Mungu yupo, na ni muumini mzuri tu. Ila mambo mengine ni ujinga. Yaani mtu na suti yako, kazini uko mkali kwa wafanyakazi wengine halafu Jumapili unaenda kukanyaga mafuta. Badilika.
5. Unaogopa kukiri kuwa hujui kitu fulani
Kuwa na cheti, degree au PhD haimaanishi kuwa basi wewe una akili. Labda una akili, lakini haimaanishi unafahamu kila kitu. Nimekutana watu wengi wengi wanaogopa kukiri, kuwa hawafahamu kitu fulani, au wanaoogopa kuomba msaada wa kawaida kisa ya elimu au wadhifa walio nao. Hii inamaanisha unabaki kwenye sintofahamu milele.
6. Una dharau mtu uliyemzidi elimu
Kuna kitu cha mtu aliyemaliza kidato cha nne kujiona ni superior kwa wenye elimu ya la saba. Au mhitimu wa chuo, kujichanganya na wa kidato cha nne anaona kama haileti maana, kitu ambacho sio kabisa. Wanasema kila mtu unayekutana nae, iwe ni barabarani, msikitni, kanisani au kwenye daladala, ana maisha ameishi toka kazaliwa mpaka pale mlipokutana. Hivyo lazima kuna mambo kibao atakuwa anafahamu ambayo hufahamu na unaweza usifahamu.
Muhesimu kwa hilo peke yake.
Yapo mengine mengi, kwa kifupi tubadilike.
✍ Hizi tender za Sensa zimetoka watu wanaandikiwa application kwenye stationary.
✍ Mtu anaomba kazi hajui andika proposal au kupangilia wasivu wake.
✍ Kujielezea kwa Kingereza walau dakika 5, hata kwenye maandishi ni shughuli.
✍ Unapendelea filamu zilizotafsiriwa halafu hata huyo VJ akikudanganya hata haugundui na subtitle zinaonesha!
Badilikeni, mnatia aibu.
Ila hawa, ambao walipaswa sasa kuwa walau ndiyo wana ile elimu, kuna mambo bado wanayo ambayo yanatia aibu, unajiuliza sasa huyu ndiyo kasomea nini?
Kama unafaa kwenye kipengele kimoja wapo kati ya hizo hapo juu na unafanya yafuatayo, badilika maana sasa hiyo elimu yako ni sawa na kazi bure.
1. Unalipa kutengenezewa e-mail
Nilikua sijui kama na hiki ni kitu ambacho huwa kipo, hadi jana nikiwa nanunua simu, akaingia mtu dukani kapiga zake nguo za heshima, ana simu nzuri tu mkononi, halafu anamuuliza kijana wa pale, "Kutengeneza email shingapi?" Mie niko nahisi labda ni kama utani fulani, naona anajibiwa "elfu tano email ya kawaida, kumi na tano ya matumizi yote", mbaba wa watu akatoa kumi na tano. halafu anapokea simu na kuanza kuongea kwa misamiati, na misamiati yote hio hujui kufungua email?! Badilika.
2. Unalipia kuwekewe filamu/nyimbo kwenye laptop
Hawa wako wengi, unakuta mtu anachofahamu kwenye laptop ni kutumia Microsoft Word, Excel na PowerPoint. Mbali na hapo ni kubrowse mafile, kuplay muvi na miziki, kucopy na kupaste, basi. Haichukui hata dakika tano kujifunza kudownload audios au videos mwenyewe. Changamsheni ubongo.
3. Unasikiliza "The StoryBook" na kumeza kila kitu kama sahihi 100%
Hii nimekutana nayo na wanawake na wanaume wa umri 40+. Yaani mtu anakaa ananielezea jinsi Michael Jackson alivyouwawa kisa ni Illuminati sijui, au sijui siri ganigani na yuko serious. Muda wote unakua unajitahidi kubana kicheko usije kuwa fired. Kutafuta facts ni muhimu pia. Ukisikia kitu, fanya research ujiridhishe sio kumeza kisa kimeelezewa vizuri kwenye TV.
4. Unaendeshwa kirahisi na 'Watu wa Mungu'
Sikuhizi huko mtaani kuna manabii na mitume kibao, na wana brainwash watu wengi. Inatia huruma na kutisha kidogo kukuta umesoma na bado unaweza kuwa manipulated kirahisi hivyo.
Kwa mambo yanavyoelekea taratibu, dini ndiyo inageuka kuwa aina mpya ya imani potofu. Mchungaji akitaka gari mnamchangia, akitaka nyumba mnamjengea, akiugua anatulia kwanza apone, wewe ukitaka gari, unaenda kumpelekea sadaka ya shukrani akuombee. Unaweka mipango yako sawa, lakini kabla ya kuexecute unaenda sikiliza nabii anasemaje. Hii inatisha.
Nb. Naamini Mungu yupo, na ni muumini mzuri tu. Ila mambo mengine ni ujinga. Yaani mtu na suti yako, kazini uko mkali kwa wafanyakazi wengine halafu Jumapili unaenda kukanyaga mafuta. Badilika.
5. Unaogopa kukiri kuwa hujui kitu fulani
Kuwa na cheti, degree au PhD haimaanishi kuwa basi wewe una akili. Labda una akili, lakini haimaanishi unafahamu kila kitu. Nimekutana watu wengi wengi wanaogopa kukiri, kuwa hawafahamu kitu fulani, au wanaoogopa kuomba msaada wa kawaida kisa ya elimu au wadhifa walio nao. Hii inamaanisha unabaki kwenye sintofahamu milele.
6. Una dharau mtu uliyemzidi elimu
Kuna kitu cha mtu aliyemaliza kidato cha nne kujiona ni superior kwa wenye elimu ya la saba. Au mhitimu wa chuo, kujichanganya na wa kidato cha nne anaona kama haileti maana, kitu ambacho sio kabisa. Wanasema kila mtu unayekutana nae, iwe ni barabarani, msikitni, kanisani au kwenye daladala, ana maisha ameishi toka kazaliwa mpaka pale mlipokutana. Hivyo lazima kuna mambo kibao atakuwa anafahamu ambayo hufahamu na unaweza usifahamu.
Muhesimu kwa hilo peke yake.
Yapo mengine mengi, kwa kifupi tubadilike.
✍ Hizi tender za Sensa zimetoka watu wanaandikiwa application kwenye stationary.
✍ Mtu anaomba kazi hajui andika proposal au kupangilia wasivu wake.
✍ Kujielezea kwa Kingereza walau dakika 5, hata kwenye maandishi ni shughuli.
✍ Unapendelea filamu zilizotafsiriwa halafu hata huyo VJ akikudanganya hata haugundui na subtitle zinaonesha!
Badilikeni, mnatia aibu.